Entertainment

MAANDY AWAJIBU WANAODAI ANATOKA KIMAPENZI NA MAPRODYUZA

MAANDY AWAJIBU WANAODAI ANATOKA KIMAPENZI NA MAPRODYUZA

Msanii wa kike nchini Maandy amewajibu wanaodai kuwa mafanikio yake kimuziki yametokana na yeye kutoka kimapenzi na maprodyuza wa muziki.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram hitmaker huyo wa ngoma ya “By The Way” ameonakana kukasirishwa na wanaomema vibaya kwa kusema kwamba tuhuma hizo hazina ukweli wowote bali zimeibuliwa na watesi wake ambao wanalenga kumuharibia jina.

Mrembo huyo ameenda mbali zaidi na kusema kwamba kama kweliย  angekuwa anajiuza kimwili kwa maprodyuza angeshapeleka muziki wake kimataifa kitambo.

“Huko clock app Wanasema Nagawa mbaya . If I was to use my body to get ahead , ningekua Grammies nikipigania space na Beyoncรฉ ,si hapa ungwaro ๐Ÿ˜ฎโ€๐Ÿ’จ๐Ÿ˜ฎโ€๐Ÿ’จ To the producers Iโ€™ve worked with kindly mark register hapa tuone mko wangapi ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚”, Aliandika Instagram.

Hii si mara ya kwanza kwa Maandy kuzushiwa taarifa za aina hii kwani kipindi cha nyuma alidaiwa kutoka kimapenzi na rapa Breeder LW, madai ambayo aliyakanusha vikali.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *