Arrow Bwoy Aitetea Taasisi ya Ndoa

Arrow Bwoy Aitetea Taasisi ya Ndoa

Msanii kutoka Kenya, Arrow Bwoy, ameingilia kati mjadala unaoendelea mitandaoni kuhusu mada ya “Marriage hubamba mafala” iliyoanzishwa na socialite Chebet Ronoh. Chebet alizua gumzo kubwa akidai kwamba ndoa ni ya mafala (wajinga), kauli ambayo imewagawa mashabiki mtandaoni. Wengi wamekuwa wakitoa maoni tofauti, huku baadhi wakiunga mkono na wengine kupinga vikali. Akizungumza kwa mtazamo wake, Arrow Bwoy amesema kuwa yeye binafsi haoni tatizo la ndoa na anajivunia maisha ya kifamilia. Ameongeza kuwa wao kama vijana hawapaswi kubeza ndoa kwa sababu hata wazazi wao waliishi katika ndoa na wakafanikiwa kulea familia zao. Kwa maoni yake, ndoa ni jambo la hiari na lina pande mbili, nzuri na mbaya na kushindwa kwa mtu mmoja hakumaanishi kwamba taasisi ya ndoa haina maana kwa kila mtu. Msanii huyo amesisitiza kuwa kuanzisha mitazamo ya kupinga ndoa kunaweza kuwapotosha vijana, akihimiza kila mtu afanye maamuzi kulingana na maisha yake binafsi.

Read More
 Arrow Bwoy Atoa Wimbo Mpya Baada ya Kupigwa na Polisi

Arrow Bwoy Atoa Wimbo Mpya Baada ya Kupigwa na Polisi

Msanii maarufu wa muziki wa Dancehall, Arrow Bwoy, ameibua hisia kali mitandaoni baada ya kuachia wimbo mpya wenye ujumbe mzito unaogusa madhila ya ukatili wa polisi, kufuatia tukio la kushangaza alilokumbana nalo katika maandamano ya hivi karibuni jijini Nairobi. Katika ujumbe wake wa wazi kwa umma kupitia mitandao ya kijamii, msanii huyo alieleza kuwa alinusurika kujeruhiwa vibaya baada ya kushambuliwa kwa nyahunyo na kukumbwa na gesi ya kutoa machozi wakati wa maandamano ya amani yaliyokuwa yakipinga sera tata za serikali na ukosefu wa uwajibikaji wa vyombo vya usalama. Alieleza kuwa hali hiyo ilimfanya kutambua uzito wa changamoto ambazo wananchi wa kawaida hukumbana nazo kila siku. “Sikuwahi jua kuwa siku moja nitakuwa mhanga wa ukatili wa polisi. Ninamshukuru Mungu nilirudi jana nyumbani nikiwa hai – wengine hawakurudi. Naamini kuwa tunaweza kuishi kwa amani iwapo sote tutafuata na kuheshimu sheria. Sikiliza wimbo wangu mpya, link ipo kwenye bio. Bado ni #Mapambano ✊🏿❤️🇰🇪.” Arrow Bwoy aliandika Instagram. Wimbo wake mpya, “Mapambano”, umetumika kama jukwaa la kuonyesha mshikamano na wananchi waliopoteza maisha au kujeruhiwa katika maandamano hayo, huku ukihimiza utulivu, mshikamano na utawala wa sheria kama njia ya kweli ya kusuluhisha tofauti za kijamii na kisiasa. Maandamano hayo, yaliyoongozwa na vijana katika zaidi ya kaunti 20 nchini Kenya, yameacha majeraha ya kitaifa baada ya taarifa rasmi kuthibitisha vifo vya watu wasiopungua 16 na wengine wengi kujeruhiwa. Tukio hilo limezua mjadala mpana kuhusu haki za kiraia, uhuru wa kujieleza na matumizi ya nguvu kupita kiasi na vikosi vya usalama. Arrow Bwoy, ambaye ni miongoni mwa wasanii wachache walioshuhudia na kuathirika moja kwa moja na vurugu hizo, sasa anatumia sauti yake ya kisanii kutoa mwito wa mabadiliko, akihimiza jamii kushikamana na kutafuta suluhisho kwa njia ya amani na haki.

