ANGELINA AKANUSHA TAARIFA ZA KUWA MJA MZITO
Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Angelina amekanusha madai yanayotembea kwenye mitandao ya kijamii kuwa ni mja mzito. Katika mahojiano yake hivi karibuni Angelina amesema ameshangazwa na hatua ya watu kumtumia jumbe za kumtakia kheri ya kupata uja uzito licha ya kutokuwa na uja uzito wowote. Angelina amesema taarifa za yeye kuwa mja mzito zimechangiwa na namna ambavyo amebadilika kimwili na picha ambazo pia amekuwa akizichapisha kwenye mitandao yake ya kijamii, jambo ambalo amedai liliwaaminisha walimwengu kuwa huenda mrembo huyo ana-edit sana picha zake kuficha uja uzito. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Go Down” amesema hana mpango wa kupata uja uzito kwa sasa ila ameamua kuelekeza nguvu zake zote kwenye muziki wake hivyo mashabiki watarajie kazi nzuri kutoka kwake.
Read More