
Rapa kutoka Marekani, Dababy ameonekana Nigeria akiwa pamoja na Davido ambaye ndiye kama mwenyeji wake nchini humo.
Wawili hao walionekana wakizunguka katika mitaa mbalimbali ya Jiji la Lagos, huku kila mmoja akishare baadae video wakiwa pamoja kupitia mitandao yao ya kijamii.
Aidha, Dababy ametumia ukurasa wake wa Instagram kumshukuru Davido kwa kumfanya ajisikie yupo nyumbani.
“Davido amenifanya nijisikie kama nipo nyumbani ”, Ameandika Dababy.
Utakumbuka Dababy ametua nchini Nigeria akitokea Ujerumani, ambapo yupo nchini humo kwa ajili ya kukamilisha video ya collabo yake na Davido.