Read More
 Wasanii Wapaza Sauti Kufuatia Kujeruhiwa kwa Arrow Bwoy na Polisi Wakati wa Maandamano ya Amani

Wasanii Wapaza Sauti Kufuatia Kujeruhiwa kwa Arrow Bwoy na Polisi Wakati wa Maandamano ya Amani

Tukio la kujeruhiwa kwa msanii mashuhuri wa muziki wa Kenya, Arrow Bwoy, na polisi wakati wa maandamano ya amani limezua taharuki kubwa mitandaoni na kusababisha wasanii wenzake kuibua hisia kali za hasira na kukemea ukatili wa polisi. Arrow Bwoy alikuwa ameungana na rapa maarufu Khaligraph Jones pamoja na raia wengine katika maandamano ya kupinga ukatili wa vyombo vya usalama. Hata hivyo, maandamano hayo yaliishia kwa vurugu baada ya polisi kuwatawanya waandamanaji kwa kutumia mabomu ya machozi na nguvu kupita kiasi, hali iliyomwacha Arrow Bwoy amejeruhiwa. Khaligraph Jones alilalamikia tukio hilo kupitia mitandao ya kijamii, akisema kwa uchungu kuwa waandamanaji walikuwa wakifanya maandamano kwa amani, lakini walishambuliwa na polisi waliokuwa wakifyatua mabomu ya machozi moja kwa moja kwao. Alisema kitendo hicho ni mfano tosha wa ukatili wa polisi unaopaswa kukomeshwa mara moja. “Unapofanya maandamano ya amani halafu wanaanza kukupiga risasi za mabomu ya machozi… Kukomesha ukatili wa polisi nchini Kenya ni muhimu sana. #RespectTheOGs,”  Alielezea kwa uchungu Khaligraph Jones, ambaye alikuwa sambamba na Arrow Bwoy wakati wa maandamano hayo. Naye mchumba wa Arrow Bwoy na mama wa mtoto wake, Nadia Mukami, alionekana kuguswa sana na tukio hilo. Kupitia ujumbe alioutuma mtandaoni, aliandika kwa hasira kuwa polisi hawapaswi kumshika baba wa mtoto wake na kutaka ukatili huo ukome mara moja. “Nyinyi mafala msimguse baba watoto wangu!!!! #EndPoliceBrutality Nimejam ata!!!!!,” Aliandika kwa hasira Instagram. Kauli za wasanii hao zimeungwa mkono na maelfu ya mashabiki na wakenya wa kawaida, huku wengi wakitumia mitandao ya kijamii kulaani hatua ya polisi kutumia nguvu dhidi ya waandamanaji wa amani. Hashtag kama #EndPoliceBrutality na #RespectTheOGs zimeendelea kutrendi huku wito ukitolewa kwa serikali kuwajibisha maafisa waliohusika. Tukio hili limezua mjadala mpana kuhusu haki ya kuandamana na uhuru wa kujieleza nchini Kenya, huku wasanii wakionyesha kuwa wako tayari kusimama na wananchi kupigania haki na mabadiliko katika jamii.

Read More
 Msanii Arrow Bwoy Ajeruhiwa Vibaya na Polisi Katika Maandamano ya Amani Jijini Nairobi

Msanii Arrow Bwoy Ajeruhiwa Vibaya na Polisi Katika Maandamano ya Amani Jijini Nairobi

Msanii maarufu wa muziki nchini Kenya, Arrow Bwoy, amejeruhiwa vibaya baada ya kushambuliwa na afisa wa polisi wakati wa maandamano ya amani yaliyofanyika jijini Nairobi. Maandamano hayo yaliandaliwa kwa lengo la kushinikiza haki kufuatia kifo cha Albert Ojwang, bloga na mwalimu mchanga aliyefariki akiwa mikononi mwa polisi. Tukio hilo lilijiri mbele ya mashuhuda kadhaa, huku video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonesha Arrow Bwoy akipigwa kichwani na afisa wa polisi, licha ya kuwa hakuwa na silaha wala hakukuwa na ishara yoyote ya vurugu kutoka kwake. Msanii huyo alikuwa amesimama kwa amani miongoni mwa waandamanaji wengine wakati alipopigwa ghafla. Video hiyo imezua ghadhabu kubwa miongoni mwa wananchi, wanaharakati wa haki za binadamu, na wadau wa tasnia ya muziki, wakilaani vikali matumizi ya nguvu kupita kiasi na ukatili wa polisi dhidi ya raia wasio na hatia. Tukio hili linatokea siku chache tu baada ya video nyingine kuibuka ikimuonesha polisi akimpiga risasi kwa karibu mfanyabiashara wa barakoa aliyekuwa akiandamana kwa amani. Mwanaume huyo alipigwa kichwani na kwa sasa amelazwa hospitalini akiwa katika hali mahututi. Wito umetolewa kwa taasisi husika, ikiwemo IPOA (Independent Policing Oversight Authority) na Tume ya Haki za Binadamu, kuchukua hatua za haraka na za wazi ili kuwajibisha waliohusika na kuhakikisha kuwa haki inatendeka kwa wahanga wote wa ukatili huu wa polisi.

