Entertainment

PUSHA T AFUNGUKA SABABU ZA KUMALIZA UGOMVI WAKE NA DRAKE

PUSHA T AFUNGUKA SABABU ZA KUMALIZA UGOMVI WAKE NA DRAKE

Rapa kutoka Marekani Pusha T hatimaye amefunguka sababu iliyomfanya kumaliza bifu yake na Drake ambayo ilidumu kwa miaka 10.

Kwenye mahojiano na Desus & Mero, Pusha T ameeleza kwamba, kuwa Baba mwaka 2020 ndio sababu pekee iliyomfanya aimalize bifu yake na Drizzy kwani kulimbadilisha mtazamo wake kwa ujumla hasa kuwahusisha watoto kwenye ugomvi.

Kama utakumbuka vyema, Pusha T ndiye aliifahamisha dunia kwamba Drake ana mtoto anaitwa Adonis lakini alimficha.

Kupitia freestyle yake β€˜The Story of Adidon’ Pusha alichana β€œYou are hiding a child, let that boy come home/ Deadbeat mothaf*cka, playin’ border patrol/ Adonis is your son.”

Hii ilimfanya Drake na baadaye kuthibitisha taarifa hizo kupitia album yake, Scorpion mwaka 2018.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *