Akothee Akataa Wahudumu wa Benki Wanawake kwa Madai ya Kukiuka Faragha

Akothee Akataa Wahudumu wa Benki Wanawake kwa Madai ya Kukiuka Faragha

Mwanamuziki, Akothee, ameeleza wazi kutoridhishwa kwake na namna baadhi ya wahudumu wa benki nchini Kenya, hasa wanawake, wanavyomhudumia. Kupitia kurasa zake za kijamii, Akothee amesema kuwa kuanzia mwaka 2026 hataki kuhudumiwa na wahudumu wa benki wanawake. Amedai kuwa baadhi yao wamekuwa wakimuonesha kukosa weledi wanapokutana naye kazini. Amesema kuwa mara nyingi anapoingia benki, baadhi ya wahudumu huanza kwa kumweleza jinsi wanavyomfuatilia mitandaoni na namna anavyowapa motisha, jambo ambalo halimfurahishi. Aidha, amelalamika kuhusu ukiukwaji wa faragha akidai kuwa baadhi ya wahudumu wamekuwa wakimtambulisha kwa wateja wengine kama msanii maarufu. Kwa mujibu wake, hali hiyo humfanya ajisikie dhaifu na kukosa usalama. Hata hivyo, amesema kuwa amekuwa akipendelea kuhudumiwa na wahudumu wa kiume, akisema changamoto kubwa aliyowahi kukumbana nayo ni kupigiwa simu nje ya saa za kazi, jambo ambalo alikomesha mara moja.

Read More
 Akothee Amjibu Shabiki Aliyedai Alimpotezea Nelly Oaks Muda

Akothee Amjibu Shabiki Aliyedai Alimpotezea Nelly Oaks Muda

Mwanamuziki na mfanyabiashara Akothee amemjibu kwa hasira shabiki aliyetoa maoni mtandaoni akidai kuwa alimharibia aliyekuwa mpenzi wake wa zamani, Nelly Oaks, muda wa ujana wake na kumtaka atafute mke ili asalie watoto kabla hajachelewa. Shabiki huyo alidai kuwa Nelly Oaks anapaswa kuendelea na maisha yake na kujenga familia mapema, akihusisha uhusiano wake wa zamani na Akothee kama sababu ya kupoteza muda. Akothee hakuvumilia kauli hiyo na aliibuka kumkemea shabiki huyo kwa kumhusisha Nelly katika mjadala huo. Amehoji kwa nini jina la Nelly linavutwa katika mazungumzo hayo na kusisitiza kuwa ana heshima kubwa kwake. Aidha, ameeleza kuwa si sahihi kwa watu wa nje kudhani wanajua mipango au maamuzi ya maisha ya Nelly Oaks, akiuliza ni nani aliyesema hana au hatakuwa na mke na watoto.. Akothee na Nelly Oaks waliwahi kuwa katika uhusiano uliovuta hisia za wengi kabla ya kutengana, lakini wameonekana kudumisha heshima ya pande zote hata baada ya kuachana.

Read More
 Akothee Atoa Rate Card Rasmi kwa Matukio na Deals za Kibiashara

Akothee Atoa Rate Card Rasmi kwa Matukio na Deals za Kibiashara

Msanii wa muziki kutoka Kenya, Akothee, ameachia rasmi rate card yake, ikionyesha gharama za kum-book kwa shughuli mbalimbali za burudani na ushirikiano wa kibiashara. Kwa mujibu wa taarifa alizochapisha mtandaoni, Akothee anatoza KSh 700,000 kwa kuhudhuria hafla bila kutumbuiza. Hii ni kwa matukio kama mikutano ya kibiashara, sherehe binafsi au hafla za kitaasisi ambapo uwepo wake pekee unahitajika. Kwa upande wa maonyesho ya moja kwa moja (live performances), bei yake inaanzia KSh 1.2 milioni hadi KSh 1.5 milioni, kutegemeana na aina ya hafla, maandalizi ya jukwaa na mahitaji ya tukio husika. Aidha, Akothee anatoza KSh 2 milioni kwa ground activations, pamoja na KSh 2 milioni kwa mwezi kwa mikataba ya brand ambassadorship na shughuli za masoko (Marketing).

Read More
 Akothee Achoshwa na Maswali ya Uhusiano Wake wa Nelly Oaks

Akothee Achoshwa na Maswali ya Uhusiano Wake wa Nelly Oaks

Msanii wa muziki kutoka Kenya, Akothee, ameonekana kukerwa na maswali ya mara kwa mara kutoka kwa baadhi ya mashabiki wake wanaoendelea kumuulizia aliyekuwa mpenzi wake, Nelly Oaks. Kupitia kauli yake ya moja kwa moja, Akothee amewajibu mashabiki hao kwa ukali akisema, “Mumeskia ametangazwa amekufa?” kauli iliyoonyesha wazi kuchoshwa kwake na mada hiyo ambayo anaonekana hataki kuirudia tena. Akothee ameonekana kusisitiza kuwa kila mtu ana maisha yake na kwamba uhusiano wake wa zamani haupaswi kuendelea kuwa mjadala wa kila siku mitandaoni. Mwanamama huyo, ameeleza kuwa mashabiki wanapaswa kuzingatia mambo ya maana zaidi badala ya kuendelea kuchimba masuala aliyoyaacha nyuma.

Read More
 Akothee Asema Hana Pesa ya Kulea Wanaume Baada ya DM Nyingi za Mapenzi

Akothee Asema Hana Pesa ya Kulea Wanaume Baada ya DM Nyingi za Mapenzi

Msanii asiyeishia na matukio kila leo, Akothee, ameonyesha kuchukizwa kwake na tabia ya baadhi ya wanaume wanaomfuata kupitia jumbe za faragha wakimtaka kimapenzi au hata kumuomba msaada wa kifedha. Kupitia mitandao ya kijamii, Akothee amesema amechoshwa na wanaume anaowataja kuwa wazembe, ambao badala ya kufanya kazi na kujituma, wamegeuza mitandao ya kijamii kuwa sehemu ya kuomba mahusiano na misaada ya kifedha kutoka kwa wanawake waliopiga hatua kimaisha. Akothee amewataka wanawake kupuuza kabisa wanaume wa sampuli hiyo, akisisitiza kuwa mwanamke hapaswi kubeba majukumu ya mwanaume mzima kwa misingi ya mapenzi. Kauli yake inakuja siku chache baada ya kudai kuwa mwaka 2026 ataanza kuwaanika hadharani wanaume wanaomfuata kwa siri wakimuomba pesa, akisema tabia hiyo imevuka mipaka na haikubaliki katika ulimwengu wa sasa.

Read More
 Akothee Ashauri Binti Yake Kuchagua Pesa Badala ya Mapenzi Kwenye Mahusiano

Akothee Ashauri Binti Yake Kuchagua Pesa Badala ya Mapenzi Kwenye Mahusiano

Msanii mwenye utata nchini Kenya, Akothee, amemshauri hadharani binti yake Rue Baby achague mwanaume mwenye uwezo wa kifedha badala ya kufuata mapenzi pekee katika mahusiano. Kwa mujibu wa Akothee, uthabiti wa kifedha hujenga msingi imara wa maisha, huku mapenzi yakija baadaye pale mazingira yanapokuwa salama na yenye utulivu. Mwanamama huyo amesisitiza kuwa atakuwa mwenye furaha zaidi akimuona binti yake Rue Baby akililia Dubai akiwa na tajiri mwenye pesa kuliko alilie kijijini kwao Kanyamkago bila msaada wowote. Kauli hiyo imezua hisia mseto miongoni mwa watumiaji wa mitandao ya kijamii. Wapo waliounga mkono wakisema ushauri huo unatokana na uzoefu wa maisha na changamoto halisi zinazokumba mahusiano mengi, huku wengine wakipinga wakidai mapenzi ya kweli hayawezi kubadilishwa na maslahi ya kifedha.

