Azziad Nasenya Awasilisha Kesi Kuzuia Mnada wa Nyumba Yake Kileleshwa
Mwanamitindo na mtangazaji wa redio, Azziad Nasenya, amewasilisha kesi katika Mahakama ya Biashara jijini Nairobi akiomba kusitishwa kwa mnada uliopangwa kufanywa dhidi ya nyumba yake ya kifahari iliyoko Kileleshwa, Nairobi. Kulingana na hati za mahakama, Azziad anasema yuko katika hatari ya kupoteza mali hiyo licha ya kwamba tayari amekamilisha kulipa deni lote la mkopo aliochukua kupitia mpango wa kifedha wa mortgage kutoka kwa chama cha akiba na mikopo (SACCO) kinachoruhusiwa kukusanya amana. Azziad anadai kuwa taasisi hiyo ya kifedha imeanza mchakato wa kurejesha mkopo mzima kinyume cha makubaliano ya awali, na hata kutoa maagizo kwa mnada ili kuuza nyumba hiyo inayokadiriwa kuwa na thamani ya takribani shilingi milioni 20.3. Kupitia ombi lake kwa mahakama, mjasiriamali huyo wa kidijitali anataka zuio la muda liwekwe dhidi ya mnada huo akisema hatua hiyo ni ya kinyume cha sheria na ya mapema mno, kwani hana deni lolote lililobaki. Kesi hiyo sasa inasubiri kusikilizwa huku mashabiki wakionyesha kumuunga mkono mrembo huyo ambaye amejizolea umaarufu mkubwa kupitia kazi zake katika mitandao ya kijamii na vyombo vya habari.
Read More