BEKA FLAVOUR AACHIA RASMI ALBUM YAKE MPYA

BEKA FLAVOUR AACHIA RASMI ALBUM YAKE MPYA

Msanii wa Bongofleva Beka Flavour ameachia rasmi Album yake mpya inayokwenda kwa jina la First Born. Album hiyo ambayo inapatikana exclusive kupitia Boomplay ina jumla ya ngoma 15 ya moto huku ikiwa na kolabo 7 pekee. Beka flavour amewashirikisha wakali kama Barnaba, Christian Bella, Naiboi, Linah, Young Lunya, na Yamoto Band huku Album yenyewe ikiwa na nyimbo kama Wivu, Medula, Dunia Tunapita na nyingine nyingi. First Born ni album ya kwanza kwa mtu mzima Beka flavour kuitoa tangu aanze safari yake ya muziki.

Read More
 BEKA FLAVOUR AACHIA RASMI TRACKLIST YA ALBUM YAKE MPYA

BEKA FLAVOUR AACHIA RASMI TRACKLIST YA ALBUM YAKE MPYA

Msanii wa Bongofleva Beka Flavour ameanika hadharani tracklist ya Album yake mpya inayokwenda kwa jina la First Born. Kupitia Instagram yake msanii huyo amechapisha Artwork ya Album hiyo ambayo ina jumla ya ngoma 15 ya moto huku ikiwa na kolabo 7 pekee. Beka flavour amewashirikisha wakali kama Barnaba, Christian Bella, Naiboi, Linah, Young Lunya, na Yamoto Band huku Album yenyewe ikiwa na nyimbo kama Wivu, Medula, Dunia Tunapita na nyingine nyingi. Hata hivyo hajataja tarehe rasmi ya kuiachia album hiyo zaidi ya kuwataka mashabiki kuendelea kusalia kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii kwa taarifa zaidi. First Born ni album ya kwanza kwa mtu mzima Beka flavour kuitoa tangu aanze safari yake ya muziki.

Read More
 BEKA FLAVOUR ATHIBITISHA KUFUTWA KWA VIDEO ZA NYIMBO ZAKE YOUTUBE

BEKA FLAVOUR ATHIBITISHA KUFUTWA KWA VIDEO ZA NYIMBO ZAKE YOUTUBE

Mwanamuziki wa Bongofleva, Beka Flavour amedai kuwa video mbili za nyimbo zake,  Libebe na Sikinai zimefutwa katika chaneli yake ya YouTube. Beka  flavour amesema hata alipowasiliana na YouTube amejibiwa kuwa video hizo zimefutwa na mtu ambaye wanafanya naye kazi. Hitmaker huyo wa “In Love” amewatoa hofu mashabiki zake kwa kusema kuwa timu yake inajaribu kila wawezalo kuhakikisha video za nyimbo zinarejea youtube ila hana uhakika kama zitarejeshwa kwenye mtandao huo. “Kwa hiyo hatujajua ni nani ambaye amezifuta video hizo, tunaendelea kupambana ziweze kurudi japo sina uhakika kama zitarudi,” amesema Beka. Utakumbuka Beka Flavour alikuwa miongoni mwa wasanii wanne waliokuwa wanaunda kundi la Yamoto Band, akiwemo Aslay, Mbosso na Enock Bella.

Read More
 BEKA FLAVOUR: SIENDEKEZI UTIMU KWENYE MUZIKI WANGU

BEKA FLAVOUR: SIENDEKEZI UTIMU KWENYE MUZIKI WANGU

Mwanamuziki wa Bongofleva, Beka Flavour amedai haweza kujihushisha na timu yoyote katika muziki huo ili kunufaika na mashabiki wa timu fulani kwani yeye anatengenezea kazi nzuri ambazo anajua zinaweza kupendwa na wote. Beka Flavour amesema anafanya muziki mzuri kwa ajili ya mashabiki wake ambao wapo naye kwa ajili ya ubora wa kazi zao na sio timu ambazo kamwe hawezi kujiunga nazo. Kwa miaka ya hivi karibuni wasanii Alikiba na Diamond Platnumz wamekuwa ni washindani wakubwa ambao wametengeneza timu ambazo hadi baadhi ya wasanii wengine wamejiunga nazo. Ikumbukwe Beka Flavour alikuwa ni miongoni mwa wasanii waliokuzwa na kituo cha Mkubwa na Wanawe chake Mkubwa Fella, na chini ya kundi la Yamoto Band ambalo lilikuwa linaundwa na wasanii Aslay, Enock Bellla na  Mbosso ambaye alichukuliwa na lebo ya WCB Wasafi yake Diamond.

Read More