Apple Yazindua iPhone 17, iPhone 17 Pro na iPhone Air

Apple Yazindua iPhone 17, iPhone 17 Pro na iPhone Air

Kampuni ya Apple imezindua rasmi simu mpya ya iPhone 17, ambayo japokuwa muonekano wake unafanana na iPhone 16, imeboreshwa kwa kiwango kikubwa upande wa teknolojia. Sasa inakuja na skrini ya ProMotion inayowezesha refresh rate hadi 120Hz, badala ya 60Hz ya toleo lililopita. Pia, ina kamera kuu ya 48MP, kioo cha Ceramic Shield 2 kilichoimara zaidi dhidi ya michubuko na ajali, pamoja na teknolojia mpya ya kuchaji haraka. Kwa upande mwingine, Apple imezindua pia iPhone 17 Pro, ikiwa na mabadiliko makubwa zaidi. Toleo hili linatumia heat-forged aluminium badala ya titanium, na muundo wa kamera ya nyuma umeboreshwa. Kamera zote ni 48MP, ina zoom ya hadi 8x, na sasa inakuja na lens mpya ya 200mm, ikiwa ni moja ya simu zenye uwezo mkubwa zaidi wa upigaji picha na video kwa sasa. Uzinduzi huu pia umeleta mshangao kwa wengi baada ya Apple kutambulisha iPhone Air, simu mpya kabisa isiyo na jina la namba tofauti na utaratibu wa kawaida. iPhone Air ni iPhone nyembamba zaidi kuwahi kutengenezwa, lakini yenye uwezo wa kifaa cha kiwango cha juu kama iPhone 17 Pro. Inakuja na kamera ya 48MP, lensi za 26mm hadi 52mm, selfie kamera ya 24MP, uwezo wa kurekodi 4K kwa 60fps, na inatumia chip ya iPhone Pro. Kutokana na muundo wake wa kisasa, classic na wa kuvutia, iPhone Air tayari imeanza kushika kasi mtandaoni, huku watumiaji wengi wakionesha kuvutiwa na muonekano wake wa kipekee pamoja na uwezo wa hali ya juu, licha ya mwonekano wake mwembamba. Apple inaendelea kuonesha kwamba teknolojia ya simu janja bado ina nafasi kubwa ya ubunifu.

Read More
 iPhone 17 Pro Kutambulishwa Rasmi Kesho Usiku na Apple

iPhone 17 Pro Kutambulishwa Rasmi Kesho Usiku na Apple

Kampuni ya Apple inatarajiwa kuzindua rasmi simu zake mpya za mwaka huu usiku wa kesho, katika hafla maalum itakayofanyika saa 2 usiku kwa saa za Afrika Mashariki. Katika uzinduzi huo, Apple inatarajiwa kuonyesha kwa mara ya kwanza hadharani matoleo mapya ya iPhone 17 Pro na iPhone 17 Pro Max, ambayo yamesemwa kuwa yatakuja na mabadiliko makubwa ya kimwonekano na kiteknolojia, ikilinganishwa na vizazi vya awali vya iPhone. Mbali na matoleo hayo, Apple pia inatarajiwa kutangaza simu mpya kabisa kwa jina iPhone Air aina ambayo haijawahi kuwepo katika familia ya iPhone. Taarifa kutoka kwa wachambuzi wa teknolojia zinasema kuwa iPhone Air huenda ikawa simu nyepesi zaidi kwa uzito, yenye kioo cha kisasa na betri yenye ufanisi mkubwa, ikiwa imelenga kuvutia watumiaji wanaopendelea unyumbufu na muonekano wa kifahari. Sambamba na uzinduzi wa simu hizo, Apple pia itatoa toleo jipya la mfumo wa uendeshaji wa iOS, ambalo litaanza kupatikana kwa watumiaji wote wa iPhone kuanzia iPhone 11 hadi iPhone 16. Maboresho hayo yanatarajiwa kuleta vipengele vipya vya usalama, muonekano, pamoja na utendaji wa hali ya juu unaolenga kuboresha uzoefu wa mtumiaji.

