Entertainment

Meek Mill atangaza kutua barani Afrika kwa mara ya pili

Meek Mill atangaza kutua barani Afrika kwa mara ya pili

Rapa kutoka nchini Marekani Meek Mill ametangaza kurudi tena barani Afrika kwa mara ya pili baada ya kutua kwa mara ya kwanza nchini Ghana kwenye tamasha la Afro Nation lililofanyika mwishoni mwa mwaka 2022

Meek ametoa taarifa kupitia ukurasa wake wa twitter kuwa anatarajia kutua nchini Nigeria muda wowote kuanzia sasa.

“Nakuja Nigeria”, Aliandika.

Lakini pia Rapa huyo amefunguka kuwa anahitaji msambazaji wa kazi zake Barani Afrika na Uingereza. Si hivyo tu Meek amesisitiza kuwa Afrika ni Bara kubwa zaidi duniani, inabidi watu tujiunge kwa pamoja

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *