
Msanii wa muziki nchini Akothee amedokeza mpango wa kupata mimba kwa njia ya kisanyasi ili kukata kiu yake ya kutamani mtoto.
Akothee ambaye ana umri wa miaka 39 amesema kwa sasa ana mpango wa kumtafuta mpenzi, hivyo ameamua kutumia njia ya kupandikazi mbegu za kiume hospitalini ili mwisho wa siku apate mimba.
Akothee yupo kwenye ziara ya kimuziki nchini ufaransa na watoto wake watano amesema watu wasishangaa au kumuuliza baba wa mtoto wake pindi watakapomuona akiwa mjamzito hivi karibuni.
“I have something for kids. I miss something and I don’t want to get pregnant at 45. Since looks like a partner won’t be possible soon. I will be going for Artificial Insemination here in France. So when you see me pregnant don’t ask me who the father is. All I want is my own baby with No drama,. Cheers and good night,” Akothee ameandika kwenye ukurasa wake wa Instagram.
Hata hivyo amewashauri watu kwenye jamii kujihusisha au kufanya mambo yanayowafurahisha duniani kwa kuwa maisha ni yao.
“Do what you want to do in this life, Its your life,” Amesema.