Arsenal Watinga Raundi ya Nne Baada ya Kulaza Portsmouth 4-1

Arsenal Watinga Raundi ya Nne Baada ya Kulaza Portsmouth 4-1

Washika Mitutu, Arsenal, wamepiga hatua kubwa katika Kombe la FA baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Portsmouth katika mchezo wa raundi ya tano. Mashabiki wa Portsmouth walipata furaha ya mapema baada ya Bishop kufunga bao dakika ya 3 na kuipa timu yake uongozi. Hata hivyo, matumaini hayo yalidumu kwa muda mfupi tu, kwani Dozzell alijifunga dakika ya 8 na kuisawazishia Arsenal. Dakika ya 25, Martinelli alionyesha makali yake kwa kufunga bao la pili na kuipa Arsenal uongozi. Baada ya mapumziko, kijana huyo aliongeza bao la tatu dakika ya 51, kabla ya kukamilisha ‘hat-trick’ yake dakika ya 72 na kuhitimisha ushindi wa kishindo kwa Washika Mitutu. Matokeo haya yanawaweka Arsenal katika nafasi nzuri ya kuendeleza safari yao ya kutafuta taji la Kombe la FA huku mashabiki wakibaki na matumaini makubwa ya kutwaa kombe

Read More
 Arsenal Yadhibu Atlético Madrid Mabao 4-0 Uwanjani Emirates

Arsenal Yadhibu Atlético Madrid Mabao 4-0 Uwanjani Emirates

Klabu ya Arsenal imeanza kampeni zao za Ligi ya Mabingwa kwa kishindo baada ya kuichapa Atlético Madrid kwa mabao 4–0 katika mchezo uliopigwa usiku wa Jumanne kwenye uwanja wa Emirates, London. Timu hiyo ya kocha Mikel Arteta ilionyesha kiwango cha kuvutia katika kipindi cha pili, baada ya kipindi cha kwanza kumalizika bila timu yoyote kupata goli. Katika kipindi cha pili cha mchezo, Arsenal ilionyesha ubora wake kwa kufunga mabao manne ndani ya dakika 13. Gabriel Magalhãesalifungua ukurasa wa mabao kwa kichwa cha nguvu akimalizia mpira wa mkwaju wa bure kutoka kwa Declan Rice katika dakika ya 57. Dakika 7 baadaye, Gabriel Martinelli aliongeza bao la pili kwa shuti kali lililomshinda kipa Jan Oblak. Viktor Gyökeres alifunga mabao mawili kwa mfululizo katika dakika ya 67 na 70, akimaliza ukame wa mabao wa mechi tisa. Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta, amekiri kuwa timu yake ilicheza kwa umoja na ari, akisisitiza umuhimu wa kuendelea na kasi hii katika mechi zijazo. Kwa upande mwingine, kocha wa Atlético Madrid, Diego Simeone, alikiri makosa ya kiufundi yaliyosababisha kipigo hicho. Kwa ushindi huu, Arsenal inaendelea kuwa na rekodi safi ya ushindi katika makundi ya Champions League, ikiwa na pointi 9 na mabao 4 bila kuruhusu nyavu zao kuguswa. Atlético Madrid, licha ya kuanza vizuri, sasa ina pointi 3 baada ya mechi tatu.

