Bebe Cool Aomba Msaada wa Rais Kutangaza Albamu yake Mpya Kimataifa

Bebe Cool Aomba Msaada wa Rais Kutangaza Albamu yake Mpya Kimataifa

Msanii maarufu wa Uganda na mwanzilishi wa Gagamel Crew, Bebe Cool, ametangaza kuwa albamu yake mpya “Break the Chains” itazinduliwa rasmi tarehe 30 mwezi huu. Albamu hiyo, ambayo ni ya saba katika kazi yake ya muziki, imechukua karibu mwaka mmoja kuikamilisha na imerekodiwa katika studio za kimataifa nchini Nigeria, Afrika Kusini, na Uingereza. Katika mahojiano na televisheni ya ndani, Bebe Cool alifichua kuwa hadi sasa ametumia zaidi ya shilingi bilioni 2.56 za Uganda katika utayarishaji wa albamu hiyo, ikijumuisha gharama za uandishi wa nyimbo, uzalishaji, mastering, na posho kwa timu yake ya uzalishaji ndani na nje ya nchi. Hata hivyo, alieleza kuwa changamoto kubwa sasa ni kuisambaza na kuitangaza kimataifa, jambo ambalo litahitaji zaidi ya shilingi bilioni 7 (takriban dola milioni 2). “Mpaka sasa nimetumia dola 700,000. Kufanya muziki wa kiwango cha juu kunahitaji uwekezaji mkubwa. Ili niweze kuitangaza albamu hii kimataifa, nitahitaji zaidi ya dola milioni 2. Nampasa Rais Museveni kuniunga mkono katika hili,” alieleza Bebe Cool. Kwa msingi huo, Bebe Cool ameeleza kuwa anatafuta msaada wa kifedha kutoka kwa Rais Yoweri Kaguta Museveni, ili kufanikisha azma ya kuitangaza albamu hiyo katika soko la kimataifa. Anaamini “Break the Chains” itaweka muziki wa Uganda kwenye ramani ya dunia, na kuwa kichocheo kwa wasanii wengine kuwekeza katika kazi zao kwa maendeleo ya sekta nzima ya burudani nchini.

Read More
 Mfululizo wa Picha za Drake Mtandaoni Wazua Tetesi za Albamu Mpya Iitwayo Ice Man

Mfululizo wa Picha za Drake Mtandaoni Wazua Tetesi za Albamu Mpya Iitwayo Ice Man

Rapa nyota wa Canada, Drake, amezua gumzo mitandaoni baada ya kuchapisha mfululizo wa picha kwenye ukurasa wake wa Instagram, ambazo mashabiki na wachambuzi wa muziki wanazitafsiri kama uthibitisho wa albamu yake mpya kwa jina la ICEMAN. Katika chapisho lake kwenye akaunti rasmi ya Instagram (@champagnepapi), Drake alionekana kuweka picha ya mandhari ya theluji yenye mlima uliofunikwa na barafu, na chini yake akaandika kwa herufi kubwa; ICEMAN. Chapisho hilo limepokea zaidi ya likes milioni moja na maelfu ya maoni kutoka kwa mashabiki waliotafsiri ujumbe huo kama tangazo la jina la albamu mpya. Drizzy pia alichapisha picha za watu mbalimbali mashuhuri wanaohusiana na jina hilo, ikiwa ni pamoja na Bobby Drake, mhusika wa Marvel Comics, Kimi Räikkönen, dereva wa zamani wa Formula 1 na Val Kilmer, ambaye aliigiza kama Iceman katika filamu ya Top Gun. Hata hivyo, Drake hajatoa tamko rasmi kuthibitisha jina la albamu hiyo, lakini machapisho hayo yameongeza matarajio makubwa miongoni mwa mashabiki wake duniani kote. Albamu hii itakuwa kazi yake ya kwanza ya solo tangu kutolewa kwa For All The Dogs mwaka 2023. Kwa sasa, wapenzi wa muziki wanasubiri kwa hamu taarifa rasmi kutoka kwa rapa huyo anayejulikana kwa ubunifu wa hali ya juu na mbinu za kipekee za kusisimua kwenye mitandao ya kijamii

