ANGELLA KATATUMBA AKIRI KUTESWA NA MAPENZI

ANGELLA KATATUMBA AKIRI KUTESWA NA MAPENZI

Mwanamuziki kutoka uganda Angella Katatumba amewashangaza mashabiki wake alipofichua kwamba kuna kipindi maishani mwake alikula tu vipande vya barafu kwa takriban wiki tatu. Katika mahojiano yake hivi karibuni msanii huyo wa Black Market Records (BMR) amefunguka kuhusu matatizo yake ya maisha akisema kwamba alikula vipande vya barafu kwa wiki tatu alipoachwa na mume wake wa zamani nchini Marekani. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Wendy” amesema kwamba alipoachwa, alikuwa amefulia kiuchumi na hakuwa kitu cha kufanya ila kula tu vipande vya barafu. Angella katatumba ameenda mbali zaidi na kusema kwamba aliogopa hata kuwapigia simu wazazi wake nyumbani kwa ajili ya kuomba msaada wa kifedha kwa kuwa aliona aibu juu kuachwa na mume wake. Hata hivyo amesema anamshukuru Mungu kwa kumfanya ashinde hali ngumu aliyokuwa akipitia kipindi hicho ingawa alipoteza takriban kilo 38 kwa wiki tatu alizokuwa anakula vipande vya barafu.

Read More
 BLACK MARKET RECORDS YAMTAKA PRODYUZA DADDY ANDRE KUFUFUA MUZIKI WA ANGELLA KATATUMBA

BLACK MARKET RECORDS YAMTAKA PRODYUZA DADDY ANDRE KUFUFUA MUZIKI WA ANGELLA KATATUMBA

Angella Katatumba ni moja kati wasanii ambao wamedumu kwenye tasnia muziki nchini uganda kwa muda mrefu. Licha ya kuanza muziki miaka 15 iliyopita, mrembo huyo mwenye umri wa miaka 46 amekuwa akipambana kuupeleka muziki wake kimataifa. Wakati alikutana na prodyuza Daddy Andre mwaka wa 2018 walirekodi wimbo wa pamoja uitwao “Tonelabira” ambao ulikuja ukawa mkubwa sana nchini Uganda mwaka wa 2019. Hata hivyo walikuja wakakosana vibaya baada ya wawili hao kuchanganya raha ya mapenzi na muziki, jambo lilompelekea Angella katatumba kusuasua kimuziki. Sasa taarifa mpya mjini ni kwamba lebo ya muziki ya Black Market Records imetoa rai kwa prodyuza Daddy Andre kumshika tena mkono Angella Katatumba  kama njia kufufua muziki wake. Kulingana na chanzo cha karibu na lebo ya Black Market, Daddy Andrea ana mpango wa kumtayarishia Angella Katatumba nyimbo nne kali mwaka  huu wa 2022 ambazo zitakuwa moto wa kuotea mbali. Utakumbuka wawili hao kwa sasa wana wimbo wa pamoja uitwao “Wendi” ambao unafanya vizuri kwenye chati mbali mbali nchini uganda.

Read More
 DADDY ANDREA NA ANGELLA KATATUMBA WAFUFUA TENA PENZI LAO

DADDY ANDREA NA ANGELLA KATATUMBA WAFUFUA TENA PENZI LAO

Wasanii Angella Katatumba na Daddy Andrea walivunja uhusiano wao mwaka wa 2020 baada andrea kudinda kufanya vipimo vya HIV.   Kwenye mahojiano mbali mbali Daddy Andrea alithibitisha kwamba hajawahi mpenda Angella Katatumba na jambo hilo lilimsumbua sana mrembo huyo.   Andrea alienda mbali zaidi na kuanza mahusiano mapya na Nina Roz ila mahusiano yao yalikuja yakiingiwa na ukungu kwa madai ya usaliti na kumvunjiana heshima.   Sasa mapya yameibuka  baada ya Angella Katatumba kuthibitisha kwamba wamerudiana na Daddy Andrea kwenye moja ya interview.   Hitmaker huyo wa amesema amerudiana na mpenzi wake wa zamani Daddy Andrea baada ya prodyuza huyo kumuomba msamaha.   Wawili hao wamedai kwamba tayari wamerekodi wimbo wa pamoja uitwao Wendi ambao utatoka hivi karibuni.   Ikumbukwe daddy andrea na Angella Katatumba wapo chini ya lebo ya muziki ya black market records ambayo inasimamia kazi zao za muziki.    

Read More