Mke wa Ali Kiba awaacha mashabiki njia panda kuhusu ndoa yake
Mke wa Ali Kiba ameacha maswali mengi kwenye vichwa vya mashabiki wa hitmaker huyo wa “Utu” baada ya kuandika ujumbe wenye ukakasi kwenye akaunti yake ya Instagram. Kupitia insta story yake Amina ameandika “Rasmi nipo huru” ujumbe ambao wengi wametafsiri kama ndoa yake na Ali Kiba imefikia mwisho. Kama utakumbuka vizuri, mwezi Februari mwaka huu mitandao mikubwa ya habari nchini iliripoti kuwa Amina ameomba talaka na ametaka alipwe kiasi cha shillingi laki 2 kwa mwezi kwa ajili ya matunzo ya watoto.
Read More