Read More
 Arsenal Yaomboleza Kifo Cha Raila Odinga

Arsenal Yaomboleza Kifo Cha Raila Odinga

Klabu ya Arsenal imejiunga na mamilioni ya waombolezaji duniani kote kuomboleza kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Amolo Odinga, ikimtaja kama kiongozi mwenye maono, aliyependa maendeleo na kuhimiza amani. Kupitia taarifa rasmi, miamba hao wa soka wa Uingereza wametuma salamu za rambirambi kwa taifa la Kenya na familia ya Odinga, wakisema Raila alikuwa mtu mwenye ushawishi mkubwa na shabiki wa dhati wa timu hiyo. Raila alikuwa mashabiki maarufu wa Arsenal, akifuatilia kwa karibu michezo yao na kuhudhuria mechi kadhaa katika uwanja wa Emirates jijini London. Mara yake ya mwisho kushuhudia pambano la Arsenal ilikuwa mwezi Machi mwaka 2022, wakati kikosi hicho kilipomenyana na Liverpool. Kifo cha Raila Odinga kimezua majonzi makubwa si tu nchini Kenya bali pia duniani kote, huku viongozi, mashirika na mashabiki wa michezo wakitoa salamu za pole kwa familia yake na wananchi wa Kenya

Read More
 Arsenal Yaibuka na Ushindi Mnono Dhidi ya Manchester United Ugenini

Arsenal Yaibuka na Ushindi Mnono Dhidi ya Manchester United Ugenini

Klabu ya Arsenal imeanza msimu mpya kwa kishindo baada ya kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Manchester United katika uwanja wa Old Trafford, katika mechi ya kwanza ya msimu wa ligi kuu ya Uingereza. Bao pekee la mchezo huo lilifungwa mapema dakika ya 13 na beki mpya wa Arsenal, Riccardo Calafiori, aliyemalizia kona kwa ustadi na kuzamisha matumaini ya mashabiki wa nyumbani. Goli hilo lilitosha kuipa Arsenal alama zote tatu dhidi ya wapinzani wao wa jadi. Kwa ushindi huu, Arsenal inaendelea kuonyesha ubabe wake dhidi ya Mashetani Wekundu, ikiwa ni ushindi wao wa tano katika mechi sita za mwisho dhidi ya Manchester United. Aidha, The Gunners hawajapoteza mchezo katika dimba la Old Trafford kwa zaidi ya miaka mitatu, rekodi inayowapa morali kubwa katika mbio za ubingwa msimu huu. Manchester United, kwa upande wao, watalazimika kujitathmini mapema baada ya kuanza msimu kwa kipigo nyumbani. Mashabiki wao walionekana kukata tamaa mapema kutokana na ukosefu wa ubunifu katika safu ya ushambuliaji na mapungufu katika safu ya ulinzi.

Read More
 Kieran Tierney Arejea Celtic kwa Mkataba wa Miaka Mitano

Kieran Tierney Arejea Celtic kwa Mkataba wa Miaka Mitano

Klabu ya Celtic imethibitisha kumsajili beki wa kushoto Kieran Tierney kwa mkataba wa miaka mitano, akisajiliwa kama mchezaji huru baada ya kuachana rasmi na Arsenal. Tierney, mwenye umri wa miaka 28, anarudi nyumbani katika klabu alikolelewa kisoka, baada ya miaka sita ya kuichezea Arsenal tangu alipojiunga nao mwaka 2019 kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni 25. Katika kipindi chake na The Gunners, raia huyo wa Scotland alicheza jumla ya mechi 144 na kufunga mabao sita, akitoa mchango mkubwa hasa katika mafanikio ya awali ya kocha Mikel Arteta, ikiwa ni pamoja na kushinda Kombe la FA mwaka 2020. Usajili wa Tierney unachukuliwa kama hatua muhimu kwa Celtic, wakijaribu kuimarisha kikosi chao kwa msimu ujao wa Ligi ya Mabingwa Ulaya na kutetea ubingwa wa Ligi Kuu ya Scotland. Mashabiki wa Celtic wamepokea taarifa hiyo kwa shangwe, wakimkaribisha mchezaji ambaye si tu ni kipenzi chao bali pia ni zao la akademia ya klabu hiyo, na aliwahi kuwa nahodha chipukizi kabla ya kuondoka kuelekea Ligi Kuu ya England. Kwa sasa, mashabiki wanatazamia kuona iwapo kurejea kwa Tierney kutazidi kuimarisha safu ya ulinzi ya Celtic na kuwapa ushindani mkubwa ndani na nje ya nchi.

