Mbosso Amtaka Diamond Kuvunja Ukimya Kuhusu Kauli za Baba Levo

Mbosso Amtaka Diamond Kuvunja Ukimya Kuhusu Kauli za Baba Levo

Mwanamuziki Mbosso ameibuka na kuweka wazi msimamo wake kufuatia mvutano unaoendelea mitandaoni kati yake, Diamond Platnumz, na Baba Levo, kuhusu tuhuma za kushirikiana kumchafua kwa jina au kazi zake. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Mbosso amesema kwa uwazi kuwa hana ukaribu wowote na Baba Levo, na hivyo hawezi kushirikiana naye kwa jambo lolote, tofauti na madai yanayoenezwa. Amefafanua kuwa yeye si mtu wa migogoro, na kwamba anamuheshimu Diamond kama kiongozi na kama msanii mkubwa aliyechangia ukuaji wa muziki wake. Hata hivyo, Mbosso amesisitiza kuwa ni wajibu wa Diamond kuzungumza hadharani kumkemea Baba Levo, kwani ukimya wake unaweza kutafsiriwa kama kukubaliana au kuunga mkono vitendo vya matusi na kejeli vinavyotolewa hadharani na Baba Levo. Kauli ya Mbosso imekuja muda mfupi baada ya Baba Levo kumuomba msamaha na Diamond Platinumz akidai kuwa hana ajenda yoyote na Mbosso ya kumchafulia brand yake. “Mzee Lukuga, sina Agenda yoyote na Mbosso na wala siwezi kupanga njama yoyote na Mbosso, nisamehe mzee wangu” Aliandika Instagram. Ikumbukwe jana kulizuka sintofahamu kati ya Mbosso na Baba Levo baada ya Baba Levo kudai kuwa ngoma ya Pawa imetungwa na Diamond Platnumz, ambapo Mbosso alikasirika na kudai huenda WCB inamfanyia figisu wakati aliondoka salama na anaheshimu sana mchango wao kwenye muziki na mara zote amekuwa akiwashukuru.

Read More
 Baba Levo ahaidi kumsaidia Anjella baada ya Harmonize kumkimbia

Baba Levo ahaidi kumsaidia Anjella baada ya Harmonize kumkimbia

Sakata la Harmonize na msanii wake Anjella limemgusa mwanamuziki wa Bongofleva Baba Levo ambaye ameweka wazi atamsaidia msanii huyo matibabu ya mguu wake kwa kumpeleka India na Qatar. Kupitia ukurasa wake instagram Baba Levo amesema “Dada Anjella Naitwa Baba Levo NAKUHAKIKISHIA UTAENDA QATAR NA UTAENDA INDIA PIA KWA AJILI YA MATIBABU …!! KIRANDAGE PAMOJA NA BANGE ZAKE ILA AMEKUTOA MBALI SEMA TU AMEISHIWA HELA KWA SASA NA HII NI KWASABABU YA KUTAKA KUSHINDANA NA DIAMOND PLATINUMZ AMEJIKUTA AMEFILISIKA KABISA…!” Ikumbukwe, jana Harmonize kupitia insta story yake aliweka ujumbe akitaka mtu yeyote anaeweza kuendeleza kipaji cha Anjella asisite kujitokeza kwa ajili ya kumsaidia msanii huyo. Hata hivyo, kwenye ujumbe huo boss huyo wa Konde Gang hakuweka wazi kama lebo yake ndio imeachana rasmi na Anjella.

Read More
 LINEX AMCHANA BABA LEVO KWA MADAI YA KUMZUNGUMZIA VIBAYA

LINEX AMCHANA BABA LEVO KWA MADAI YA KUMZUNGUMZIA VIBAYA

Mwanamuziki wa Bongofleva Linex mjeda ameamua kumtolea uvivu baba levo baada ya msanii huyo kuendelea kuongelea maisha yake mara kwa mara kwenye vyombo vya habari Kupitia ukurasa wake wa Instagram Linex amemchana Baba Levo kuwa aache kuongelea maisha yake kwenye redio kwani jambo hilo linamkosesha amani huku akimuomba baba levo msamaha kama amewahi kumkosoa. Linex na Baba Levo ni marafiki wa miaka mingi na Baba Levo ameshawahi kukiri mara nyingi kuwa Linex ni kati ya watu ambao walimsaidia miaka ya hapo nyuma akiwa Dareesalaam akijaribu kuupambania kipaji chake cha muziki. Hata hivyo Baba Levo amekuwa akifunguka matukio na tabia za Linex ambazo walikuwa wanazipitia miaka ya nyuma. Lakini pia amekuwa akilitaja jina la Linex kwenye mifano mbalimbali afanyapo mahojiano na vyombo vya habari jambo ambalo limemfanya Linex kukwazika

Read More