Bebe Cool Asema Mwanawe Allan Hendrick Anakumbwa na Changamoto za Afya ya Akili

Bebe Cool Asema Mwanawe Allan Hendrick Anakumbwa na Changamoto za Afya ya Akili

Msanii maarufu wa muziki wa Uganda, Bebe Cool, amefunguka na kuthibitisha kuwa mwanawe Allan Hendrick anapambana na changamoto za afya ya akili. Ingawa hakutoa maelezo ya kina kuhusu hali hiyo, amesisitiza kuwa ni jukumu la mwanawe mwenyewe kushinda na kuweza kushughulikia matatizo hayo binafsi. Katika mahojiano na vyombo vya habari, Bebe Cool alieleza kuwa changamoto hizo ni za kibinafsi na zilimfikia Allan kwa kiwango ambacho hata familia na marafiki walishindwa kumpa msaada wa kutosha. “Ni kweli Allan alikuwa anakumbwa na changamoto binafsi ambazo mimi au mtu mwingine hatukuweza kumsaidia kutoka kwao.” Alisema Bebe Cool. Taarifa hii imeibua hisia mchanganyiko kutoka kwa mashabiki na wafuasi wake, wengi wakimwombea nguvu na kuonyesha mshikamano kwa Allan. Afya ya akili ni changamoto inayogusa watu wengi duniani, na kuzungumzia hadhi hii wazi ni hatua muhimu katika kupambana na unyanyapaa unaozunguka. Watu maarufu kama Bebe Cool wanachukuliwa kuwa nguzo muhimu katika kuleta mabadiliko chanya kwa kuzungumza hadharani kuhusu masuala haya nyeti.

Read More
 ALLAN HENDRICK AAPA KUANIKA MAOVU YA KING SAHA

ALLAN HENDRICK AAPA KUANIKA MAOVU YA KING SAHA

Msanii Allan Hendrik ameahidi kuanika siri nzito kuhusu baba mzazi wa King Saha iwapo hatoacha kumshambulia baba yake Bebe Cool. Katika mahojiano yake hivi karibuni Hendrick amesema amefanya utafiti na amegundua baadhi ya maovu ambayo baba mzazi wa king saha anajihusisha nayo. Msanii huyo amesema atamuaibisha King Saha akikataa kumtukana bebe cool licha ya baba yake huyo kumpuza kwa muda kwa muda. “I have done my research and discovered some dirty things about his father. I’ll go personal if he refuses to chill my dad. He keeps attacking him despite of ignoring him,” amesema Hendrik. Allan Hendrik tayari ameshaachia nyimbo mbili mbili zinazomtolea uvivu King Saha ambaye amekuwa akimshambulia Bebe Cool kwenye mahojiano mbali mbali. Utakumbuka juzi kati Bebe Cool alimpa ruhusa mwanae huyo apambane na wanaomkosoa kwenye mitandao ya kijamii.

Read More
 BEBE COOL AVUNJA KIMYA CHAKE KUHUSU BIFU YA KING SAHA NA ALLAN HENDRICK.

BEBE COOL AVUNJA KIMYA CHAKE KUHUSU BIFU YA KING SAHA NA ALLAN HENDRICK.

Bebe Cool amekuwa kwenye kiwanda cha muziki Afrika Mashariki kwa kipindi cha miaka 20 bila kupoa. Ni moja kati ya wasanii wakongwe ambao wakiongea chochote kila mtu kwenye tasnia muziki nchini Uganda anamsikiliza licha ya maisha yake kuandamwa na kashfa nyingi. Msaniii huyo ametoa wito kwa kijana yake Allan Hendrik na King Saha wajitenge na vita vya maneno na badala yake wafanya muziki mzuri Hitmaker huyo wa Gyenvudde amesema wawili hao wanapaswa kuelekeza nguvu zao zote kwenye muziki kwani kutupia maneno makali mtandaoni kutawapoteza kimuziki huku akitoa angalizo kwa King Saha aache kutumia dawa za kulevya. “They have time to be productive because they are still young. They should focus on releasing music, they shouldn’t go after one another. I just want to  King Saha stay away from drugs,” Amesema kwenye mahojiano yake hivi karibuni. Mapema wiki hii , Allan Hendrick alithibitisha kuwa hana ugomvi wowote na King Saha licha ya wimbo wake uitwao  ‘matayo’ kuonekana kumlenga moja kwa moja msanii huyo.