Read More
 Arsenal Yatoa Ofa ya Pauni 59 Milioni kwa Viktor Gyokeres wa Sporting

Arsenal Yatoa Ofa ya Pauni 59 Milioni kwa Viktor Gyokeres wa Sporting

Klabu ya Arsenal imeanza mazungumzo rasmi na wakala wa mshambuliaji wa Sporting Lisbon, Viktor Gyokeres, jijini Lisbon, Ureno. Lengo la mazungumzo hayo ni kuhakikisha wanamnasa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Sweden, ambapo tayari Arsenal imewasilisha ofa ya Pauni milioni 59. Ingawa mazungumzo bado yanaendelea, Sporting imeonyesha utayari wa kumwachia Gyokeres kwa kiasi hicho, kutokana na heshima aliyoionyesha klabu hiyo kwa kukataa kuondoka katika dirisha la usajili la majira ya baridi, licha ya kupokea ofa kubwa kutoka klabu mbalimbali. Gyokeres, ambaye mkataba wake unamalizika mwaka 2028, amekuwa na msimu wa kuvutia akiwa na Sporting, akifunga mabao 54 na kutoa asisti 13 katika mechi 52 za michuano yote. Arsenal inamtazama kama chaguo bora kuimarisha safu yake ya ushambuliaji kwa msimu ujao.

Read More
 Arsenal Yaizamisha Newcastle, Yajihakikishia Nafasi ya Pili na Tiketi ya Ligi ya Mabingwa

Arsenal Yaizamisha Newcastle, Yajihakikishia Nafasi ya Pili na Tiketi ya Ligi ya Mabingwa

Arsenal waliendeleza ubabe wao nyumbani kwa kuilaza Newcastle United kwa bao 1-0 katika mechi ya Ligi Kuu ya Uingereza iliyopigwa Jumapili, Mei 18, 2025, kwenye dimba la Emirates. Ushindi huo umeiwezesha The Gunners kufikisha pointi 71 na kuthibitisha nafasi yao ya pili kwenye msimamo wa ligi, nyuma ya mabingwa wa msimu huu, Liverpool. Katika mechi hiyo, Arsenal walitawala kwa muda mrefu na kuilazimisha Newcastle kucheza kwa tahadhari kubwa, huku wageni hao wakishindwa kutengeneza nafasi za wazi za kufunga. Bao pekee la mchezo lilipatikana dakika ya 55 kupitia kiungo Declan Rice, aliyefunga kwa kichwa baada ya kona ya Bukayo Saka. Newcastle, ambao wapo katika harakati za kuwania nafasi ya kufuzu kwa michuano ya Ulaya, walionekana kuandamwa na presha nzito kutoka kwa Arsenal katika vipindi vyote vya mchezo. Mashambulizi ya Arsenal yalikuwa ya kasi, huku safu ya kati na ya mbele ikidhibiti mchezo kwa ustadi. Kwa matokeo hayo, Newcastle wanasalia na alama 66, sawa na Chelsea na Aston Villa, na sasa wanategemea matokeo ya mwisho ya msimu ili kufuzu kwa mashindano ya bara Ulaya. Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta, aliwapongeza vijana wake kwa ushindi huo muhimu na kusema kuwa kurejea kwao katika Ligi ya Mabingwa ni ushahidi wa maendeleo ya klabu msimu huu. Mashabiki wa Arsenal walijitokeza kwa wingi na kusherehekea ushindi huo, wakitazamia kurejea kwa klabu yao katika jukwaa la kifahari barani Ulaya msimu ujao. Mashabiki wa soka sasa wanasubiri kwa hamu mechi ya mwisho ya msimu itakayoweka mambo bayana kuhusu nafasi za Ulaya.