Read More
 Akothee Awaonya Wanaume Wanaomtaka Kimapenzi

Akothee Awaonya Wanaume Wanaomtaka Kimapenzi

Msanii asiyeishiwa na matukio kila leo, Akothee, amewaonya vikali wanaume wanaojaribu kuonyesha nia ya kuanzisha mahusiano ya kimapenzi naye, akisema wazi kuwa kwa sasa hayuko sokoni wala hana mpango wa kuingia kwenye uhusiano wowote. Kupitia ujumbe wake uliojaa msimamo Instagram, Akothee amesema hataki kutafutwa kimapenzi na wanaume wasiokuwa na mwelekeo wa maisha au maandalizi ya kifedha. Ameeleza kuwa mapenzi ya kweli hayawezi kuwepo bila msingi wa kifedha. Akothee, anayejulikana kwa kujiamini na kusema mambo bila kuficha, amesema anajua anachotaka katika maisha na hawezi kuruhusu kuvurugwa na maneno matamu yasiyoambatana na vitendo. Kwa mujibu wake, wanaume wanaomfuata bila uwezo wa kujisimamia kifedha wanapoteza muda wao. Mwanamama huyo, amesema amejikita zaidi katika kujijenga binafsi na kukuza biashara zake, huku akiwahimiza wanaume kuwekeza kwanza katika maisha yao kabla ya kufikiria mahusiano.

Read More
 Akothee Ataka Jamii Iache Kuingilia na Kukosoa Mtindo Wake wa Mavazi

Akothee Ataka Jamii Iache Kuingilia na Kukosoa Mtindo Wake wa Mavazi

Msanii wa muziki kutoka Kenya, Akothee, amewataka wakosoaji wake kuacha kuingilia mtindo wake wa mavazi na maisha binafsi, akisema lawama nyingi zinazomkabili zinatoka kwa watu wasioishi kulingana na maadili wanayoyahubiri mitandaoni. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Akothee ameweka wazi kuwa hataki kuelekezwa jinsi ya kuvaa na watu anaodai wanaficha maovu yao binafsi nyuma ya pazia la maadili ya kijamii. Ameeleza kuwa kuna watu wanaojifanya walinzi wa maadili ilhali familia zao zinakumbwa na matatizo makubwa kama ulevi, usaliti katika ndoa na kuvunjika kwa familia. Msanii huyo amesisitiza kuwa sanaa ni njia ya kujieleza na kwamba jamii inapaswa kujifunza kuheshimu uhuru wa wasanii badala ya kuwahukumu kwa misingi ya mitazamo binafsi. Aidha, amewataka wanaomkosoa waangalie kwanza mienendo yao kabla ya kumshambulia hadharani. Kauli hiyo ya Akothee imekuja baada ya kukosolewa vikali na baadhi ya wanajamii kufuatia kusambaa kwa vipande vya video ya wimbo wake mpya uitwao Society. Video hiyo inaonyesha mavazi yanayobana na kufichua sehemu nyeti za mwili wake.

Read More
 Akothee Awaonya Mabinti zake Dhidi ya Kuingia Kwenye Mahusiano na Wanasiasa

Akothee Awaonya Mabinti zake Dhidi ya Kuingia Kwenye Mahusiano na Wanasiasa

Mwanamuziki, Akothee, ameibua mjadala mitandaoni baada ya kutoa onyo kali kwa mabinti zake kuhusu kujiingiza kwenye mahusiano ya kimapenzi na wanasiasa. Akizungumza kupitia mitandao yake ya kijamii, Akothee amesema kuwa ameshuhudia visa vingi vya vijana wa kike kuumizwa kihisia na hata kifedha wanapodanganywa na viongozi wanaotumia nafasi zao kwa anasa na starehe. Akothee amesisitiza kuwa wanasiasa wengi huwa na maisha yenye mkanganyiko na ratiba isiyoeleweka, jambo linalofanya mahusiano yao kuwa na changamoto nyingi. Amehitimisha ujumbe wake kwa kusema anataka mabinti wake wakue wakiwa na uthabiti wa kimaamuzi na wasikubali kushawishiwa na hadhi au pesa. Kauli ya Akothee imezua mjadala mtandaoni, baadhi wakikubaliana naye kuwa vijana wengi wanahitaji ushauri wa namna hii, huku wengine wakiona kila mtu anapaswa kupewa nafasi ya kufanya maamuzi yake ya kimahusiano.

