Ivory Coast na Algeria Zatinga Robo Fainali AFCON 2025

Ivory Coast na Algeria Zatinga Robo Fainali AFCON 2025

Timu ya Taifa ya Ivory Coast, maarufu kama The Elephants, imefanikiwa kutinga hatua ya robo fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2025) baada ya kuibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Burkina Faso katika mchezo wa hatua ya 16 bora. Katika mchezo huo, Ivory Coast ilionyesha ubora mkubwa tangu mwanzo, ambapo Amad Diallo alifungua ukurasa wa mabao dakika ya 20. Yan Diomande aliongeza bao la pili dakika ya 32, kabla ya mchezaji wa akiba Bazoumana TourΓ© kufunga bao la tatu dakika ya 87 na kukamilisha ushindi huo mnono kwa The Elephants. Wakati huo huo, Timu ya Taifa ya Algeria nayo imefuzu robo fainali baada ya kuiondoa DR Congo kwa ushindi wa bao 1-0 katika mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa na wa kusisimua. Mchezo huo ulimalizika bila mabao ndani ya dakika 90 za kawaida, hali iliyosababisha kuchezwa kwa muda wa nyongeza. Bao la ushindi kwa Algeria lilifungwa na mchezaji wa akiba Adil Boulbina dakika ya 119 ya mchezo, kwa shuti kali lililowashangaza walinzi na kipa wa DR Congo, na kuwapeleka The Desert Foxes hatua ya nane bora. Kutokana na matokeo hayo, Ivory Coast sasa itavaana na Egypt katika mchezo wa robo fainali, huku Algeria ikitarajiwa kupambana vikali na Nigeria. Mechi hizo za robo fainali zinatarajiwa kuchezwa Jumamosi.

Read More
 Nigeria na Misri Zatinga Robo Fainali AFCON 2025

Nigeria na Misri Zatinga Robo Fainali AFCON 2025

Timu ya Taifa ya Nigeria, maarufu kama Super Eagles, imefanikiwa kutinga robo fainali ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON 2025) baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Msumbiji katika hatua ya 16 bora. Kwa matokeo hayo, Nigeria sasa inasubiri mshindi wa mchezo mwingine wa hatua ya 16 bora kati ya Algeria na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ili kujua wapinzani wao kwenye robo fainali. Wakati huo huo, Timu ya Taifa ya Misri, maarufu kama Mafarao, nayo imejikatia tiketi ya robo fainali baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3–1 dhidi ya Benin katika muda wa ziada. Mchezo huo ulikuwa umemalizika kwa sare ya bao 1–1 ndani ya dakika 90 za kawaida kabla ya Misri kuonyesha ubora wake katika dakika za nyongeza. Kwa matokeo hayo, Misri sasa itakutana na mshindi wa mchezo wa hatua ya 16 bora kati ya Ivory Coast na Burkina Faso katika robo fainali. Kwa sasa, mashabiki wa soka barani Afrika wanasubiri kwa hamu kuona nani atajiunga na Nigeria na Misri katika hatua ya robo fainali ya AFCON 2025, hatua ambayo mara nyingi huamua mustakabali wa timu kuelekea kutwaa taji.

Read More