Entertainment

MENEJA WA 001 MUSIC AKANUSHA HAPPY C KUUZA GARI KISA KUTOSWA NA JOHO

MENEJA WA 001 MUSIC AKANUSHA HAPPY C KUUZA GARI KISA KUTOSWA NA JOHO

Meneja kutoka lebo ya muziki ya 001 Music Mangisi amepuzilia mbali madai ya msanii Happy C kuuza gari lake baada ya walimwengu kuhoji ametoswa na bosi wa lebo hiyo Hassan Joho.

Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Mangisi amesema madai hayo hayana ukweli wowote kwani happy c bado anaendelea kupata msaada kutoka kwa gavana huyo wa zamani wa kaunti ya mombasa.

Mangisi amekazia kuwa kuondoka kwa Hassan Joho mamlakani hautamrudisha nyuma kimuziki msanii Happy C kwa sababu ana imani kuwa Joho atamsaidia hata akiwa nje ya siasa.

Kauli yake imekuja mara baada ya walimwengu kwenye mitandao ya kijamii kudai kuwa huenda Happy C ameuza gari lake kwani mara kwa mara amekuwa akitumia usafiri wa boda boda kwenye shughuli zake.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *