Entertainment

RAPPER MKONGWE KUTOKA KENYA NYASHINSKI ADOKEZA MPANGO WA KUJENGA MJI WAKE

RAPPER  MKONGWE KUTOKA KENYA NYASHINSKI ADOKEZA MPANGO WA KUJENGA MJI WAKE

Msanii nyota nchini Nyashinski ameahidi kujenga mji wake mpya  nchini Kenya, mji ambao utatumika na mashabiki zake

Nyashinski ameyaweka wazi hayo Februari 13 mwaka huu kwenye moja ya performance yake iliyofanyika huko Two River Mall jijini Nairobi.

Hitmaker huyo wa ngoma ya “Properly” alienda mbali na kuwashauri wasanii wa muziki nchini watoa nyimbo zenye maudhui safi zitakazodumu kwa muda mrefu.

Hata hivyo amewaacha mashabiki zake na maswali mengi mara baada ya kufuta post zake zote kwenye mtandao wa instagram jambo ambalo walimwengu kwenye mitandao ya kijamii wamehoji kuwa huenda rapa huyo ana matatizo ya kiakili huku wengine wakisema huenda ana mpango wa kuachia project yake mpya

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *