
Msanii wa kike nchini Miss P amefunguka na kudai kuwa hatawahi fanya collabo tena na msaani mwenzake Willy Paul hadi mwisho wa dunia.
Miss P ametujuza hayo kupitia ukurasa wake wa instagram alipomjibu shabiki yake aliyemuomba wafanya kollabo tena na Willy Paul kwa kusema “Naheshimu sana mawazo yako shabiki yangu ila hutokaa uje tena kusikia Β kollabo hiyo.”
Miss P na Willy P walishawahi kufanya kolabo kupitia nyimbo kama Liar, Fall in Love na Mashallah zilizotoka mwaka wa 2021 lakini walikuja wakaingia kwenye ugomvi mwishoni mwa mwaka jana baada Miss P kujitokeza na kudai kwamba aliondoka kwenye lebo ya muziki ya saldido International kwa sababu alinyanyaswa kimapenzi na willy paul ambaye ndiye mmiliki wa lebo hiyo.