Wezi Wapora Hard Drives Zenye Kazi Muhimu za Beyonce Jijini Atlanta

Wezi Wapora Hard Drives Zenye Kazi Muhimu za Beyonce Jijini Atlanta

Kabla ya maonyesho ya msanii nyota duniani Beyonce yaliyofanyika jijini Atlanta, ripoti zinasema kuwa wezi walivunja magari ya baadhi ya watu wa karibu na msanii huyo na kuiba vifaa muhimu vya kazi. Kwa mujibu wa vyanzo vya karibu na timu ya Beyonce, tukio hilo lilitokea Julai 8 ambapo gari la choreographer na dancer mmoja lilivunjwa na hard drives kadhaa kuibwa. Inadaiwa kuwa vifaa hivyo vilikuwa na kazi ambazo bado hazijatolewa kwa umma, zikiwemo nyimbo mpya, video, mipango ya maonesho ya siku zijazo na nyaraka zingine za kipekee. Hadi sasa, hakuna taarifa rasmi ya kupatikana kwa hard drives hizo, lakini uchunguzi wa kina umeanzishwa na mamlaka za usalama wa mji wa Atlanta ili kuwabaini wahusika na kurejesha mali iliyoibiwa. Tukio hili limeibua wasiwasi miongoni mwa mashabiki kuhusu usalama wa kazi za wasanii na athari zinazoweza kutokea endapo maudhui hayo yatavujishwa mitandaoni bila idhini.

Read More
 Jeezy Adai Jay Z Alimtoa Kwenye Wimbo wa Beyoncé

Jeezy Adai Jay Z Alimtoa Kwenye Wimbo wa Beyoncé

Rapa kutoka Marekani, Jeezy, amefunguka kuhusu tukio lililomkuta nyuma ya pazia la utengenezaji wa wimbo maarufu wa Beyoncé “Drunk In Love”. Jeezy ameeleza kuwa awali alikuwa sehemu ya mradi huo, tayari akiwa ameandika verse yake kwa ajili ya kushiriki kwenye wimbo huo, lakini mambo yalibadilika ghafla. Kwa mujibu wa Jeezy, baada ya maandalizi ya awali kukamilika, alipokea taarifa kutoka kwa Jay Z akielezwa kuwa hatakuwa tena kwenye wimbo huo, na kwamba Jay Z mwenyewe ndiye atakayeshirikiana na Beyoncé kwenye ngoma hiyo. Kauli hiyo imeibua mjadala mkubwa mtandaoni huku mashabiki na wachambuzi wa muziki wakigawanyika. Wapo wanaodai huenda verse ya Jeezy haikuwa na mvuto wa kutosha, jambo lililomfanya Jay Z kuchukua nafasi hiyo. Hata hivyo, wengine wanaamini verse ya Jeezy ilikuwa kali kupita kiasi, hali iliyoweza kumfanya Jay Z kuhofia Jeezy angefika mbali zaidi kupitia wimbo huo. Aidha, baadhi ya wapenzi wa muziki wameenda mbali zaidi kwa kusema kuwa verse ya Jay Z kwenye Drunk In Love haikuwa kali sana, na huenda ingekuwa busara zaidi kumuacha Jeezy ashiriki.

Read More
 Vurugu za Mashabiki Zazua Taharuki Katika Show ya Beyoncé Jijini Chicago

