Sports news

IOC Yapiga Marufuku Wanawake Waliobadili Jinsia Kushiriki Mashindano ya Wanawake

IOC Yapiga Marufuku Wanawake Waliobadili Jinsia Kushiriki Mashindano ya Wanawake

Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki, IOC, imechukua hatua kubwa ya kupiga marufuku wanawake waliobadili jinsia kushiriki katika mashindano ya wanawake katika michezo yote.

Kinara wa IOC, Kirsty Coventry, ambaye ni mwogeleaji wa zamani na mshindi wa medali saba za Olimpiki, amethibitisha kuwa hatua hii ni sehemu ya kampeni yake ya uchaguzi. Marufuku hiyo inaweza kutangazwa rasmi mapema mwaka ujao.

Coventry ameeleza kuwa IOC itachukua jukumu kuu katika mijadala kuhusu hustahiki wa jinsia katika michezo, ikilenga kuhakikisha usawa katika mashindano ya wanawake.

Kwa upande mwingine, Marekani tayari imechukua hatua kama hiyo. Mwezi Februari, Rais wa Marekani Donald Trump alitia saini amri ya utendaji inayowazuia wanawake waliobadili jinsia kushindana katika mashindano ya wanawake, ikiwemo Michezo ya Olimpiki ya Los Angeles mwaka 2028. Wanariadha waliobadili jinsia watakaotaka kuingia Marekani kushiriki katika michezo hiyo hawatapewa visa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *