Bien Aikosoa Vikali Hatua ya NACADA Kupiga Marufuku Wasanii Kutangaza Pombe

Bien Aikosoa Vikali Hatua ya NACADA Kupiga Marufuku Wasanii Kutangaza Pombe

Msanii nyota wa Kenya na mwanachama wa kundi la Sauti Sol, Bien-Aimé Baraza, ameikosoa vikali Mamlaka ya Kitaifa ya Kudhibiti Matumizi ya Pombe na Dawa za Kulevya (NACADA) kwa pendekezo la kuzuia watu mashuhuri kushiriki kwenye matangazo ya bidhaa za pombe. Kupitia ujumbe mzito alioutuma kwenye ukurasa wake wa Instagram, Bien amesema hatua hiyo ni ya kinafiki na inadhuru moja kwa moja sekta ya sanaa, ubunifu na maudhui, inayotegemewa na maelfu ya vijana kwa ajira. “Hii ni unafiki. Mnajifanya kuwajali vijana huku mnaua ndoto zao. Mnashangaa kwa nini ukosefu wa ajira ni mkubwa? Mnaua kila nafasi tunayopata,” aliandika Bien. Bien amesisitiza kuwa badala ya kuweka marufuku inayowakandamiza vijana, serikali inapaswa kuja na sera bora zinazolinda afya ya umma bila kuathiri vipato vya watu wanaotegemea sekta hizo.  “Je, sisi ndio nchi ya kwanza kuwa na matatizo kama haya? Mbona tuendelee kujifanya watakatifu kuliko wengine wakati hatutoi suluhisho mbadala?” aliongeza Bien kwa ukali. Kauli yake imezua mjadala mitandaoni, wengi wakimtetea na kuitaka serikali kuweka sera zenye kuzingatia uhalisia wa kiuchumi.

Read More
 Bien Akutana na Burna Boy BBC Studios, Adokeza Wimbo Mpya

Bien Akutana na Burna Boy BBC Studios, Adokeza Wimbo Mpya

Msanii nguli wa Afro-pop kutoka Kenya, Bien-Aimé Baraza, ameonekana akiendelea kupanda ngazi za kimataifa baada ya kukutana na msanii mashuhuri wa Nigeria, Burna Boy, katika studio za BBC Radio 1 mjini London. Mkutano huo, ambao umevutia maelfu ya mashabiki mtandaoni, unazua tetesi za uwezekano wa ushirikiano wa kisanii kati ya wawili hao. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Bien alipakia video akiwa kwenye studio pamoja na mchekeshaji wa Kimataifa, Edie Kadi, huku akidokeza ujio wa wimbo mpya. “Onwards and upwards! Had a good time with @comediekadi at @bbcradio1. New single loading… stay tuned. 🔥🎶 Get your tickets for Hamburg, O2, and Kenya tour. Link in bio! Don’t suffer like your enemies,” Bien aliandika kwenye Instagram yake baada ya mkutano huo. Kauli hiyo imeibua msisimko mkubwa, hasa ikizingatiwa kuwa mkutano wake na Burna Boy umetokea muda mfupi kabla ya ujumbe huo. Ingawa Bien hakutaja moja kwa moja kuhusu ushirikiano na Burna Boy, mashabiki wameanza kuunganisha nukta na kutarajia collabo ya kimataifa inayoweza kutikisa muziki wa Afrika. Bien, ambaye kwa sasa anazunguka Ulaya kwa ajili ya ziara na mahojiano, ameendelea kujijenga kama msanii wa kujitegemea tangu kundi la Sauti Sol lipumzike kwa muda. Kwa upande mwingine, Burna Boy anaendelea kutamba duniani na amekuwa mstari wa mbele kuipeperusha bendera ya Afrobeats kwenye majukwaa ya kimataifa.

