Juma Lokole Amlalamikia Wema Sepetu kwa Kukimbia Dili la Kazi

Juma Lokole Amlalamikia Wema Sepetu kwa Kukimbia Dili la Kazi

Mdau wa masuala ya burudani, Juma Lokole, ameonyesha maumivu na masikitiko makubwa kufuatia kitendo cha muigizaji maarufu Wema Sepetu kudaiwa kukimbia kazi waliyokuwa wamekubaliana. Akizungumza kwa uchungu, Juma amesema alimpa Wema dili la kazi baada ya makubaliano yote kukamilika ikiwemo kukubali kiwango cha malipo na kukatiwa tiketi ya ndege kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo. Hata hivyo, anadai kuwa muigizaji huyo aliingia mitini dakika za mwisho bila kutoa maelezo yoyote ya kuridhisha. Kwa mujibu wa Juma, kilichomuudhi zaidi ni taarifa kwamba Wema alichagua kuthamini masuala ya mapenzi kuliko kazi, jambo alilodai ni kukosa weledi na kujituma kazini. Anasema alimheshimu Wema kama msanii mkubwa, jambo lililomfanya kumpa imani kubwa, lakini matokeo yakawa tofauti na matarajio yake.

Read More
 Juma Lokole Atoboa Siri Nzito Kuhusu Wemasepetu,

Juma Lokole Atoboa Siri Nzito Kuhusu Wemasepetu,

Mdau wa masuala ya burudani, Juma Lokole, amezua mjadala mpana mitandaoni baada ya kudai kuwa Wema Sepetu aliwahi kuwa katika mahusiano ya kimapenzi na mfanyabiashara tajiri anayefahamika kwa jina la MO. Akizungumza kupitia Instagram yake, Juma Lokole amesema licha ya madai hayo, Wema aliweza kuficha siri za mahusiano yake na hakuwahi kuanika mambo ya ndani hadharani, hali ambayo imemsaidia kulinda heshima yake katika jamii. Kutokana na hilo, Juma Lokole amemtaka Rita, Mrembo anadaiwa kutoka kimapenzi Diamond, kuiga mfano wa Wema Sepetu kwa kuacha tabia ya kusambaza siri za mahusiano mitandaoni. Amesema badala ya kelele na lawama, Rita anapaswa kutumia fursa anazopata katika mahusiano kujijenga kiuchumi na kimaendeleo. Kwa mujibu wa Juma Lokole, mahusiano yanaweza kuwa daraja la kuboresha maisha ya wanawake endapo yatatumika kwa busara, nidhamu na hekima, huku akisisitiza kuwa kuanika siri hadharani kunaharibu taswira ya mwanamke na kunapunguza fursa za wanaume kumchumbia.

Read More
 Juma Lokole Asema Ritha Hana Mvuto wa Kumfanya Diamond Kumuacha Zuchu

Juma Lokole Asema Ritha Hana Mvuto wa Kumfanya Diamond Kumuacha Zuchu

Mdau wa burudani Juma Lokole amtolea uvivu mrembo Ritha, akisema hana uwezo wa kuvunja uhusiano wa kimapenzi kati ya Diamond Platnumz na Zuchu. Akizungumzia sakata hilo, Juma Lokole amesema wazi kuwa Ritha hana uzuri wala mvuto wa kumfanya Diamond kumuacha Zuchu, akisisitiza kuwa penzi la wawili hao lipo imara na halitetereki kwa tetesi au maneno ya mitandaoni. Lokole amedai kuwa endapo Ritha anadhani kuvujisha sauti au taarifa zinazodaiwa kumhusisha na Diamond kunaweza kuharibu au kusambaratisha mahusiano ya wawili hao, basi ajue hilo halitowezekana. Aidha, Juma Lokole amemwonya Ritha kuacha tabia ya kuvujisha sauti au siri za watu, akisema mwenendo huo unaweza kumharibia mustakabali wa mahusiano yake, kwani wanaume wengi wanaweza kumuogopa kwa kuhofia siri zao kuwekwa hadharani. Kauli ya Juma Lokole imekuja baada ya Ritha ambaye anadaiwa kutoka kimapenzi na Diamond kumtolea Diamond na Zuchu maneno mazito, ambapo alienda mbali zaidi na kudai Diamond amekuwa akimtaka kimapenzi kwa siri na hata kuwatuma baadhi ya ndugu zake kumshawishi ili warudiane.

Read More