
Ikiwa ni miezi miwili imepita tangu kuachiwa kwa album ya The African Experience ya Staa muziki nchini Willy Paul, album hiyo inaendela kufanya vizuri kwenye mtandao wa Audio Mack.
Mpaka sasa album hiyo imesha sikiliza zaidi ya mara milioni moja na kuifanya kuwa album iliyosikilizwa zaidi kwenye mtandao huo nchini ndani ya muda mfupi tangu itoke rasmi.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Willy Paul amewashukuru mashabiki zake kwa kuendelea kufuatilia kazi zake ambazo zimeonyesha mafanikio makubwa ndani ya kipindi cha muda mfupi.
Ikumbukwe album ya “The African Experience” kutoka kwa mtu mzima Willy Paul iliachiwa rasmi Oktoba 21 mwaka huu ikiwa na jumla ya mikwaju 17 ya moto.