ASAP Rocky Azima Tetezi za Albamu ya Pamoja na Young Thug

ASAP Rocky Azima Tetezi za Albamu ya Pamoja na Young Thug

Rapa maarufu kutoka Marekani, ASAP Rocky, amevunja kimya na kuzima uvumi uliokuwa ukisambaa mitandaoni kuhusu uwezekano wa kutoa albamu ya pamoja na Young Thug. Tetezi hizo zilianza kushika kasi jana baada ya ASAP Illz, mmoja wa wanachama wa ASAP Mob, kuashiria uwezekano wa collabo hiyo kupitia ujumbe wa kuvutia kwenye mitandao ya kijamii. Hata hivyo, ASAP Rocky amekatisha matumaini ya mashabiki kupitia mtandao wa X kwa kuweka wazi kuwa hilo halipo kwenye mipango kwa sasa “FALESE MY BROTHER, UY SCUTI OTW” kwa tafsiri ya haraka: “Umesema uongo kaka, UY Scuti iko njiani”. Aliandika Kauli hiyo inaonyesha kuwa badala ya albamu ya pamoja, ASAP Rocky anajiandaa kuachia mradi wake binafsi unaoitwa UY Scuti, ambao tayari umeanza kuvutia hisia miongoni mwa mashabiki wake. Ingawa collabo kati ya Rocky na Thug bado ni ndoto kwa sasa, mashabiki sasa wanasubiri kwa hamu kufahamu zaidi kuhusu UY Scuti, huku wakifuatilia kila dalili kutoka kwa rapa huyo anayejulikana kwa ubunifu na mitindo isiyotabirika.

Read More
 ASAP ROCKY AMTOLEA UVIVU CHRIS BROWN KUPITIA WIMBO WAKE MPYA D.M.B

ASAP ROCKY AMTOLEA UVIVU CHRIS BROWN KUPITIA WIMBO WAKE MPYA D.M.B

Rapa kutoka Marekani Asap Rocky amemchana Chris Brown kwenye wimbo wake mpya (D.M.B) ambao umetoka Mei 5 Mwaka huu. Kwenye moja ya verse katika ngoma hiyo, A$AP Rocky amesema “I don’t beat my b*tch, I need my b*tch.” akihusisha na tukio la Chris Brown kumpiga Rihanna mwaka 2009. Jina la wimbo huo limefupishwa kuwa (D.M.B) ikiwa na maana ya “DAT$ MAH B!*$H.” Utakumbuka mwaka 2009 Chris Brown alimpiga Rihanna wakiwa kwenye gari na kumsababishia michubuko usoni kiasi cha kupelekea wawili hao kuachana. Chris Brown alihukumiwa kifungo cha nje miaka 5 huku akiwa chini ya uangalizi pamoja na kufanya kazi za Kijamii.

Read More
 ASAP ROCKY ATUPWA JELA KWA KUMILIKI SILAHA KINYUME CHA SHERIA

ASAP ROCKY ATUPWA JELA KWA KUMILIKI SILAHA KINYUME CHA SHERIA

Rapa kutoka Marekani Asap Rocky ametiwa mbaroni na polisi wakati akiwasili katika uwanja wa ndege wa Los Angeles Aprili 20 akitokea visiwani Barbados na ndege binafsi. Kwa mujibu wa mashahidi waliotazama tukio hilo, wameiambia tovuti ya TMZ kwamba rapa huyo alitiwa pingu na kuondoka pamoja na polisi. NBC wameripoti kwamba, Asap Rocky amekamatwa kufuatia tukio la November mwaka 2021 ambalo lilihusisha silaha ambapo mtu mmoja alidai rapa huyo alimpiga risasi 4 kwenye mkono wake wa kushoto. Haijafahamika bado tukio hilo lilitokea wapi lakini inasemekana kuwa kuna watu wamefungua kesi ya kushambuliwa na Rapa huyo mwaka wa 2021.