Read More
 Apple Yatangaza Uzinduzi wa Vifaa Vipya Jumanne ya Septemba 9

Apple Yatangaza Uzinduzi wa Vifaa Vipya Jumanne ya Septemba 9

Kampuni ya teknolojia ya Apple imetangaza kuwa itafanya hafla rasmi ya kutambulisha vifaa vyake vipya siku ya Jumanne, Septemba 9, kuanzia saa 2 usiku kwa saa za Afrika Mashariki. Katika hafla hiyo, Apple inatarajiwa kuzindua rasmi iPhone 17 katika matoleo yake yote ya mwaka huu, pamoja na AirPods Pro 3 na toleo jipya la Apple Watch. Mbali na vifaa hivyo, Apple pia itazindua mfumo mpya wa uendeshaji wa iOS 26, ambao utaanza kupatikana rasmi kwa watumiaji wote wa iPhone wanaotumia vifaa vinavyokubaliana na toleo hilo jipya. Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika kwa njia ya kidijitali kupitia mtandao rasmi wa Apple na huduma za utiririshaji (livestream), huku mashabiki wa teknolojia duniani kote wakisubiri kwa hamu kuangalia maboresho na vipengele vipya katika bidhaa hizo maarufu. iPhone 17 inatarajiwa kuja na mabadiliko makubwa katika muundo, kamera na utendaji wa mfumo, huku AirPods Pro 3 zikiripotiwa kuwa na teknolojia mpya ya sauti na uunganishaji wa kasi zaidi. Apple Watch mpya nayo huenda ikaleta maboresho ya kiafya, betri na mawasiliano. Watumiaji wa bidhaa za Apple, wadau wa teknolojia, na wachambuzi wa soko watakuwa wakifuatilia kwa karibu hafla hii muhimu inayoweka mwelekeo wa vifaa vya kidijitali kwa mwaka 2025 na kuendelea.

Read More
 Apple Yatangaza iPhone Mpya Yenye Vioo Viwili

Apple Yatangaza iPhone Mpya Yenye Vioo Viwili

Kampuni ya teknolojia ya Apple, inatarajiwa kuzindua toleo jipya la iPhone ambalo linatajwa kuwa tofauti kabisa na matoleo ya awali. Taarifa kutoka kwa vyanzo vya karibu na kampuni hiyo zinaeleza kuwa iPhone hiyo mpya itakuwa na vioo viwili, hatua ambayo imeibua mjadala mkubwa miongoni mwa wapenzi wa teknolojia duniani. Kioo cha kwanza kitakuwa kikubwa na cha ndani, kama ilivyo kawaida kwa simu za iPhone. Lakini kipya zaidi ni kioo cha nje ambacho kitakuwa na ukubwa wa inchi 5.5, sawa kabisa na simu ya kawaida. Kioo hicho cha nje kinatarajiwa kuwa na uwezo wa kuonyesha taarifa muhimu kama muda, ujumbe mfupi, arifa, na hata kutumia baadhi ya apps bila kulazimika kufungua kioo kikuu. Hii ni mara ya kwanza kwa Apple kujaribu rasmi teknolojia ya simu yenye vioo viwili, teknolojia ambayo tayari imejaribiwa na makampuni kama Samsung kupitia simu zake za “foldable”. Tofauti na simu zinazokunjwa, iPhone hii mpya haikunjiki, bali inakuwa na kioo cha pili kwa matumizi ya haraka na ya nje. Hadi sasa, Apple haijatoa tarehe rasmi ya uzinduzi wa iPhone hii, lakini matarajio ni kwamba itazinduliwa katika tukio kubwa la uzinduzi wa bidhaa za Apple ambalo hufanyika kila Septemba.

