
Msanii Catherine Kusasira bado anajutia hatua ya kutokamilisha masomo yake baada ya kudai kuwa amekosa kazi serikalini kutokana na ukosefu wa elimu ya kutosha.
Katika mahojiano yake hivi karibuni Kusasira amesema angekuwa waziri katika serikali ya rais Yoweri Museveni kama angekuwa amemaliza masomo yake
Hitmaker huyo wa “I love you” amesema anaumizwa na kitendo cha serikali kutompa kazi kutokana na yeye kukosa elimu licha ya kuwa na ukaribu na maafisa wakuu serikalini
“It hurts me that I didn’t finish school early enough. I would be a minister or even the prime minister but I am limited by my academic qualifications. That’s why I went back to school,” Alisema.
Catherine kusasira ambaye ni mshauri wa masuala ya ndani ya jiji la kampala kwa sasa amejiunga na chuo kikuu cha Nkumba kuendeleza masomo yake.