
Msanii wa Bongofleva Harmonize ameweka wazi rasmi kwa sasa anaanza kutoza kiasi cha KSh. Milioni 5.2 kwa ajili ya kufanya naye Kolabo, lakini sharti la kwanza wimbo uwe mkali.
Kupitia insta story yake kwenye mtandao wa Instagram amekazia kwamba kuna mtu fulani atamtoza kiasi cha KSh. Milioni 26 atakapo hitaji kolabo naye.
Lakini pia Harmonize amebainisha kwamba kama mwanamuziki hajatengeza hits zaidi ya 10 kwa mwaka 2022 asimuongeleshe, na hii ndio mood yake ya mwezi Disemba.