Read More
 Apple Kutambulisha Mfumo Mpya wa Uendeshaji kwa Vifaa vya Nyumbani

Apple Kutambulisha Mfumo Mpya wa Uendeshaji kwa Vifaa vya Nyumbani

Kampuni ya Apple imeanza kutengeneza mfumo mpya wa uendeshaji (operating system) ambao unalenga kubadilisha kabisa jinsi vifaa vya nyumbani vinavyofanya kazi. Taarifa zinaeleza kuwa mfumo huo mpya utafanya kazi katika aina mbalimbali za vifaa vya nyumbani kama spika zenye skrini ndogo, roboti wa usafi (cleaning robots), vifaa vya kielektroniki vya nyumbani, na vifaa vya kiusalama kama vile kufuli za milango. Mfumo huo unatajwa kuwa na muundo unaofanana na tvOS na watchOS, mifumo ambayo tayari inatumika katika Apple TV na saa janja za Apple. Lengo kuu ni kufanya vifaa vya Apple viweze kuzungumza kwa urahisi kupitia jukwaa moja la kipekee, lenye uwezo wa kutumia akili bandia (AI) na huduma za kisasa kama Siri na FaceID. Kwa mujibu wa vyanzo vya ndani, mfumo huu mpya utawezesha vifaa kutumia FaceID kwa kufuli za milango, huku Siri ikibaki kuwa kiini cha mawasiliano kati ya mtumiaji na kifaa. Aidha, mfumo huu utakuja na programu muhimu kama Kalenda, Kamera, Muziki, Notes pamoja na Siri kama msaidizi wa kidijitali. Apple inatarajia kuzindua rasmi mfumo huu mwishoni mwa mwaka huu au mapema mwaka 2026, hatua ambayo inatazamiwa kuleta mapinduzi makubwa katika teknolojia ya nyumbani na kuweka Apple katika nafasi nzuri ya kushindana katika soko la smart home devices. Mashabiki wa teknolojia na watumiaji wa vifaa vya Apple wanasubiri kwa hamu kuona mapinduzi haya mapya yatakavyoleta urahisi, usalama na ufanisi zaidi katika maisha ya kila siku ya nyumbani.

Read More
 FaceTime Kuanzisha Teknolojia ya Kuzuia Video Call Endapo Mtumiaji Atavua Nguo

FaceTime Kuanzisha Teknolojia ya Kuzuia Video Call Endapo Mtumiaji Atavua Nguo

Kampuni ya Apple imeanzisha teknolojia mpya ya usalama katika huduma ya FaceTime, itakayoweza kusitisha simu za video pale ambapo itabainika kuwa mtumiaji amevua nguo au kutumia lugha ya matusi wakati wa mawasiliano. Hatua hii inalenga kulinda watumiaji dhidi ya unyanyasaji wa kingono na maudhui yasiyofaa. Teknolojia hiyo mpya, inayotegemea akili bandia (AI), itaweza kutambua si tu picha za utupu bali pia sauti zenye matusi au lugha ya kudhalilisha. Endapo mfumo huo utagundua maudhui hayo, FaceTime itakatiza mazungumzo mara moja na kutoa arifa kwa mtumiaji aliyeathirika, huku ikimpa chaguo la kuripoti tukio hilo. Apple imesema kuwa uchakataji wa data utafanyika moja kwa moja kwenye kifaa (on-device processing), ili kulinda faragha ya mtumiaji bila kutuma data hizo kwenye seva za kampuni. Watumiaji wengi wamesifia hatua hiyo wakisema inasaidia kudhibiti unyanyasaji wa kimtandao, hasa kwa watoto na watu wazima wanaolengwa na wanyanyasaji kupitia simu za video. Maboresho haya mapya yanatarajiwa kuzinduliwa rasmi kupitia toleo la hivi punde la iOS, litakalotoka msimu wa vuli (Fall) mwaka huu. Apple inatarajia FaceTime kuendelea kuwa mojawapo ya majukwaa salama zaidi ya mawasiliano ya video duniani.

Read More
 iPhone Yapanua Uwezo wa Kuhamisha eSIM kwa Simu za Android

iPhone Yapanua Uwezo wa Kuhamisha eSIM kwa Simu za Android

Apple imezindua mfumo mpya wa iPhone ambao utarahisisha uhamisho wa eSIM kati ya simu za Android na iPhone. Mfumo huu mpya unalenga kutoa suluhisho rahisi na salama kwa watumiaji wanaotaka kubadilisha simu zao bila shida ya kuondoa na kuweka kadi za simu za kawaida. Sehemu hii mpya ya kuhamisha eSIM itawawezesha watumiaji kuhamisha taarifa za eSIM kwa urahisi zaidi, bila kuhitaji kutumia kadi za simu za kawaida au kutafuta msaada wa wataalamu wa simu. Hii ni hatua muhimu kwa watumiaji wa Android wanaohamia iPhone, kwani imekuwa changamoto kwa muda mrefu kuhamisha namba zao na mipango ya simu kupitia eSIM. Mfumo huu unatarajiwa kuja kama sehemu ya toleo lijalo la iOS na utakuwa ni sehemu ya juhudi za Apple za kuboresha uzoefu wa watumiaji na kuongeza usaidizi wa teknolojia ya eSIM kwa wateja wake. Watumiaji wanahimizwa kusasisha simu zao ili kufurahia huduma hii mpya itakayowezesha uhamishaji wa eSIM kwa urahisi na haraka zaidi kuliko hapo awali.

