Nairobi United Itashuka Dimbani Dhidi ya Azam Jumapili

Nairobi United Itashuka Dimbani Dhidi ya Azam Jumapili

Nairobi United itashuka dimbani Jumapili hii dhidi ya Azam FC ya Tanzania kwenye mechi ya hatua ya makundi ya Kombe la Mashirikisho katika Uwanja wa Taifa wa Nyayo. Nai Boys, ambao wanashiriki kwa mara ya kwanza katika michuano ya bara Afrika, wanatafuta ushindi wao wa kwanza baada ya matokeo mchanganyiko katika mechi mbili za ufunguzi. Walifungua kampeni kwa ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Wydad Casablanca ya Morocco, kisha wakafungwa bao 1-0 nyumbani na AS Maniema Union ya Kongo. Kwa upande wa Azam FC, kampeni yao ya makundi imekuwa ngumu. Walichapwa mabao 2-0 ugenini na AS Maniema Union, kisha wakafungwa bao 1-0 nyumbani na Wydad Casablanca. Safari ya Nairobi United kufika hatua ya makundi iliandikwa kama historia, baada ya kuibandua Etoile du Sahel ya Tunisia kwa jumla ya mabao 7-6 kupitia mikwaju ya penalti, kufuatia sare ya mabao 2-2 katika raundi ya pili ya mchujo. Azam FC nao walifuzu kwa kishindo baada ya kuiondoa KMKM kwa jumla ya mabao 9-0.

Read More
 Nairobi United Kutafuta Heshima kwenye Kombe la Shirikisho Afrika

Nairobi United Kutafuta Heshima kwenye Kombe la Shirikisho Afrika

Timu ya ligi kuu ya FKF, Nairobi United, imetengwa katika kundi B la michuano ya kuwania Kombe la Mashirikisho barani Afrika (CAF Confederation Cup) kufuatia droo iliyoandaliwa jana jioni jijini Johannesburg, Afrika Kusini. Nairobi United itakuwa na kibarua kigumu kwani itachuana na Azam FC kutoka Tanzania, AS Maniema Union ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, pamoja na Wydad Casablanca, miamba wa soka kutoka Morocco. Michuano hiyo inatarajiwa kuanza rasmi tarehe 21 mwezi huu, huku awamu ya mwondoano (knockout stage) ikipangwa kuanza tarehe 13 Machi 2026. Katika droo hiyo, kundi A linajumuisha USM Alger (Algeria), Djoliba AC (Mali), OC Safi (Morocco) na San Pedro (Côte d’Ivoire). Kundi C linaundwa na CR Belouizdad, Stellenbosch FC, AS Otoho na Singida Fountain Gate kutoka Tanzania. Kundi D, linalotajwa kuwa la “mauti”, linashirikisha Zamalek, Al Masry, Kaizer Chiefs, na Zesco United. Kwa mujibu wa kanuni za mashindano, timu mbili bora kutoka kila kundi zitafuzu kwa hatua ya robo fainali, zikifungua ukurasa mpya wa mchuano wa kusaka taji la heshima la klabu bingwa wa Kombe la Shirikisho barani Afrika.

Read More