Msanii Akothee Afunguka Kuhusu Mipango Yake ya Mazishi

Msanii Akothee Afunguka Kuhusu Mipango Yake ya Mazishi

Mwanamuziki kutoka Kenya, Akothee, ameibua gumzo mitandaoni baada ya kutoa tamko jipya kuhusu mipango yake ya mazishi. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, ameeleza kuwa hataki chakula chochote kipikwe siku ya mazishi yake, akisisitiza kuwa watu wanaohudhuria wanapaswa kubeba chakula chao kutoka nyumbani badala ya kutegemea familia yake. Akothee amehoji ni vipi watu wanaweza kumudu kula kwenye mazishi, akiongeza kuwa yeyote anayetaka kula siku hiyo anapaswa kuchangia gharama mapema na kula nyumbani kwao. Mwanamama huyo, amesema wazi kuwa hafurahishwi na utamaduni wa baadhi ya watu kutumia mazishi kama fursa ya kula na kunywa badala ya kutoa heshima kwa marehemu. Kauli yake inakuja siku chache baada ya kueleza kuwa atakapoaga dunia angependa kuzikwa ndani ya saa 48, bila kujali mahali atakapofia, akisisitiza kuwa hataki mchakato wa mazishi wake ucheleweshwe.

Read More
 Juma Jux Ampongeza Diamond kwa Kufungua Milango ya Kimataifa kwa Wasanii wa Bongo

Juma Jux Ampongeza Diamond kwa Kufungua Milango ya Kimataifa kwa Wasanii wa Bongo

Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Juma Jux, amempongeza Diamond Platnumz kwa mchango wake mkubwa katika kufungua njia za kimataifa kwa wasanii wa Tanzania. Akizungumza katika mahojiano na El Mando TZ, Jux amesema kuwa Diamond ameonyesha mfano wa kuigwa kupitia matamasha yake makubwa aliyoandaa nchini Uingereza, ikiwemo London, Manchester na Glasgow mwezi Julai, ambayo yalitoa fursa kwa muziki wa Tanzania kufika hadhira ya kimataifa. Jux amesisitiza kuwa hatua kama hizo ni muhimu katika kuinua tasnia ya muziki wa Bongo Fleva, hasa pale msanii mmoja anapowapa nafasi wenzao kupata exposure kupitia majukwaa ya kimataifa. Jux ametolea mfano wasanii wa Nigeria ambao wanapoenda kufanya maonesho barani Ulaya, kama vile katika ukumbi wa O2 Arena, huwa hawasahau kuwashirikisha wasanii wenzao wa nyumbani. Hata hivyo amesema kuwa ni muhimu kwa wasanii wa Tanzania pia kuendeleza utamaduni huo wa kusaidiana, ili kuhakikisha muziki wa Bongo Fleva unaendelea kupanuka na kushindana kimataifa.

Read More
 Msanii Sanaipei Tande Aonya Dhidi ya Mahusiano ya Kifedha

Msanii Sanaipei Tande Aonya Dhidi ya Mahusiano ya Kifedha

Mwanamuziki na mtangazaji wa Kenya, Sanaipei Tande, ameeleza kuwa mahusiano ya kweli yanapaswa kujengwa juu ya urafiki na ushirikiano badala ya kuzingatia kile mtu analeta mezani. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni, Sanaipei ameeleza kuwa watu wengi wa kizazi cha sasa (GenZ) wamepoteza maana halisi ya uhusiano kutokana na kuangalia zaidi masuala ya kifedha na faida binafsi. Anasema kuwa uhusiano wa kudumu unahitaji mawasiliano, urafiki, na msaada wa kihisia na kiroho kati ya wawili wanaopendana. Msanii huyo, anayefahamika kwa nyimbo kama Amina na Najuta, ameongeza kuwa urafiki ndio msingi wa uelewano wa kweli katika mahusiano, kwani hutoa nafasi kwa watu kujifunza na kuelewana kabla ya kuchukua hatua kubwa zaidi. Kauli ya Sanaipei imepokelewa kwa hisia tofauti mitandaoni, wengi wakimsifu kwa kuzungumzia ukweli kuhusu changamoto za mahusiano ya kisasa.

