Gloria Bugie Akiri Mwili Wake Sio Hekalu la Mungu

Gloria Bugie Akiri Mwili Wake Sio Hekalu la Mungu

Msanii wa muziki kutoka Uganda, Gloria Bugie, amezua mjadala mpana baada ya kukiri wazi kuwa mwili wake sio hekalu la Mungu, akisema amefanya dhambi nyingi katika maisha yake ya nyuma. Gloria Bugie amesema kuwa amewahi kuingia katika mahusiano ya kimapenzi na watu wenye ushawishi mkubwa ndani ya tasnia ya burudani. Kwa mujibu wake, mahusiano hayo yalichangia kwa kiasi kikubwa kufunguka kwa milango ya fursa, hususan kupata mikataba mikubwa ya kazi, tofauti na mafanikio aliyoyapata kupitia muziki wake pekee. Amesema kuwa wakati huo alifanya maamuzi ambayo hakuyapima kwa misingi ya imani au maadili, akieleza kuwa alikuwa akitafuta njia za haraka za kufanikiwa na kujijenga kimaisha. Gloria Bugie ameongeza kuwa hakujiona kama alikuwa anajidharau, bali alikuwa akifanya kile alichoona ni njia ya kujinusuru katika mazingira magumu ya ushindani mkubwa kwenye tasnia. Hata hivyo, kauli hizo zimeibua hisia mseto miongoni mwa watumiaji wa mitandao ya kijamii, ambapo baadhi wamempongeza kwa ujasiri wa kusema ukweli wake bila kuficha, huku wengine wakimkosoa vikali wakidai kauli hizo zinaweza kuhamasisha mmomonyoko wa maadili, hasa kwa vijana.

Read More
 Msanii wa Uganda Glorie Bugie Akataa Shinikizo la Kuzaa Watoto

Msanii wa Uganda Glorie Bugie Akataa Shinikizo la Kuzaa Watoto

Msanii chipukizi kutoka Uganda, Glorie Bugie, amesema kwa sasa hataki kabisa kusikia masuala ya kuzaa watoto, akibainisha kuwa kipaumbele chake kikubwa ni kuijenga na kuikuza taaluma yake ya muziki. Akizungumza kwenye moja ya Interview, Glorie Bugie amesema kuwa bado ana ndoto nyingi za kimuziki anazotaka kutimiza, ikiwemo kutoa kazi zenye ubora wa kimataifa na kupeperusha vyema bendera ya Uganda na Afrika Mashariki kwa ujumla. Mrembo huyo amesisitiza kuwa kwa sasa muda na nguvu zake zote anazielekeza kwenye muziki, si masuala ya familia. Kauli hiyo ya Glorie Bugie imekuja mara baada ya kushinda tuzo ya Msanii Bora wa Kike Afrika Mashariki katika tuzo za Zikomo Awards, hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Read More
 Gloria Bugie Ashinda Tuzo ya Msanii Bora wa Kike Afrika Mashariki

Gloria Bugie Ashinda Tuzo ya Msanii Bora wa Kike Afrika Mashariki

Nyota wa muziki anayechipukia kwa kasi kutoka nchini Uganda, Gloria Bugie, ameibuka mshindi wa tuzo ya Msanii Bora wa Kike Afrika Mashariki (Best Female Artist East Africa) katika kilele cha tuzo za Zikomo Africa Awards 2025. Akizungumza kwa hisia kali mara baada ya kupokea tuzo hiyo jukwaani, Bugie hakuweza kuficha furaha yake, akitoa shukrani za dhati kwa Mwenyezi Mungu pamoja na mashabiki wake kwa kumuwezesha kufikia mafanikio hayo makubwa ndani ya kipindi kifupi cha safari yake ya muziki. Tuzo hizo zilizofanyika usiku wa kuamkia leo jijini Dar es Salaam, zimeshuhudia Gloria Bugie akiweka historia baada ya kuwashinda wapinzani wakubwa na wenye majina mazito katika kiwanda cha muziki wa ukanda huu. Katika kipengele hicho kilichokuwa na ushindani mkali, Bugie aliwabwaga wasanii wenye ushawishi mkubwa akiwemo Spice Diana (Uganda), Abigail Chams na Phina kutoka Tanzania, pamoja na Nikita Kering wa Kenya.

Read More
 Gloria Bugie Akana Madai ya Kuchumbiana na Wanaume Walio kwenye Ndoa

Gloria Bugie Akana Madai ya Kuchumbiana na Wanaume Walio kwenye Ndoa

Msanii wa muziki kutoka Uganda, Gloria Bugie, ameweka wazi msimamo wake kuhusu mahusiano, akisema kwa uthabiti kwamba hatawahi kuchumbiana na mwanaume aliye kwenye ndoa. Akipiga stori na kituo kimoja cha habari, Gloria amedai kuwa hajawahi kuwa kwenye uhusiano wa aina hiyo, na kwamba anajithamini kiasi cha kutoshiriki mwanaume na mwanamke mwingine. Amesema kuwa wanaume walio kwenye ndoa wamekuwa wakimtumia ujumbe mara kwa mara kupitia mitandao ya kijamii, lakini hana nia kabisa ya kutoka nao kimapenzi. Gloria Bugie ameongeza kuwa kwa sasa ameelekeza nguvu na muda wake wote kwenye muziki, na anataka kujenga taswira inayojikita kwenye kazi na si tetesi za mitandaoni. Hitmaker huyo wa ngoma ya Chikicha, amesisitiza kwamba maisha anayoyaishi ni matokeo ya kazi yake na sio misaada kutoka kwa mwanaume aliye kwenye ndoa kama inavyodaiwa. Kauli yake imekuja kufuatia madai yaliyosambaa mitandaoni yakimhusisha na uhusiano na wanaume wa watu kutokana na maisha yake ya kifahari.

Read More