ANGELINA ATANGAZA KUACHA MUZIKI

ANGELINA ATANGAZA KUACHA MUZIKI

Nyota wa muziki nchini uganda Angelina amedokeza mpango wa kuachana kabisa na masuala ya muziki. Angelina ameweka wazi hayo kupitia ukurasa wake wa twitter ambapo amesema ataacha muziki mwaka wa 2022 baada ya kuachia project yake ya mwisho ambayo amekuwa akiifanyia kazi kwa muda. Kulingana na mrembo huyo baada ya kuacha muziki ataelekeza nguvu zake kwingine katika suala zima la kujitafutia riziki. Hata hivyo tweet yake hiyo haikukaa kwa muda kwenye ukurasa wake twitter kwani alikuja akaifuta baada ya kuchapisha. Angelina amekuwa kwenye kiwanda cha muziki nchini Uganda kwa muda wa miaka kumi na ametoa hits kali kama Go Down, Ghetto Lovin, Ronaldo na nyingine kibao.

Read More
 ARSENE WENGER ASEMA KUNA UWEZEKANO WA OFFSIDE KUAMULIWA NA TEKNOLOJIA MWAKA 2022

ARSENE WENGER ASEMA KUNA UWEZEKANO WA OFFSIDE KUAMULIWA NA TEKNOLOJIA MWAKA 2022

Kocha wa zamani wa Arsenal, Arsene Wenger amesema kuna uwezekano mkubwa kwamba maamuzi ya ‘Offside’ yakaamuliwa moja kwa moja kwa kutumia Teknolojia kwenye fainali za Kombe la Dunia 2022 zitakazofanyika nchini Qatar. Wenger ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi wa maendeleo ya mpira wa miguu katika Shirikisho la Soka duniani FIFA, amesema hiyo itakuwa hatua kubwa kwenye soka la dunia kwani pia itapunguza lawana nyingi kwa waamuzi. Kwa sasa teknolojia imechukua nafasi kubwa kwenye mpira kwani maaumizi mengi nyeti yanafanywa na VAR na Goal Line Technology.

Read More