Vurugu za Mashabiki Zazua Taharuki Katika Show ya Beyoncé Jijini Chicago

Tamasha la muziki lililojaa hamasa kubwa kutoka kwa malkia wa pop Beyoncé liligeuka kuwa eneo la sintofahamu baada ya mashabiki wake wawili kuingia katika ugomvi mkali karibu kabisa na jukwaa. Tukio hilo lilinaswa kwenye video na kusambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii, likizua mijadala miongoni mwa mashabiki na wapenzi wa muziki. Katika video hiyo, ambayo sasa imevutia maelfu ya watazamaji, wanawake wawili wanaonekana wakitupiana maneno makali kabla ya kushikana mashati na kuanza kurushiana makonde yote hayo yakifanyika zikiwa ni mita chache kutoka mahali Beyoncé alikuwa akitumbuiza. Walinzi wa usalama walionekana wakijaribu kuingilia kati haraka, huku baadhi ya mashabiki wakisikitika kwa hali hiyo kuvuruga uzuri wa onyesho hilo. Mashabiki wengine waliokuwepo eneo hilo walisema mzozo huo huenda ulitokana na msongamano mkubwa karibu na jukwaa, ambapo kila mtu alikuwa akijaribu kupata nafasi nzuri ya kumwona Beyoncé kwa ukaribu zaidi. Watu wengi wamesikitishwa na tukio hilo, wakisema kuwa Beyoncé amekuwa mstari wa mbele katika kuhubiri upendo na umoja katika kazi zake za sanaa, hivyo haifai mashabiki wake kutenda kinyume na misingi hiyo. Hadi sasa, Beyoncé mwenyewe pamoja na timu yake ya usimamizi hawajatoa tamko rasmi kuhusiana na tukio hilo. Hata hivyo, vyombo vya usalama vya mji wa Chicago vimesema kuwa uchunguzi unaendelea na huenda hatua za kisheria zikachukuliwa kwa wahusika, hasa ikiwa walivunja sheria za usalama wa umma. Tamasha hilo lilikuwa sehemu ya ziara ya kimataifa ya Beyoncé ya CowBoy Carter na lilihudhuriwa na maelfu ya mashabiki waliokuwa na matarajio makubwa ya kupata burudani ya kiwango cha juu  ambayo licha ya tukio hilo dogo, bado ilifanyika kwa mafanikio makubwa.

Read More
 BEYONCE ARIDHIA OMBI LA KUONDOA NENO “SP*Z”  KWENYE WIMBO WAKE “HEATED”

BEYONCE ARIDHIA OMBI LA KUONDOA NENO “SP*Z” KWENYE WIMBO WAKE “HEATED”

Hatimaye Beyonce amekubali kuondoa neno ambalo ni kero kwa walemavu kutoka katika wimbo wake uitwao “Heated” ulio kwenye album yake mpya iitwayo “Renaissance” wimbo ambao uliandikwa na rappa Drake na wengine. Msemaji wa Beyoncé ambaye alitoa taarifa kwa vyombo vya habari, amesema kwamba neno hilo halikutumika makusudi ili kuwakejeli walemavu na litaondolewa. Neno hilo ni “SP*Z” ufupisho wa “Spastic” ambalo maana yake ni mtu ambaye amepoteza uwezo wa kutumia vyema viungo vya mwili au hata akili na ni aina ya ugonjwa wa kupooza ubongo yaani Cerebral Palsy. Utakumbuka, hili linajiri kwa Beyonce kufuatia mwezi mmoja kupita, mwanamuziki mwingine aitwae Lizzo nae kubadili neno hilo hilo ambapo alilitumia kwenye wimbo wake uitwao Grrrls. Hannah Diviney, mmoja wa watetezi wa walemavu nchini Marekani, ameandika kwenye ukurasa wake wa Twitter kwamba; kusikia matumizi ya neno hilo tena na Beyonce, ni kama kofi usoni mwake na kwenye nyuso za walemavu na hatua walizopiga na Lizzo.

Read More
 WANAHARAKATI MAREKANI WAZIDI KUMSHINIKIZA BEYONCE KUOMBA MSAMAHA

WANAHARAKATI MAREKANI WAZIDI KUMSHINIKIZA BEYONCE KUOMBA MSAMAHA

Mwanamuziki kuoka Marekani Beyonce amejikuta kwenye kiti cha moto kufuatia kutumia neno “Spazzin” kwenye wimbo wake Heated unaopatikana kwenye album yake Renaissance aliyoiachia hivi karibuni Baadhi ya wanaharakati kwenye mitandao ya kijamii wamehoji juu ya mwimbaji huyo kutumia neno hilo ambalo hutumika kuwadhihaki watu wenye ulemavu wa akili. Kufuatia tuhuma hizo Beyonce ameahidi kufuta maneno hayo kwenye wimbo huo japo hajaomba radhi mpaka sasa. Si Beyonce tu aliyewahi kusakamwa kwa kutumia neno hilo ila hata mwimbaji Lizzo alilazimika kubadili mstari kwenye wimbo wake  Grrls baada ya kutumia neno hilo Pamoja na ahadi hiyo ya kubadili maneno hayo kwenye wimbo wake wanaharakati wanataka Beyonce aombe radhi kwa uma kama alivyofanya Lizzo.

