BIEN WA SAUTI SOL ATAKA WIZARA YA UTAMADUNI KUBUNIWA NCHINI KENYA

BIEN WA SAUTI SOL ATAKA WIZARA YA UTAMADUNI KUBUNIWA NCHINI KENYA

Msanii wa Sauti Sol, Bien amependekeza kubuniwa kwa wizara ya masuala ya utamaduni kwa kile alichokitaja kuwa ni nyanja iliyotengwa kwa muda mrefu nchini. Kupitia instastory yake kwenye mtandao wa Instagram Bien amesema hatua ya Kenya kuunganisha michezo na utamaduni huku ikizidi kuipa kipau mbele sekta ya michezo haina mashiko kwa kuwa ni nyanja mbili tofauti ambazo zinapaswa kupewa uzito kwa usawa. Hitmaker huyo wa “Inauma” ametaka serikali kuweka nguvu zaidi kwenye masuala ya utamaduni kama inavyofanya kwa sekta ya michezo kwani mataifa yote yanayoendelea duniani yana wizara ya utamaduni. Kauli ya Bien imekuja mara baada ya Rais wa Kenya William Ruto kutaja baraza lake la mawaziri

Read More
 BIEN WA SAUTI SOL ATANGAZA KUWEKEZA ZAIDI KWENYE ISHU YA KUFANYA KOLABO NA WASANII WENGINE KAMA MSANII UHURU

BIEN WA SAUTI SOL ATANGAZA KUWEKEZA ZAIDI KWENYE ISHU YA KUFANYA KOLABO NA WASANII WENGINE KAMA MSANII UHURU

Msanii wa Sauti Sol, Bien amefunguka na kudai kwamba mwaka huu atajikita zaidi kwenye suala la kufanya kolabo na kuwashirikisha wasanii wengine kwenye kazi zake atakazo achia. Katika mahojiano na mpasho Bien amesema kuwa amepokea maombi nyingi za wasanii wanaotaka kufanya naye kazi huku akidokeza ujio wa album mpya ya kundi la Sauti Sol ambayo itaingia sokoni mwezi Aprili mwaka wa 2022. Kauli ya Bien inakuja wakati kundi la Sauti Sol linajianda kufanya ziara yao ya kimuziki  Barani Ulaya kuanzia Aprili Mosi, mwaka huu huko Barcelona nchini Uhispania na itafanyika ndani ya miji 19 kwa kipindi cha mwezi mmoja.. Ziara hiyo inatarajiwa kuzunguka kwenye miji mbalimbali nchini Ujerumani, Ureno, Ufaransa, Denmark, Uingereza, Belgium ambapo kilele chake kitakuwa nchini Uholanzi Juni 28 mwaka wa 2022.

Read More