Anjella awataka mashabiki wawe na subira

Anjella awataka mashabiki wawe na subira

Mwimbaji Anjella  baada ya kuaga Konde Music Worldwide amewataka mashabiki wake wawe na subira. Nyota huyo wa kizazi kipya amebainisha hilo akizungumza kwenye mahojiano na CloudsE ya Clouds Fm mchana huu. “Kila kitu nitakuja kukiweka wazi, mashabiki wangu wawe na subira,” -ameeleza Anjella akiiambia Clouds E. Anjella ameamua kueleza hilo kufuatia mashabiki wake kutamani kujua hatma yake ama nini kifuatacho kutoka kwake baada ya kuachana na Konde Gang. Itakumbukwa, Anjella alitambulishwa kwenye lebo ya Konde Music Worldwide Machi 11, 2021, hadi anaaga leo hii, Januari 02, 2023 anakuwa amedumu kwenye lebo hiyo kwa muda wa mwaka mmoja na miezi tisa

Read More
 Anjella aaga rasmi Konde Gang

Anjella aaga rasmi Konde Gang

Hatimaye mwanamuziki Anjella ameaga rasmi kwa waliokuwa waajiri wake lebo ya muziki Konde Music Worldwide Nyota huyo amewashukuru Konde Gang kwa kukiona kipaji chake na kumpa nafasi iliyochangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wake kisanaa, Anjella ameutumia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram kutuma salamu hizo, ikiwa ni ishara ya kukamilika kwa taratibu zote za kisheria kuondoka ndani ya lebo hiyo inayoongozwa na msanii Harmonize Sasa ni rasmi Anjella yupo huru kufanya kazi nje ya lebo hiyo Harmonize ndiye aliyeanza kutangaza kuachana na mwimbaji huyo kwenye lebo yake, ambapo aliweka wazi hilo Novemba 5, 2022 akithibitisha tetesi zilizokuwa zikienea kuachana nae. Ikumbukwe, Anjella anakuwa mwanamuziki wa NNE kuachana na Konde Gang ndani ya kipindi kifupi baada ya Country Boy, Cheed na Killy kuachana na lebo hiyo.

Read More
 Baba Levo ahaidi kumsaidia Anjella baada ya Harmonize kumkimbia

Baba Levo ahaidi kumsaidia Anjella baada ya Harmonize kumkimbia

Sakata la Harmonize na msanii wake Anjella limemgusa mwanamuziki wa Bongofleva Baba Levo ambaye ameweka wazi atamsaidia msanii huyo matibabu ya mguu wake kwa kumpeleka India na Qatar. Kupitia ukurasa wake instagram Baba Levo amesema “Dada Anjella Naitwa Baba Levo NAKUHAKIKISHIA UTAENDA QATAR NA UTAENDA INDIA PIA KWA AJILI YA MATIBABU …!! KIRANDAGE PAMOJA NA BANGE ZAKE ILA AMEKUTOA MBALI SEMA TU AMEISHIWA HELA KWA SASA NA HII NI KWASABABU YA KUTAKA KUSHINDANA NA DIAMOND PLATINUMZ AMEJIKUTA AMEFILISIKA KABISA…!” Ikumbukwe, jana Harmonize kupitia insta story yake aliweka ujumbe akitaka mtu yeyote anaeweza kuendeleza kipaji cha Anjella asisite kujitokeza kwa ajili ya kumsaidia msanii huyo. Hata hivyo, kwenye ujumbe huo boss huyo wa Konde Gang hakuweka wazi kama lebo yake ndio imeachana rasmi na Anjella.

Read More
 Harmonize akanusha kumdai Anjella shillingi millioni 52

Harmonize akanusha kumdai Anjella shillingi millioni 52

Bosi wa lebo ya Konde Music Worldwide, Msanii Harmonize ameamua kuvunja kimya chake juu ya stori zinazotembea mtandaoni kuhusu kumkimbia msanii wake Anjella. Kupitia instastoy yake Harmonize ameweka wazi kuwa ni kweli amefika mwisho wa kumsapoti Anjella, hivyo kwa yeyote mwenye uwezo anaruhusiwa kumshika mkono msanii huyo bila pingamizi. Hitmaker huyo wa “Leave Me Alone amesema kuwa hamdai pesa yoyote Anjella kama malipo ya kuachana na lebo ya Konde Gang huku akiwataka watu kupuuza mambo ya uongo yanayoendelea mtandaoni. “Nilikutana na Anjella akiwa amejikatia tamaa akiwa na ndoto kichwani, sikujiangalia nina kiasi gani niliamini kuwa wapo wanaonisapoti bila kuwalipa senti 5 basi watasapoti kipaji cha sister Anjella”. “Nilichoangalia ni ndoto hasa za mtoto wa kike nimejitahidi kadri ya uwezo wangu najua kuna wenye uwezo mkubwa kunizidi ukizingangatia nimeanza juzi” “Kama kuna anayeweza kumuendeleza kipaji chake ni faraja kwangu asisite kujitokeza. Puuzia siasa za kusema sijui namdai mahela sikumuuliza kuhusu pesa hata senti 1”

Read More