Read More
 Arsenal yaibamiza Manchester City magoli 5-1 huku Man United ikikubali kichapo Old Trafford

Arsenal yaibamiza Manchester City magoli 5-1 huku Man United ikikubali kichapo Old Trafford

Klabu ya Arsenal iliibamiza Manchester city kipigo cha magoli matano kwa moja kwenye mechi ya ligi nchini England iliyochezwa leo ugani Emirates. Magoli ya Arsenal yalifungwa na Martin Odergard, Thomas Partey, Myles Lewis Skelly, Kai Havertz na Ethan Nwaneri dakika ya 2, 56, 62, 76 na 90+3 huku Earling Haaland akifungia Manchester city bao pekee la kufutia machozi dakika ya 55. Kwa matokeo hayo Arsenal anashikilia nafasi ya pili kwa pointi 50 nyuma ya vinara Liverpool ambao wana pointi 56 kwenye msimamo wa ligi kuu England. Manchester city iko katika nafasi ya nne na pointi ya 41. Kwengineko Manchester United imekubali kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa Crystal Palace katika dimbani la Old Trafford. Mabao ya mawili ya Jean Mateta dakika ya 64 na 89 yalitosha kabisa kuharibu wikiendi ya vijana wa Ruben Amorin, Manchester United iko nafasi ya 13 ikiwa na alama 29 baada ya michezo 24 kwenye Ligi Kuu ya Uingereza EPL Kwenye matokeo mengine iliyochezwa hii leo, Totenham Hotspurs akiwa ugenini dhidi ya Brentford alipata ushindi wa magoli mawili bila jibu. Magoli ya Spurs yalifungwa na Vitaly Janelt ambaye alijifunga dakika ya 29 na Paper  Matar Sarr dakika ya 87. Kwa matokeo hayo, Spurs anashikilia nafasi 14 ya na pointi 27 nyuma ya Brentford ambao wanashikilia nafasi 11 ya na pointi 31 kwenye msimamo wa ligi kuu nchini England.

Read More
 LIVERPOOL NA ARSENAL YATOKA SARE YA KUTOFUNGANA KWENYE MCHEZO WA CARABAO

LIVERPOOL NA ARSENAL YATOKA SARE YA KUTOFUNGANA KWENYE MCHEZO WA CARABAO

Liverpool imelazimishwa Suluhu tasa na Arsenal katika mchezo wa nusu fainali ya kwanza ya kombe la Carabao uliopigwa katika dimba la Anfield Januari 13 mwaka 2022. Arsenal walilazimika kucheza pungufu katika muda mwingi wa mchezo huo baada ya kiungo Granit Xhaka kuonesha kadi nyekundu mapema kipindi cha kwanza Hata hivyo Liverpool wameshindwa kutumia Mwanya huo na kutoa sifa kwa mbinu za mwalimu Mikel Arteta. Timu hizo zitarudiana juma lijalo katika dimba la Emirates kuamua Mshindi atakayetinga fainali ya michuano hiyo. Mshindi atakutana na Chelsea katika fainali

Read More
 MCHEZO WA ARSENAL DHIDI YA LIVERPOOL YASOGEZWA KISA CORONA

MCHEZO WA ARSENAL DHIDI YA LIVERPOOL YASOGEZWA KISA CORONA

Mchezo wa nusu fainali ya Carabao Cup, kati ya Liverpool dhidi ya Arsenal umesogezwa mbele, sababu kubwa ikiwa ni maambukizi ya Virusi vya Corona. Mchezo huo uliokuwa upigwe kesho Alhamisi kwenye Uwanja wa Anfield sasa utapigwa Januari 13 kisha marudio ni Januari 20, mwaka wa 2022. Liverpool chini ya Kocha Jurgen Klopp iliomba mchezo huo kusogezwa mbele kutokana na msaidizi wa kocha huyo, Pep Lijnders na wachezaji wengike kadhaa kuoata maambukizi ya Virusi vya Corona.

Read More