Read More
 BEYONCE ATEULIWA KUWANIA TUZO ZA EMMY

BEYONCE ATEULIWA KUWANIA TUZO ZA EMMY

Mwanamuziki nyota kutoka Marekani, Beyonce, ameteuliwa kuwania tuzo ya Emmy kwa vipindi vinavyoonyeshwa mchana yaani ‘Daytime Emmy’ kutokana na wimbo wa kutambulisha kipindi cha mama yake cha Facebook kiitwacho “Talks with Mama Tina” Beyonce aliwaongoza wanawe Blue Ivy, Sir na Rumi katika kuimba wimbo huo jambo ambalo lilimgusa sana Bi. Tina Knowles-Lawson. Kipindi chake ni cha mazungumzo na wageni mbalimbali ambao huwa anawakaribisha na chakula. Uteuzi wa Beyonce kuwania tuzo ya vipindi vya mchana kupitia wimbo huo wa kipindi cha mama yake ndio wa kwanza chini ya kitengo cha vipindi ambavyo huonyeshwa mchana lakini amewahi kuteuliwa mara nane kuwania tuzo ya Emmy kwa vipindi vinavyoonyeshwa usiku. Kipindi cha Mama Beyonce kilianza rasmi Disemba mwaka jana na hadi kufikia sasa tayari amehoji wageni kadhaa wakiwemo Kelly Rowland, Zendaya, Chloe na Halle Bailey, Tiffany Haddish, Kevin Hart na Ciara.

Read More
 BEYONCE KUTUMBUIZA KWENYE TUZO ZA OSCAR JUMAPILI HII

BEYONCE KUTUMBUIZA KWENYE TUZO ZA OSCAR JUMAPILI HII

Mwanamuziki maarufu duniani Beyonce ametajwa kutumbuiza kwenye tuzo za 94 za Oscar zitakazofanyika, Machi 27 katika ukumbi wa Dolby Thearter,nchini Marekani. Beyonce anatajwa kutumbuiza wimbo “Be alive” ambao unapatikana kwenye filamu ya King Richard. Wasanii wengine ambao wanatarajiwa kuwasha moto kwenye jukwaa hilo ni pamoja Van Morrison wimbo “Down to joy”, ambao unatikana kwenye filamu ya Belfast, wengine ni Billie Eilish & Finneas ambao watatumbuiza wimbo “No time to die” unayopatikana kwenye filamu ya No time to die, na wasanii wengine wengi. Tuzo hizo maarufu za filamu duniani, zitahudhuriwa na mastaa kibao kutoka Marekani na nje ya Marekani. Tuzo hizo zina jumla ya vipengele 24 ambazo wasanii mbalimbali wakiwemo wa muziki na filamu wanaziwania. Wakati huo huo Regina Hall, Amy Schumer na Wanda Sykes wanatarajiwa kuwa host wa tuzo hizo. Hii inakuwa kwa mara ya pili tangu mwaka 2011 tuzo hizo kuwa na host watatu.

Read More
 BEYONCE APATA NOMINATION YAKE YA KWANZA KWENYE TUZO ZA OSCAR 2022

BEYONCE APATA NOMINATION YAKE YA KWANZA KWENYE TUZO ZA OSCAR 2022

Vipengele vya Tuzo za Oscar vimetolewa Februari 8, mwaka wa 2022 ambapo dunia imemshuhudia staa wa muziki kutoka nchini marekani Beyonce akipata Nomination yake ya kwanza kupitia kipengele cha Best Original Song na wimbo wa “Be Alive”. Wimbo huo ulitumika kwenye filamu ya “King Richard”,  filamu fupi iliyogusa maisha ya Baba mzazi wa Serena na Venus Williams. Tuzo hizo za 94 zimetajwa kufanyika March 27, mwaka wa 2022 katika ukumbi wa Dolby Theatre nchini Marekani

Read More