
Hakika huu ni mwaka wenye neema kwa msanii wa nyimbo za nchini Moji Short Baba kwa sababu licha ya ngoma zake kufanya vizuri kupitia digital platforms mbalimbali, kubwa zaidi ni ametajwa kuwa miongoni mwa wasanii watakaowania kwenye tuzo za muziki nchini Uganda.
Moji Short Babaa ametajwa kuwania kipengele cha African Act of the Year kwenye tuzo za muziki wa injili za Vine music Awards ambapo atachuana wasanii kama Judikay, Limo Blaze, Maruzi na Pompi.
Wasanii wengi waliotajwa kwwnye tuzo ni pamoja na Levixxone,D Reign, Coopy Bly, Sandra Suubi ambao wote wanangangania kipengele cha msanii bora wa mwaka.
Tuzo hizo za nchini Uganda zinatarajiwa kutolewa Mei 7 2022 katika hoteli ya Serena jiji Kampala na tayari zoezi la upigaji kura limeanza kupitia wavuti www.vineentgroup.com/vote huku likitarajiwa kukamilika Aprili 8 mwaka huu.