Read More
 JUMA NATURE ATHIBITISHA KUKAMILIKA KWA ALBUM YAKE MPYA

JUMA NATURE ATHIBITISHA KUKAMILIKA KWA ALBUM YAKE MPYA

Msanii mkongwe wa Bongofleva, Juma Nature amesema anajiandaa kuachia albamu yake mpya ambayo imekamilika. Nature amesema anachokifanya kwa sasa ni kutayarisha video kadhaa za nyimbo zinazopatikana kwenye albamu hiyo kabla ya kuingia sokoni hivi karibuni. Hata hivyo Sir Nature hajatuambia jina la album, idadi nyimbo na wasanii aliyowashirikisha kwenye album yake hiyo ila ni jambo la kusubiriwa. Utakumbuka Juma Nature ana historia ya kuwa msanii wa kwanza Bongo kuujaza ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam katika uzinduzi wa albamu yake iitwayo Ugali. Wasanii wengine tanzania ambao tayari wametangaza kukamilika kwa albamu zao ni pamoja na Diamond Platnumz, Harmonize, Marioo, Young Lunya, Lava Lava, Tommy Flavour, Maua Sama, Ommy Dimpoz na wengine wengi.

Read More
 KENRAZY AACHIA RASMI SON OF GOD ALBUM

KENRAZY AACHIA RASMI SON OF GOD ALBUM

Mkali wa muziki nchini Kenrazy ameachia rasmi album yake mpya inayokwenda kwa jina la Son of God. Son of God album imebeba jumla ya mikwaju 20 ya moto huku ikiwa na kolabo 7 pekee. Kenrazy amewashirikisha wasanii mbali mbali wa humu nchini kama Bigpin, Kaya,Visita, Sosuun, Civa Ramah K na Young haze. Album ya “Son of God” ni album ya tatu kwa mtu mzima kenrazy baada ya Ti-chi ya mwaka wa 2008 na Get it Right from Kenrazy ya mwaka wa 2011. Hata hivyo Album hiyo inapatikana ‘Exclusive’ kupitia mitandao yote ya  kukisikiliza na kuuza muziki duniani kama vile youtube, na Spotify

Read More
 ONLY ONE KING ALBUM YA ALI KIBA NDANI YA TIMES SQUARE,NEW YORK.

ONLY ONE KING ALBUM YA ALI KIBA NDANI YA TIMES SQUARE,NEW YORK.

Album mpya ya msanii Ali kiba “Only One King” inazidi kuweka historia mara baada ya cover la album hiyo kuonekana katika Screen za eneo maarufu Times Square huko Jijini New York, nchini Marekani. Album hiyo ambayo ina siku tatu tangu iachiwe, ina kuwa kazi ya kwanza Kwa Ali kiba kuonekana Times Square sehemu ambayo matangazo makubwa duniani huonekana. Sanjari na hilo “Only One King” album imefanikiwa kufikisha jumla ya Streams Milioni 1 katika mtandao wa BoomPlay tangu iachiwe rasmi Oktoba 7. Album hiyo ambaye ni ya tatu kwa mtu mzima Ali Kiba ina nyimbo 16 alizoshirikisha wasanii kutoka Tanzania, Kenya na Nigeria. Miongoni mwa nyimbo zilizoko ni Utu, Let me, Niteke, Bwana mdogo, Happy, na nyingine nyingi.

Read More
 SAUTI SOL MBIONI KUJA NA ALBUM MPYA

SAUTI SOL MBIONI KUJA NA ALBUM MPYA

Kundi la muziki nchini sauti sol wametangaza mwezi ambao wataichia album yao ya sita tangu waanze safari yao ya muziki. Kupitia barua ya wazi waliyoishare kwenye ukurasa wao wa instagram sauti sol wamesema album yao mpya itaingia sokoni mwezi mei mwaka wa 2022. Wakali hao wa ngoma ya Suzzana wamesema kabla ya kuachia album yao mpya, wataachia singo yao mpya mwezi Disemba mwaka huu ambapo wamesema kwamba wataweka wazi tarehe ambayo wataachia project hiyo. Sanjari na hilo wametusanua kwamba wanakuja na documentary yao iitwayo Alone Together ambayo itazungumzia changomoto ambazo wasanii wa kundi la sauti sol wamepitia tangu ujio wa janga la korona. Kauli ya sauti sol inakuja mara baada ya kufanikisha tamasha lao la kimuziki liitwalo UK residency lilofanyika nchini uingereza mapema mwezi huu.

Read More