MC Pilipili Azikwa katika Makaburi ya Kilimo Kwanza, Dodoma

MC Pilipili Azikwa katika Makaburi ya Kilimo Kwanza, Dodoma

Mchekeshaji na mshereheshaji wa matukio Emmanuel Mathias Matebe, maarufu kama MC Pilpili, amepumzishwa kwenye nyumba yake ya milele katika makaburi ya Kilimo Kwanza jijini Dodoma leo, Novemba 20, 2025. Mamia ya waomboleza, wakiwemo wasanii, ndugu, marafiki na viongozi wa dini, walijitokeza kumuaga mchekeshaji huyo aliyekuwa akipendwa na wengi kutokana na kipaji chake cha kuiburudisha jamii. MC Pilpili, ambaye pia alijulikana kwa mchango wake katika tasnia ya filamu na uigizaji, ameacha pengo kubwa katika burudani ya Tanzania. Waomboleza waliohudhuria mazishi yake walimkumbuka kama mtu mcheshi, mnyenyekevu na mwenye uwezo wa kuleta tabasamu nyusoni mwa watu katika nyakati zote. MC Pilpili aliuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana Jumapili ya Novemba 16, 2025 akiwa jijini Dodoma. Tukio hilo lilisababisha simanzi kubwa nchini Tanzania, huku mashabiki na wadau wa sanaa wakishinikiza haki itendeke na wahusika wafikishwe mbele ya sheria. Jeshi la Polisi limeendelea na uchunguzi kuhusu mauaji hayo, likikusanya vielelezo na ushahidi ili kubaini watu waliohusika. Maafisa wa upelelezi wamesema kuwa jitihada za kusaka wahalifu zinaendelea kwa kasi na umma utaarifiwa pindi hatua muhimu zitakapofikiwa.

Read More
 Jeshi la Polisi Thibitisha Kifo cha Mchekeshaji Maarufu MC Pilpili

Jeshi la Polisi Thibitisha Kifo cha Mchekeshaji Maarufu MC Pilpili

Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma limethibitisha kifo cha mchekeshaji maarufu wa Tanzania MC Pilpili anayefahamika kama Emmanuel Mathias Matebe, kilichotokea Novemba 16, 2025 katika Kituo cha Afya Ilazo jijini Dodoma. Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, ACP William Mwanafupa, amesema marehemu alifikishwa kituoni hapo majira ya mchana akiwa katika hali mbaya na alifariki muda mfupi baada ya kuanza kupatiwa matibabu. Mwanafupa ameeleza kuwa watu watatu waliokuwa kwenye gari ndogo nyeupe walimkabidhi marehemu kwa msaidizi wake, bila kueleza kilichotokea, kisha wakatoweka mara moja. Amesema msaidizi huyo ndiye aliyemkimbiza Marehemu katika kituo cha afya kwa ajili ya huduma za dharura. Aidha amesema uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa MC Pilpili alishambuliwa na watu wasiojulikana, na majeraha aliyopata sehemu mbalimbali za mwili yanasadikiwa kuwa chanzo cha kifo chake. Hata hivyo amesema uchunguzi unaendelea ili kubaini mazingira ya tukio na kuwatambua wahusika.

Read More