Read More
 Mwanaume wa Kenya Afichua Alimdanganya Mkewe kwa Mwaka Akijifanya Eric Omondi

Mwanaume wa Kenya Afichua Alimdanganya Mkewe kwa Mwaka Akijifanya Eric Omondi

Mwanaume mwenye sura inayofanana na mchekeshaji wa Kenya, Eric Omondi, amekiri kuwa aliishi katika uhusiano wa kimapenzi kwa mwaka mmoja akijifanya kuwa yeye ndiye mchekeshaji huyo halisi. Kwa mujibu wa mahojiano yaliyosambaa mtandaoni, amesema kuwa alikutana na mwanamke huyo mtandaoni na wakaanza mahusiano, huku akitumia umaarufu wa Eric Omondi kumvutia na kumfanya aamini kuwa anachumbiana na staa huyo. Mwanaume huyo amesema kwa muda wa mwaka mmoja, alidumisha uongo huo kwa kutumia picha na video za Eric Omondi mitandaoni, jambo lililomfanya mwanamke huyo asiwe na shaka. Baada ya muda, ukweli ulifichuka na mpenzi wake kugundua kuwa alikuwa akiishi na mtu tofauti kabisa. Mwanaume huyo amekiri kosa hilo akisema kuwa hakupanga kumuumiza mwanamke huyo, bali alijikuta akizama zaidi katika uongo huo kutokana na hofu ya kumpoteza. Amesema alianza kama mzaha, lakini baadaye mambo yakachukua mwelekeo tofauti.

Read More
 Nandy Afunguka Sababu za Kutumia AI Kwenye Video ya Sweety

Nandy Afunguka Sababu za Kutumia AI Kwenye Video ya Sweety

Msanii nyota wa Bongo Fleva, Nandy, amefunguka sababu kuu ya kutumia teknolojia ya Artificial Intelligence (AI) katika utayarishaji wa video ya wimbo wake uitwao Sweety aliomshirikisha Jux, akisema hatua hiyo ilikuwa ya kulinda ndoa na heshima za kifamilia. Kwenye mahojiano hivi karibuni, Nandy amesema wazo la kutumia AI lilitokana na tahadhari baada ya kutambua kuwa baadhi ya mashabiki wanaweza kutafsiri vibaya maudhui ya video hiyo endapo wangeonekana pamoja katika baadhi ya sehemu zenye hisia za kimahaba. Amesema kama msanii aliyeolewa, anapaswa kuwa makini na aina ya kazi anazofanya ili kuepuka kuzua tafsiri zisizofaa kwa mume wake na mashabiki wake. Aidha, Nandy ameeleza kuwa teknolojia ya AI imesaidia kufanikisha video yenye ubora wa kimataifa bila wao kuhitaji kuigiza kwa pamoja. Hatua hiyo pia imeonyesha namna muziki wa Afrika Mashariki unavyoweza kutumia ubunifu wa kisasa kutatua changamoto za kijamii bila kuathiri ubora wa kazi za sanaa.

Read More
 Willy Paul Alalamikia Mashabiki Kutompa Heshima Anazostahili

Willy Paul Alalamikia Mashabiki Kutompa Heshima Anazostahili

Staa wa muziki kutoka nchini Kenya, Willy Paul, ameelezea masikitiko yake kuhusu jinsi mashabiki wa muziki wa Kenya wanavyomchukulia poa, akidai kuwa licha ya mafanikio yake makubwa kimataifa, bado hatambuliwi ipasavyo nyumbani. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, msanii huyo amesema kuwa yeye ndiye msanii pekee wa Kenya ambaye nyimbo zake zinachezwa zaidi kimataifa kuliko za wasanii wengine wengi, lakini mashabiki wa ndani wanapuuzia juhudi zake. Willy Paul amesisitiza kuwa ukweli unabaki kuwa yeye ndiye msanii anayejulikana zaidi nje ya nchi na anaamini kuwa muda utakuja ambapo mashabiki wa nyumbani watatambua thamani ya kazi zake. Kauli yake imekuja baada ya content creator wa mitandaoni Ruth K kumtaja kama msanii wa kimataifa anayepaswa kupewa heshima zaidi kutokana na ushawishi wake nje ya mipaka ya Kenya.

Read More