Read More
 Akothee Akerwa na Swali la Shabiki Kuhusu Nelly Oaks

Akothee Akerwa na Swali la Shabiki Kuhusu Nelly Oaks

Mwanamuziki na mfanyabiashara Akothee ameonekana kukerwa na shabiki aliyemuuliza kuhusu aliyekuwa mpenzi wake, Nelly Oaks, wakati akiwa nchini Afrika Kusini. Akothee alikataa kabisa kujadili kuhusu uhusiano wake wa zamani, akionyesha kwamba amesonga mbele na hataki kurudi kwenye mada hizo. Ameeleza kuwa yeyote anayevutiwa na habari za Nelly Oaks anapaswa kufuatilia taarifa zake mtandaoni, badala ya kumrudisha kwenye uhusiano uliokwisha. Akiwa katika mazingira mapya na shughuli mbalimbali Afrika Kusini, Akothee ameonyesha kutoridhishwa na mashabiki wanaoendelea kumhusisha na maisha yake ya zamani, akisisitiza kuwa yupo katika hatua tofauti ya maisha na kwamba kuna wanaume wengi kwenye dunia, hivyo hajafungamana na yaliyopita. Kauli yake imewafanya mashabiki kutofautiana mtandaoni, baadhi wakimwelewa Akothee kwa kutaka kuheshimu maisha yake mapya, huku wengine wakionyesha udadisi zaidi kuhusu historia yake ya kimapenzi.

Read More
 Akothee Awakosoa Mastaa Wanaoishi Maisha ya Kuigiza Mtandaoni

Akothee Awakosoa Mastaa Wanaoishi Maisha ya Kuigiza Mtandaoni

Msanii wa muziki kutoka Kenya, Akothee, amewakosoa vikali baadhi ya mastaa nchini humo kwa kile alichokiita kuishi maisha ya uongo kwenye mitandao ya kijamii. Akothee anadai kuwa mastaa wengi wanajionyesha kama watu wenye utajiri mkubwa mtandaoni, lakini ukweli ni kwamba wengi wao hawana uwezo huo katika maisha ya kawaida. Mwanamama huyo, amewataka mashabiki kutopoteza muda kujilinganisha na maisha ya watu wanaowaona mtandaoni, akisema maisha ya mtandaoni mara nyingi hayalingani na uhalisia. Sanjari na hilo, Akothee amewakosoa baadhi ya content creators wanaotafuta umaarufu kwa kutumia matusi na kuwashambulia mastaa, akisema aina hiyo ya maudhui inachochea chuki na inakosa ubunifu. Amewahimiza kutengeneza maudhui yanayozingatia kazi yenye thamani badala ya kutegemea kiki za muda mfupi.

Read More
 Akothee Amkingia Kifua Winnie Odinga Dhidi ya Ubaguzi wa Kisiasa

Akothee Amkingia Kifua Winnie Odinga Dhidi ya Ubaguzi wa Kisiasa

Mwanamuziki na mfanyabiashara maarufu nchini Kenya, Akothee, amejitokeza kutoa msimamo mkali, akimkinga kifua Mbunge wa EALA, Winnie Odinga dhidi ya kile anachokiita ubaguzi wa kisiasa. Akothee amekemea vikali wale wanaomdhalilisha Winnie Odinga, binti ya hayati Raila Odinga, kwa kigezo cha kuwa hajaingia kwenye ndoa. Kupitia ujumbe wake kwenye mitandao ya kijamii, Akothee, amesisitiza kuwa sifa za mtu katika siasa hazipaswi kuhukumiwa na hali yake ya ndoa. Akizungumzia suala la ndoa, amesema kwa shauku kwamba ndoa haifai kuchukuliwa kama mafanikio, akidai kuwa taasisi hiyo ya ndoa ni kwa ajili ya wanawake ambao hawana mwelekeo wa maisha na ambao wanahitaji kuongozwa. Akothee amewaonya vikali wanasiasa na wafuasi wao wanaotumia lugha chafu na unyanyasaji dhidi ya wanawake katika ulingo wa siasa, akisisitiza umuhimu wa kuzingatia akili, bidii, na mafanikio ya wanawake badala ya kuzingatia hali yao ya kibinafsi ya ndoa. Mwanamama huyo amemalizia ujumbe wake kwa kusema kwamba hata kama watu hawakubaliani na mawazo ya kisiasa ya Winnie, wanapaswa kukosoa kwa staha na kuheshimu utu wake kama binadamu.

Read More