Msanii Parroty Aingia Kwenye Bifu Kali na Militan Baada ya Kunyoa Dreadlocks Zake Bila Ridhaa

Msanii Parroty Aingia Kwenye Bifu Kali na Militan Baada ya Kunyoa Dreadlocks Zake Bila Ridhaa

Msanii Parroty ameingia kwenye bifu kali na mwenzake Militan kufuatia tukio la kushangaza lililotokana na mzaha wa soka. Parroty, ambaye ni shabiki mkubwa wa Manchester United, awali alitania kuwa angenyoa dreadlocks zake endapo timu yake ingepoteza dhidi ya Tottenham. Baada ya United kufungwa 1-0, hali ilichukua mkondo mpya. Mzaha huo sasa umegeuka kuwa chanzo cha mgogoro mkubwa baada ya Militan kumvamia Parroty na kumnyoa dreadlocks zake bila idhini. Paroty, kupitia mitandao ya kijamii, alielezea hasira na kukerwa kwake na tukio hilo, akilitaja kama udhalilishaji wa hali ya juu. “Hii imevuka mpaka. Sio kila kitu ni mchezo. Sikutegemea nishambuliwe kwa sababu ya maneno ya mzaha,” alisema Paroty, akionya kuwa iwapo watakutana na Militan ana kwa ana, huenda mambo yakaenda kombo. Mashabiki wameingia kwenye malumbano, baadhi wakidai Parroty alipaswa kutimiza ahadi yake, huku wengine wakimtetea wakisema tukio hilo lilikiuka heshima na haki za mtu binafsi. Kwa sasa, Militan bado hajajibu hadharani, huku mvutano ukizidi kuongezeka na tasnia ya burudani ikisubiri kuona hatma ya bifu hilo linalozidi kushika kasi.

Read More
 Msanii Tipsy Gee Amshutumu Militan wa Mbogi Genje kwa Kukata Dreadlocks za Parroty kwa Mabavu

Msanii Tipsy Gee Amshutumu Militan wa Mbogi Genje kwa Kukata Dreadlocks za Parroty kwa Mabavu

Msanii wa muziki wa Arbantone, Tipsy Gee, amezua mjadala mkali mtandaoni baada ya kumkemea vikali Militan, mmoja wa wanachama wa kundi la rap maarufu Mbogi Genje, kwa kile alichokiita kitendo cha kumvamia yeye na rafiki yake, Parroty, na kumnyoa dreadlocks zake kwa nguvu bila ridhaa yake. Tukio hilo lilitokea baada ya Parroty awali kuahidi kukata rasta zake endapo timu yake ya Manchester United ingefungwa na Tottenham Hotspur. Hata hivyo, licha ya Tottenham kushinda mechi hiyo, Parroty alibadilisha msimamo wake na kuomba msamaha kwa mashabiki, akisema kuwa angeacha kuishabikia Manchester United badala ya kukata rasta zake. Kwa mujibu wa Tipsy Gee, Militan alichukua sheria mkononi kwa kumshambulia Parroty na kumkata nywele bila makubaliano, kitendo ambacho kimezua hasira na lawama kutoka kwa wafuasi wa Parroty na wapenzi wa muziki wa mtaa. Mashabiki wengi wamejitokeza mitandaoni kulaani tukio hilo, wakilitaja kama ukiukaji wa haki ya mtu binafsi na ukosefu wa heshima. Wengine wameitaka Mbogi Genje kutoa msimamo rasmi kuhusu tukio hilo, huku wengine wakitaka hatua za kisheria zichukuliwe. Hadi sasa, Militan hajatoa tamko lolote rasmi kuhusiana na madai hayo. Tukio hili linaendelea kuzua mjadala mpana kuhusu mipaka ya mizaha, ahadi za mashabiki wa soka, na heshima kwa maamuzi ya mtu binafsi.

Read More