Read More
 MREMBO AMINA MUADDI AKANUSHA KUVUNJA PENZI LA RIHANNA NA ASAP ROCKY

MREMBO AMINA MUADDI AKANUSHA KUVUNJA PENZI LA RIHANNA NA ASAP ROCKY

Mrembo mbunifu wa viatu Amina Muaddi ameibuka na kukanusha taarifa za kulivunja penzi la Rihanna na Asap Rocky. Kupitia insta stories kwenye mtandao wa Instagram, mrembo huyo ameandika kwamba ameamua kufunguka kwa sababu taarifa hizo zinamvunjia heshima kwa kuwa Rihanna & A$AP Rocky ni watu ambao ana waheshimu kwa kiasi kikubwa sana. Kauli ya Mrembo huyo inakuja mara baada ya Mtu wa karibu na wawili hao kuuthibitishia mtandao wa TMZ kuwa stori za A$AP Rocky kumsaliti Rihanna na zile za kuachana hazina ukweli kwani wapenzi hao wako vizuri. Mapema jana ziliibuka stori hizo kupitia twitter na kusambaa kwenye mitandao yote duniani kwamba Riri ambaye ni mjamzito, ameachana na rapa AsapRocky mara baada ya kugundua kuwa anamsaliti kwa kutoka kimapenzi na mrembo mbunifu wa viatu kwenye kampuni ya Riri, Fenty aitwaye Amina Muaddi.

Read More
 TETESI ZA RIHANNA NA ASAP ROCKY ZASHIKA KASI MTANDAONI

TETESI ZA RIHANNA NA ASAP ROCKY ZASHIKA KASI MTANDAONI

Tetesi kutoka nchini Marekani zinaeleza kuwa mwanamuziki Rihanna amechana na mpenzi wake Asap Rock ambaye ndio baba mtoto wake mtarajiwa. Inadaiwa kuwa hii imetokana na Rihanna kumfumania mpenzi wake huyo akimsaliti na mmoja wa wabunifu wa viatu kutoka katika kampuni ya Fenty aitwaye Amina Mauddi. Tetesi hizo zinasema Asap Rocky na Amina Muaddi walianza mahusiano tangu mwezi Februari mwaka huu kwenye maonesho ya Paris Fashion Week. Taarifa hiyo imeenea kwa kasi kote mitandaoni haswa katika mtandao wa twitter baada ya mtumiaji mmoja wa mtandao huo kuvujisha taarifa hiyo. Jambo lililoifanya idadi kubwa ya mashabiki na wafuatiliaji wa wapenzi hao kuanza kutiririsha maoni mbalimbali kuhusu jambo hilo. Baadhi ya vyanzo vimeonesha kuwa huenda kukawa na ukweli wa fununu hizi. Rihanna na Asap Rock siku za hivi karibuni wamekuwa wakiingia kwenye trending kama moja ya wapenzi wenye kuvutia zaidi baada ya wawili hao kuweka bayana kuwa wanatarajia kupata mtoto siku za usoni.

Read More
 RIHANNA AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA KUHUSU UJA UZITO WAKE

RIHANNA AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA KUHUSU UJA UZITO WAKE

Staa wa muziki kutoka marekani Rihanna amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu ujauzito wake kwenye event yake ya Fenty Beauty Universe iliyofanyika Los Angeles Februari 11 mwaka huu. Akizungumza na Jarida la PEOPLE, Rihanna amefunguka kuhusu changamoto za kuwa mwanamitindo wakati akiwa mjamzito kwa kusema kuwa anafurahia kila hatua ya uja uzito wake na ndio maana anaacha tumbo lake wazi. Januari 31 mwaka huu Rihanna na AsAP Rocky walitangaza rasmi kuwa wanatarajia mtoto wao wa kwanza pamoja kwa kuachia picha wakiwa matembezini mjini New York zilizomuonesha Riri akiwa mjamzito.

Read More
 NI RASMI SASA RIHANNA ANA UJA UZITO WA MPENZI WAKE ASAP ROCKY

NI RASMI SASA RIHANNA ANA UJA UZITO WA MPENZI WAKE ASAP ROCKY

Ni Rasmi sasa mwanamuziki kutoka nchini marekani Rihanna ni mjamzito. Mwimbaji huyo ambaye pia ni mwanamitindo anatarajia mtoto wake wa kwanza na rapa Asap Rocky. Tovuti mbali mbali za nchini Marekani zimeripoti taarifa hii kufuatia picha ambazo zimewaonesha wawili hao wakiwa matembezini mjini New York wikendi iliyopita. Mwaka 2019 ziliibuka taarifa kama hizi lakini alizikanusha kwenye mahojiano na Jarida la Vogue. ASAP Rocky na Rihanna wamekuwa marafiki wa karibu katika kipindi cha muda mrefu kabla ya kuthibitisha hadharani kuwa wanapendana mwaka wa 2021. Mwaka wa 2013, Rihanna alitokea katika video ya Asap Rocky ya “Fashion Killa” kama video vixen,jambo ambalo lilihusisha uwepo wa mahusiano ya kimapenzi kati yao.

Read More