Read More
 KING SAHA AMJIBU KISOMI ALLAN HENDRICK

KING SAHA AMJIBU KISOMI ALLAN HENDRICK

Mwanamuziki kutoka Uganda King Saha amethibitisha kuwa hawezi mujibu kijana wa Bebe Cool Allan Hendrick ambaye alimshambulia kupitia wimbo uitwao Matayo ambao aliuachia jumatatu wiki iliyopita. Katika mahojiano yake hivi karibuni King Saha ameeleza adui yake ni Bebe Cool na sio mwanae Allan Hendrick. Msanii huyo amesema Allan Hendrick anatumia jina lake kutafuta umaarufu. “Sitamjibu Hendrick kwa kuwa sijui nia yake. Labda anataka wamzungumzie kwenye vyombo vya habari ila nina shida na Zakayo ambaye Baba yake mzazi”,Alijibu alipoulizwa atoe maoni kuhusu wimbo wa Matayo wake Allan Hendrick. Hata hivyo Hendrick amesisitiza kuwa wimbo wa Matayo ni mahususi kwa ajili ya King Saha na kila kijana ambaye ameathirika na matumizi ya dawa za kulevya

Read More
 ALLAN HENDRICK AKANUSHA KUWA KWENYE BIFU NA KALIFAH AGANAGA

ALLAN HENDRICK AKANUSHA KUWA KWENYE BIFU NA KALIFAH AGANAGA

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Allan Hendrick maarufu kama Paper Daddy amepuzilia mbali madai ya kuwa kwenye bifu na msanii mwenzake Kalifah Aganaga. Katika mahojiano yake hivi karibuni Allan Hendrick amesema yeye na Kalifah Aganaga ni marafiki wakubwa, hivyo hawana ugomvi wowote kama jinsi ambavyo vyombo vya habari nchini Uganda vimewaaminisha mashabiki wao. Awali Kalifah Aganaga alimsuta vikali Bebe Cool kwa hatua kumtelekeza kimuziki mwanae Allan Hendrick ambapo alienda mbali zaidi kujitolea kumuandikia nyimbo zitakazo mfanya msanii huyo awe Staa. Hata hivyo kwenye moja ya mahojiano juzi kati Kalifah Aganaga alinukuliwa akisema kwamba anajutia kumkosoa Bebe Cool na anatamani kumuomba msamaha kwa kumvunjia heshima. Utakumbuka Allan Hendrick na Kalifah Aganaga tayari wamefanya wimbo wa pamoja ambao wana mpango wa kuachia hivi karibuni.

Read More
 JOSE CHAMELEONE AMWAGIA SIFA MSANII CHIPUKIZI ALLAN HENDRICK, AAHIDI KUSIMAMIA MUZIKI WAKE

JOSE CHAMELEONE AMWAGIA SIFA MSANII CHIPUKIZI ALLAN HENDRICK, AAHIDI KUSIMAMIA MUZIKI WAKE

Mkongwe wa muziki nchini uganda Jose Chameleone amehapa kukuza muziki wa msanii Allan Hendrick kwani ni kijana ambaye ana ari ya kutaka kufanya makubwa kwenye muziki wake. Katika mahojiano yake hivi karibuni Bosi huyo wa leone island amemwagia sifa msanii huyo chipukizi kwa kumtabiria mema kuwa atakuja kuwa msanii mkubwa kwenye kiwanda cha muziki nchini uganda kutokana na kipaji chake cha kipekee katika muziki wake. Kauli ya Chameleone imekuja mara baada ya kuonekana katika siku za hivi karibuni akitumia muda wake mwingi kukaa na Allan Hendrick ambaye ni kijana wa msanii mwenzake Bebe Cool. Utakumbuka msanii Bebe cool amekuwa akikosolewa na watu kwa kutompa support kijana wake Allan Hendrick  kutokana na hatua yake ya kumuacha akipambana mwenyewe kwenye muziki wake licha ya bebe cool kumiliki lebo ya muziki ya Gagamel ambayo ina uwezo wa kukuza kipaji cha msanii huyo.

Read More