
Rapa Prezzo amefunguka sababu za kuvalia vazi la kuzuia risasa kwenye mwili anapotoka nyumbani kwake.
Katika mahojiano yake hivi karibuni Prezzo amesema alichukua maamuzi ya kuhimarisha usalama baada ya kuvamiwa na majambazi miaka kadhaa iliyopita ambapo wamlipiga risasi kadhaa huku wakitoweka na mali ya thamani ya shillingi millioni 3.5 za Kenya.
“When it comes to security; there is no second guessing because I have been shot before at close range. That’s why I know I am here for a reason. So anybody watching this make sure when you come, aim for the head,” Prezzo alieleza
Utakumbuka mwaka wa 2020 Prezzo aliweka wazi tukio lilomuacha na makovu ya risasi kichwani kwa kusema kwamba majambazi walimvamia siku chache kabla harusi yake na aliyekuwa mke wake Daisy Kiplagat.