Ben Githae Aomba Msamaha kwa Gen Z: “Ninajifunza, Naomba Radhi”

Ben Githae Aomba Msamaha kwa Gen Z: “Ninajifunza, Naomba Radhi”

Mwanamuziki mashuhuri wa nyimbo za injili na kisiasa, Ben Githae, ameomba msamaha kwa kizazi kipya cha vijana wa Kenya maarufu kama Gen Z baada ya kulengwa vikali mitandaoni kutokana na misimamo yake ya awali ya kisiasa, hasa wakati wa kampeni za “Tano Tena”. Kupitia mahojiano na kituo kimoja cha redioni nchini, Githae alikiri kwamba wakati mwingine sauti yake ilitumiwa kuunga mkono maamuzi ambayo baadaye yalileta madhara kwa wananchi, hasa vijana.  “Najua kuna vijana wengi walioumizwa, waliopoteza matumaini, na waliokatishwa tamaa na siasa ambazo niliwahi kuziunga mkono. Sikuwa na nia mbaya. Nilifanya kile nilichofikiri ni sahihi kwa wakati ule. Lakini leo najifunza kutoka kwa kizazi hiki chenye ujasiri, na kwa kweli naomba msamaha,” alisema Githae. Githae alisifu juhudi za Gen Z katika kupaza sauti zao dhidi ya ukosefu wa haki na changamoto za kiuchumi, akisema kuwa kwa mara ya kwanza, anaona mabadiliko yanayochochewa na vijana bila woga. “Ninawaunga mkono. Nimeona nguvu yenu, ujasiri wenu, na dhamira yenu ya kuleta mabadiliko ya kweli. Nawaheshimu sana, na nitakuwa mmoja wa wanaowaunga mkono katika mapambano haya ya kudai haki na uwajibikaji,” aliongeza. Msamaha wa Ben Githae unakuja wakati ambapo Gen Z wamechukua nafasi kubwa katika maandamano ya kidijitali na ya mitaani wakipinga sera za kiuchumi, ushuru wa juu, na ukosefu wa nafasi za kazi. Wengi wameipokea kauli hiyo kama hatua nzuri ya kuwajibika, ingawa wengine bado wanamkumbusha kuwa samahani pekee haitoshi, bali matendo yanahitajika. Kwa sasa, Githae ameahidi kutumia sauti yake kubeba ajenda za vijana, kuelimisha jamii, na kushirikiana na kizazi hiki ili kuleta mabadiliko ya kweli.

Read More
 Ben Githae akerwa na wanaomkejeli baada ya mrengo wa Azimio la Umoja kupoteza uchaguzi

Ben Githae akerwa na wanaomkejeli baada ya mrengo wa Azimio la Umoja kupoteza uchaguzi

Mwimbaji wa nyimbo za injili nchini Ben Githae ameonekana kuchukizwa na kitendo cha mashabiki kuendelea kumkejeli hata baada ya mrengo wa azimio la umoja kupoteza uchaguzi mkuu uliokamilika. Akizungumza kwenye hafla ya kuchangisha pesa huko Mlima Kenya, Githae amekiri kuumizwa sana na kauli ya watu wanaokumbusha kila mara namna mrengo aliokuwa anaunga mkono wa Azimio la umoja ulivyopoteza uchaguzi wa Agosti 9 huku akiwataka marafiki zake kumkubali kama mmoja wao badala ya kumsema vibaya kwa misingi ya kisiasa. Hitmaker huyo wa “Mabataro” amesema kwa sasa ameshakubali matukio kuwa muungano wa Azimio la umoja ulipoteza uchaguzi huku akisisitiza kuwa hana budi kukumbatia serikali ya Kenya Kwanza inayoongozwa na Rais William Ruto. Miezi mitano iliyopita Ben Githae alikuwa gumzo nchini baada ya kuachia wimbo wa kisiasa uitwao “Kenya Is Safe”, wimbo ambao alikuwa anamsifia Raila Odinga kwa hatua ya kumchagua Martha Karua kama mgombea mwenza wa Azimio kwenye uchaguzi wa Agosti 9 ambapo alienda mbali zaidi na kusema kuwa Kenya ipo salama mikononi mwa Odinga na Karua.

Read More