Read More
 Nadia Mukami Afichua Mpango wa Kufunga Kizazi Baada ya Mtoto wa Pili

Nadia Mukami Afichua Mpango wa Kufunga Kizazi Baada ya Mtoto wa Pili

Mwanamuziki maarufu wa Kenya, Nadia Mukami, ameweka wazi mpango wake wa kufunga kizazi (tubal ligation) baada ya kujifungua mtoto wake wa pili. Kupitia mahojiano yake hivi karibuni, Nadia alisema kuwa tayari amefikiria kwa kina kuhusu maamuzi ya uzazi na anahisi kuwa watoto wawili ni wa kutosha kwake. “Nikipata mtoto wangu wa pili, nafunga kabisa. Sina mpango wa kuzaa tena baada ya hapo,” alisema Nadia kwa uwazi. Nadia Mukami na mpenzi wake Arrow Bwoy tayari ni wazazi wa mtoto mmoja, na wawili hao wamekuwa wakionyesha maisha yao ya kifamilia kwa uwazi kupitia mitandao ya kijamii. Hata hivyo, Nadia sasa anaweka mipango thabiti ya kuhakikisha anadhibiti idadi ya watoto kwa namna anayoihisi inamfaa kiafya na kimaisha. Uamuzi wake umeibua mjadala mkubwa mitandaoni, huku baadhi ya mashabiki wakimpongeza kwa kuchukua msimamo wa wazi kuhusu afya ya uzazi, na wengine wakijadili suala hilo kwa mtazamo wa kijamii na kidini. Nadia Mukami anaendelea kuwa sauti muhimu si tu katika muziki, bali pia kwenye mijadala ya kijamii kuhusu afya ya wanawake na maamuzi ya uzazi. Kwa sasa, mashabiki wake wanaendelea kumuunga mkono huku wakisubiri kwa hamu kazi zake mpya na hatua zake za kibinafsi.

Read More
 Nadia Mukami Afunguka Sababu ya Kuahirisha Harusi Yake na Arrow Bwoy

Nadia Mukami Afunguka Sababu ya Kuahirisha Harusi Yake na Arrow Bwoy

Msanii maarufu wa muziki wa Kenya, Nadia Mukami, amefichua kwamba yeye na mchumba wake, Arrow Bwoy, walilazimika kuahirisha harusi yao baada ya kugundua kwamba walikuwa wanatarajia mtoto wao wa pili. Kupitia mahojiano ya hivi karibuni, Nadia ambaye anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Overdose’ alieleza kuwa walikuwa tayari wameweka mikakati yote muhimu kwa ajili ya tukio hilo maalum, lakini ujio wa mtoto mpya uliwalazimu kuahirisha harusi hiyo. “Tulikuwa tumepanga kila kitu, lakini sasa tumelazimika kuifuta,” alisema Nadia kwa huzuni lakini pia kwa matumaini. Ingawa mashabiki wengi walikuwa na matarajio makubwa ya kushuhudia harusi hiyo ya wanamuziki wawili maarufu, Nadia alisisitiza kuwa afya na ustawi wa familia yao ni jambo la kipaumbele kwa sasa. Hata hivyo, hakufunga mlango wa uwezekano wa harusi hiyo kufanyika siku za usoni Nadia na Arrow Bwoy, ambao walimpokea mtoto wao wa kwanza mwaka wa 2022, wamekuwa wakiendelea kudumisha uhusiano wao wa kimapenzi hadharani huku wakishirikiana pia katika kazi za muziki.