Read More
 Apple Yaja na Kipengele Kipya cha Kudhibiti Betri kwa Akili Bandia Kupitia iOS 19

Apple Yaja na Kipengele Kipya cha Kudhibiti Betri kwa Akili Bandia Kupitia iOS 19

Kampuni ya Apple imetangaza kuwa mfumo wao mpya wa uendeshaji, iOS 19, utakuja na kipengele cha kipekee cha kudhibiti matumizi ya betri kwa kutumia akili bandia (AI). Teknolojia hii mpya inalenga kuongeza ufanisi wa matumizi ya nishati kwenye simu kwa kuzingatia tabia ya mtumiaji. Kwa mfano, iOS 19 itaweza kutambua ni programu zipi unazotumia mara kwa mara na kwa muda gani, kisha itadhibiti matumizi ya umeme kulingana na hilo. Kipengele hiki kitaendesha kazi zake moja kwa moja bila kuhitaji usaidizi wa mtumiaji, na kitajifunza tabia zako kwa muda ili kupunguza matumizi yasiyo ya lazima. Hii ina maana kuwa simu yako itaweza kuhifadhi chaji kwa muda mrefu zaidi, bila kuathiri utendakazi wa programu muhimu unazozitumia kila siku. Mbali na hayo, Apple pia itaongeza kiashiria kipya kwenye skrini ya kufunga (lock screen), ambacho kitaonyesha makadirio ya muda unaohitajika kuchaji simu yako hadi kufikia asilimia 100. Kiashiria hicho kitaongozwa na hali ya afya ya betri yako, matumizi yako ya simu, pamoja na programu zinazoendelea kufanya kazi. Hii ni mara ya kwanza kwa kampuni ya simu kutumia AI kwa njia ya moja kwa moja katika kuboresha maisha ya betri kwa kiwango hiki.apple

Read More
 Apple imesogeza mbele mradi wa kutengeneza magari yasiyo na usukani

Apple imesogeza mbele mradi wa kutengeneza magari yasiyo na usukani

Kampuni ya Apple imesogeza mbele mradi wake (Project Titan) wa kutengeneza magari yasiyo na usukani wala pedeli hadi mwaka 2026. Hii ni kutokana na uhaba wa teknolojia lakini pia kutikisika kwa uongozi wa timu ya wahandisi. Tangu mwaka 2014, kampuni hiyo iliweka wazi kuja na mradi huo ambao magari yatakuwa yakijiendesha kiteknolojoa ‘Automatic’ pasina dereva kutumia usukani wala kukanyaga pedeli chini. Kwa mujibu wa taarifa, magari hayo ya Apple yataingia sokoni kwa bei ya ($100,000) zaidi ya KSh. Milioni 12

Read More
 APPLE WAONDOA UDHAMINI WAO KWA KANYE WEST BAADA YA KUTANGAZA MSIMAMO WAKE KUHUSU ALBUM YA DONDA 2

APPLE WAONDOA UDHAMINI WAO KWA KANYE WEST BAADA YA KUTANGAZA MSIMAMO WAKE KUHUSU ALBUM YA DONDA 2

Kampuni ya Apple imetangaza kuondoa kiasi cha shilling billion 2.3 pamoja na kuondoa udhamini wake kwa Kanye West ambaye mishoni mwa wiki iiliyopita alitangaza rasmi kuwa album yake mpya “DONDA 2” itapatikana kwenye Jukwaa lake la ‘Strem Player’ kifaa maalum cha kusikiliza muziki. Kupitia ukurasa wake wa instagram wiki iiliyopita, Kanye West alifunguka makubwa ikiwemo kuyakandia maduka maarufu ya kuuza muziki mtandaoni ikiwemo Apple, Amazom, Spotify na YouTube akisema kwamba inawanyonya wasanii ambao hupata asilimia 12 pekee kwenye kazi zao. Hivyo ni muda wa wasanii kuanzisha maduka yao ya kuuza muziki. Stem Player, ni kifaa maalum ambacho kitauzwa kwa zaidi ya shilling elfu 19. Kwa mujibu wa The Daily Mail, Kanye West tayari ametengeneza kiasi cha shilling million 154 ikiwa ni ndani ya masaa 12 ya tangazo lake.

Read More