LifeStyle

AKOTHEE ALAZWA HOSPITALI BAADA YA KUUGUA GHAFLA

AKOTHEE ALAZWA HOSPITALI BAADA YA KUUGUA GHAFLA

Staa wa muziki ambaye pia ni mfanyabiashara nchini Akothee amelazwa hospitali kwa mara nyingine mara baada ya kuugua ghafla.

Akothee ameweka wazi hilo kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kusema kwamba alikimbizwa hospitali Disemba 11 alipougua ghafla nyumbani kwake.

Hitmaker huyo wa “Sweet Love”  amesema ameshindwa kubaini maradhi yanayomsibu ila kwa sasa ni mwingi wa shukrani kwani ameanza kupata afueni.

Bosi huyo wa Akothee Safaris ametambua mchango wa mpenzi wake Nelly Oaks ambaye amesimama nae mara tano hospitali alipokuwa amelazwa hospitalini.

Wiki iliyopita binti yake Rue Baby alilazimika kuahirisha hafla ya kufuzu kwake kutoka chuo kikuu baada ya Akothee kulazwa tena hospitalini.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *