Baba Levo ahaidi kumsaidia Anjella baada ya Harmonize kumkimbia

Baba Levo ahaidi kumsaidia Anjella baada ya Harmonize kumkimbia

Sakata la Harmonize na msanii wake Anjella limemgusa mwanamuziki wa Bongofleva Baba Levo ambaye ameweka wazi atamsaidia msanii huyo matibabu ya mguu wake kwa kumpeleka India na Qatar. Kupitia ukurasa wake instagram Baba Levo amesema “Dada Anjella Naitwa Baba Levo NAKUHAKIKISHIA UTAENDA QATAR NA UTAENDA INDIA PIA KWA AJILI YA MATIBABU …!! KIRANDAGE PAMOJA NA BANGE ZAKE ILA AMEKUTOA MBALI SEMA TU AMEISHIWA HELA KWA SASA NA HII NI KWASABABU YA KUTAKA KUSHINDANA NA DIAMOND PLATINUMZ AMEJIKUTA AMEFILISIKA KABISA…!” Ikumbukwe, jana Harmonize kupitia insta story yake aliweka ujumbe akitaka mtu yeyote anaeweza kuendeleza kipaji cha Anjella asisite kujitokeza kwa ajili ya kumsaidia msanii huyo. Hata hivyo, kwenye ujumbe huo boss huyo wa Konde Gang hakuweka wazi kama lebo yake ndio imeachana rasmi na Anjella.

Read More
 LINEX AMCHANA BABA LEVO KWA MADAI YA KUMZUNGUMZIA VIBAYA

LINEX AMCHANA BABA LEVO KWA MADAI YA KUMZUNGUMZIA VIBAYA

Mwanamuziki wa Bongofleva Linex mjeda ameamua kumtolea uvivu baba levo baada ya msanii huyo kuendelea kuongelea maisha yake mara kwa mara kwenye vyombo vya habari Kupitia ukurasa wake wa Instagram Linex amemchana Baba Levo kuwa aache kuongelea maisha yake kwenye redio kwani jambo hilo linamkosesha amani huku akimuomba baba levo msamaha kama amewahi kumkosoa. Linex na Baba Levo ni marafiki wa miaka mingi na Baba Levo ameshawahi kukiri mara nyingi kuwa Linex ni kati ya watu ambao walimsaidia miaka ya hapo nyuma akiwa Dareesalaam akijaribu kuupambania kipaji chake cha muziki. Hata hivyo Baba Levo amekuwa akifunguka matukio na tabia za Linex ambazo walikuwa wanazipitia miaka ya nyuma. Lakini pia amekuwa akilitaja jina la Linex kwenye mifano mbalimbali afanyapo mahojiano na vyombo vya habari jambo ambalo limemfanya Linex kukwazika

Read More