Ben Pol aomba msamaha EX wake Arnelisa kwa kumzungumzia vibaya

Ben Pol aomba msamaha EX wake Arnelisa kwa kumzungumzia vibaya

Msanii wa Bongo Fleva Ben Pol ameandika barua ya wazi kumuomba msamaha aliyekuwa wake Anerlisa kutoka nchini Kenya kwa kile alichozungumza. Akifanyiwa mahojiano na mtangazaji Millardayo Ben Pol alieleza kuwa hakuwahi kufurahia ndoa yake na Anerlisa. Baada ya mahojiano hayo Anerlisa alimuomba Ben Pol aache kumzungumzia na akaahidi endapo ataendelea basi atapost meseji zake kwani anqchoongea kwenye media ni tofauti na anachomtumia. Sasa  kupitia ukurasa wake wa Instagram ameeleza kuwa lengo lake lilikuwa kueleza namna alivyopitia magumu na kuathirika kisaikolojia hakuwa na lengo na kumuumiza aliyekuwa mke wake Arnelisa. Ben Pol amechukua hatua hiyo mara baada ya Arnelisa kuanika hadharani meseji ambazo msanii huyo alikuwa akimtumia kupitia WhatsApp akitaka warudiane.

Read More
 Arnelisa aanika hadharani meseji za Ben Pol

Arnelisa aanika hadharani meseji za Ben Pol

Mwanadada mjasiriamali kutoka nchini Kenya, Anerlisa ameamua kuweka wazi mapungufu ya Ben Pol, ameachia meseji za msanii huyo wa Bongofleva ambazo alikuwa akimtumia kupitia WhatsApp tangu mwishoni mwa mwaka jana. Jumbe hizo ambazo zimeanikwa hadharani na mtandao wa Mpasho, zinaonesha Ben Pol akimkumbusha Anerlisa matukio ya maisha yao na kumueleza hisia zake, akitaka warudiane. Sakata hili lilianza baada ya Ben Pol kufanya mahojiano na mtangazaji Millard Ayo, ambapo alikaririwa akisema hakuwahi kufurahia ndoa yao na ilikuwa ya mapicha picha tu. Ni madai ambayo yalikanushwa vikali na Anerlisa ambaye alitumia insta story kumuonya Ben Pol asiongelee masuala ya mahusiano yao mitandaoni, vinginevyo atamuanika.

Read More
 Anerlisa ampa onyo Ben Pol ataka aache kumuongelea

Anerlisa ampa onyo Ben Pol ataka aache kumuongelea

Mrembo kutoka Kenya Anerlisa ambaye alikuwa mke wa msanii wa Bongofleva Ben Pol ameonyesha kutofurahishwa na kile ambacho alikizungumza Ben Pol kwenye mahojiano yake na Ayo Tv kuwa hajawahi kufurahishwa na ndoa yake na mrembo huyo. Kupitia InstaStory yake  anashangaa ni kwanini Ben Pol kila siku amekuwa akiongea mambo mengi ili aonekane mbaya mbele ya umma. “Ben naona umenizoea na unachukulia ukimya wangu kama udhaifu wangu. Ulikuwa na uwezo wa kumwambia anaekuhoji asikuulize kuhusu mimi. Kwa nini unapenda kila mara mimi nionekane mbaya. Chini ya kapeti unanitumia jumbe tofauti tofauti na namna unavyoniongelea”, Aliandika. Lakini pia amemtaka Ben Pol aache kumuongelea kwani yeye pia ana mengi kumuhusu lakini amechagua kukaa kimya kama mwanamke. “Kama kweli wewe ni mwanaume, nakuomba uweke wazi jumbe zote ulizokuwa unanitumia tangu Desemba 25 hadi Januari 4, 2023. Nina mengi ya kuzungumza kuhusu wewe au kuonyesha, lakini nimechagua kusimama kama Mwanamke.” , Aliandika.

Read More
 Ben Pol akanusha kukamilika kwa talaka yake na Arnelisa Muiga

Ben Pol akanusha kukamilika kwa talaka yake na Arnelisa Muiga

Mwimbaji wa Bongofleva, Ben Pol amejitokeza na kusema kuwa hajapata taarifa yoyote kuhusu kukamilika kwa talaka na aliyekuwa mke wake, Anerlisa. Wiki iliyopita Anerlisa ambaye ni binti wa seneta wa Nakuru Tabitha Karanja alitangaza kuwa mchakato wa talaka yake na Ben Pol umekamilika. “Mimi pia naona ripoti hizi mtandaoni. Sijafahamishwa rasmi au kwa njia isiyo rasmi. Sijui hayo mawasiliano aliyapata wapi maana hata mahakama niliyofungua kesi ya talaka haifahamu taarifa hizo,” Ben Pol aliambia Nation. Utakumbuka wawili hao walifunga ndoa Mei 2020 katika Kanisa Katoliki la St Gaspar huko Mbezi Beach, Tanzania.

Read More
 Arnelisa yupo uhuru, Akamilisha talaka yake na Mwanamuziki Ben Pol

Arnelisa yupo uhuru, Akamilisha talaka yake na Mwanamuziki Ben Pol

Ni rasmi kuwa mfanyabiashara wa Kenya Anerlisa Muigai na mwanamuziki kutoka Tanzania Ben Pol sio mke na mume tena. Anerlisa ambaye ni binti wa seneta wa Nakuru Tabitha Karanja kupitia ukurasa wake wa Instagram, amefichua kuwa talaka yake na mwimbaji huyo wa Bongofleva hatimaye imekamilika. Mrembo huyo amewashukuru mawakili wake kwa kuhakikisha kuwa mchakato wa talaka yake umekamilika “Niko huru rasmi. Haitakuwa sawa kutowatambua mawakili hawa wawili ambao walifanya kazi bila kuchoka kuhakikisha kwamba talaka inafanywa haraka na sio kusubiri kwa miaka. Hamza Jabir na Hosea Chamba, asanteni kwa kazi zenu na kwa kufanya kila kitu mlivyoombwa.” alisema kwenye Insta stori. Anerlisa na Ben Pol walifunga ndoa Mei mwaka 2020 lakini wakatengana mwaka jana ambapo Ben Pol aliwasilisha kesi ya talaka mahakamani.

Read More
 ARNELISA MUIGAI KWENYE PENZI JIPYA BAADA YA NDOA YAKE NA BEN POL KUINGIWA NA UKUNGU

ARNELISA MUIGAI KWENYE PENZI JIPYA BAADA YA NDOA YAKE NA BEN POL KUINGIWA NA UKUNGU

Huenda Ex wa msanii wa Bongofleva Ben Pol Arnelisa Muigai yupo kwenye Penzi jipya baada ya kudokeza Kuhusu hilo kupitia ukurasa wake wa Instagram. CEO huyo wa Life still water na mrithi wa shamba la Keroche Arnelisa Muigai amedokeza hilo kwa kupost kwenye insta story yake emoj ya kopa kama ishara ya mapenzi, ikiwa ni miezi kadhaa tu baada ya kuvunjika kwa ndoa yake/ na kupeana talaka na aliyekua mumewe Ben Pol. Aidha Mkurugenzi Mtendaji huyo aliingia kwenye headlines mapema wiki hii wakati wa kusherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kuonekana na mtu aliefanana na Ben Pol kwenye video ambayo ilisambaa mitandaoni akiwa amekaa kimahaba na mtu huyo ambae hajamuweka wazi kama ndie mpenzi wake wa sasa.

Read More