Read More
 ARROW BOY AMKINGIA KIFUA NADIA MUKAMI KWA KUKOSOLEWA MTANDAONI

ARROW BOY AMKINGIA KIFUA NADIA MUKAMI KWA KUKOSOLEWA MTANDAONI

Msanii nyota nchini Arrow Boy ameshindwa kuvumilia watu wanaomkosoa baby mama wake Nadia Mukami kutokana na mavazi aliyovalia juzi kati kwenye onesho lake huko Meru. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Arrow Boy ameshangazwa namna watu wanavyomshambulia Nadia Mukami kwenye mitandao ya kijamii kwa mambo yasiokuwa na msingi huku akisema kuwa huenda ni mafanikio ya msanii huyo  ndio imepelekea baadhi ya watu kuanza kumchukia. “Watu huku nje roho zao zimejaa machungu just ready to explode like a time bomb….Why too much hate?” Ameandika Instagram. Hitmaker huyo wa Enjoy amesema watu waache kumuonea Nadia Mukami wivu kwenye  muziki wake kwa kuwa anazidi kuandika historia ya kipekee ambayo hajawahi fikiwa na msanii yeyote wa kike nchini. “As you keep hating, others are making history….Tuseme tu ukweli which female artist in Kenya has pulled a move @NadiaMukami pulled over the weekend in Meru since Kenya izaliwe? Hakuna…”  Ameongeza Arrow Boy

Read More
 ARROW BWOY MBIONI KUANZA ZIARA YAKE YA MUZIKI BARANI ULAYA

ARROW BWOY MBIONI KUANZA ZIARA YAKE YA MUZIKI BARANI ULAYA

Msanii nyota nchini Arrow Boy ametangaza kuanza kwa ziara yake ya kimuziki mwezi Mei mwaka wa 2022 barani ulaya Arrow boy ameipa ziara hiyo jina la Focus Album World Tour ambayo itaanza Mei 21, mwaka wa 2022 huko Nues nchini Ujerumani. Ziara hiyo inatarajiwa kupita kwenye miji mbalimbali ikiwemo Paris,Ufaransa Mei 28, Helsinki, Finland tarehe juni 3, na Zurich, Switzerland Juni 4, mwaka wa 2022. Focus Album World Tour  pia inatarajiwa kuzunguka kwenye miji mbalimbali nchini Ujerumani ikiwemo Berlin juni 5, Sturtgart juni 11 na Bremen juni 18 ila Arrow boy ameahidi kuweka wazi nchini zingine ambazo atafanya tour yake hiyo.

Read More
 NI RASMI SASA NADIA MUKAMI ANA UJA UZITO WA MPENZI WAKE ARROW BWOY

NI RASMI SASA NADIA MUKAMI ANA UJA UZITO WA MPENZI WAKE ARROW BWOY

Malkia wa muziki nchini Nadia Mukami pamoja na mpenzi wake Arrow Boy wanatarajiwa kupata mtoto wao wa kwanza hivi karibuni. Wapenzi hao wawili wamethibitisha taarifa hiyo kwenye uzinduzi wa wakfu wao uitwao Lola na Safari ambao unalenga kuwasaidia akina mama wachanga kupata huduma nzuri ya afya ya uzazi. Lakini pia wamedokeza kuwa walipata wazo la kuja na wakfu wa Lola na Safari kipindi ambacho Nadia Mukami alipoteza uja uzito wake mwaka wa 2021, hivyo wana mpango wa kuzindua kituo cha kuwahudumia akina mama wachanga ambao ukutana na changamoto wakati wa uja uzito. Nadia Mukami amekuwa akikanusha madai ya kuwa na uja uzito licha ya mashabiki kusisitiza kuwa ana mimba ya Arrow Boy kutokana na kitendo chake cha kuvalia mavazi makubwa. Utakumbuka Mapema mwaka huu hitmaker huyo wa ngoma ya maombi alifunguka kuwa alipoteza uja uzito wake mwaka wa 2021 lakini akahamua kutoweka wazi taarifa hiyo kwa mashabiki zake. Mwezi agosti mwaka wa 2021 Nadia Mukami na Arrow Boy walithibitisha kuwa wapenzi mara baada ya kuwa kwenye mahusiano ya siri kwa muda mrefu ambapo walienda mbali zaidi na kueleza kuwa waliahamua kuyaweka wazi mahusiano yao kwa sababu tayari walikuwa wamekuwa kiakili kuingia kwenye uhusiano wa kimapenzi.

Read More