
Mkongwe wa muziki wa Bongofleva, Lady Jaydee ametangaza ujio wa album ya pamoja na msanii mwenzake Rama Dee.
Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Jide ambaye ni mwimbaji wa kike wa Bongofleva anayeongoza kutoa album nyingi zaidi akiwa nazo nane, amesema album hiyo itaingia sokoni mwezi huu kabla ya tamasha lake la muziki.
Lady Jaydee kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake mpya uitwao “Suluhu” aliomshirikisha Rama Dee, ikiwa ni wimbo wao wa pili kuachia baada ya”Kama Hauwezi” iliyotoka mwaka 2017.