Read More
 Bien wa Sauti Sol Aibuka na Kuku Hai Katika Show ya DJ AG London

Bien wa Sauti Sol Aibuka na Kuku Hai Katika Show ya DJ AG London

Msanii mashuhuri wa kundi la Sauti Sol, Bien-Aimé Baraza, ameibua mshangao na vicheko mitandaoni baada ya kuonekana akitumbuiza katika onyesho la mtaa la DJ AG maarufu jijini London huku akibeba kuku hai mikononi. Tukio hilo lilifanyika katika eneo la King’s Cross, ambapo DJ AG huandaa matukio ya kipekee ya muziki ya mtaani, yanayopata sifa kwa ubunifu na mvuto wake wa kipekee. Bien sasa amejiunga rasmi na orodha ya watu maarufu waliowahi kushiriki au kuonekana kwenye onesho hilo, akiwemo Ed Sheeran, Will Smith, Rita Ora, Flavour, Demarco, na hivi karibuni Diamond Platnumz. Katika video iliyosambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii, Bien alionekana akicheza kwa hisia na kuimba huku akiwa amembeba kuku – jambo lililowafanya mashabiki washangae, wengine wakicheka, wakitafsiri tukio hilo kama mvuto wa Kiafrika iliyoongeza ladha ya kipekee kwenye burudani hiyo. DJ AG, anayejulikana kwa kuandaa street sets zinazolenga kuonyesha vipaji vya wasanii maarufu pamoja na wachanga, ameendelea kuvutia macho ya dunia kwa namna anavyounganisha muziki, mitandao ya kijamii na utamaduni wa mitaani. Onyesho hilo limeibuka kuwa jukwaa wazi la ubunifu na maonyesho yasiyo na mipaka. Mashabiki wa Bien na kundi la Sauti Sol wamepongeza kitendo hicho kama ishara ya ubunifu wa hali ya juu na utangazaji wa utamaduni wa Kiafrika katikati ya jiji la London. “Bien ni msanii anayeweza kuwasiliana na hisia za watu, na pia ana kipaji cha kuleta vichekesho. Hii ya kuku imeweka historia nyingine kabisa!” aliandika shabiki mmoja kwenye X (zamani Twitter). Kwa sasa, mashabiki wanasubiri kwa hamu kuona ni nani mwingine maarufu atakayejiunga na DJ AG katika street shows zake zijazo

Read More
 Bien Aime Afafanua Msimamo Wake Kuhusu Ndoa ya Wake Wengi

Bien Aime Afafanua Msimamo Wake Kuhusu Ndoa ya Wake Wengi

Mwanamuziki maarufu wa kundi la Sauti Sol, Bien Aime Baraza, amefunguka kuhusu msimamo wake kuhusu ndoa za wake wengi, akisema hana mpango wa kuoa zaidi ya mke mmoja. Akihojiwa kwenye kipindi cha The Breakfast Club, Bien alieleza kuwa licha ya kukulia kwenye familia ya wake wengi, yeye ana mtazamo tofauti. “Ninatoka katika familia ya wake wengi, baba yangu ana watoto kumi kutoka kwa wanawake sita tofauti. Mimi ndiye wa mwisho kati ya hao kumi,” alisema Bien. Bien alisema uzoefu huo wa kifamilia umemfundisha mengi kuhusu mahusiano, na ndio maana amejiwekea msimamo wa kutotaka kuoa wake wengi. Mbali na hayo, Bien pia alisimulia changamoto alizopitia alipokuwa akitafuta kuku hai kwa ajili ya kipindi cha On The Radar kilichorekodiwa New York. Kwa mujibu wa msanii huyo, sheria kali za wanyama katika jiji hilo zilimuweka kwenye wakati mgumu, kwani wauzaji wengi walikataa kumuuzia kuku huyo.  “Nililazimika kuendesha gari kwa zaidi ya saa moja hadi Pennsylvania ili kupata kuku hai. New York ni ngumu sana kwa hilo,” alisema Bien. Kauli hizo zimeendelea kumweka Bien katika uangalizi wa vyombo vya habari, huku mashabiki wakifurahia uwazi wake na uhalisia wa maisha anayoshiriki.

Read More
 BIEN WA SAUTI SOL AWATOLEA UVIVU WANAOKOSOA SERIKALI

BIEN WA SAUTI SOL AWATOLEA UVIVU WANAOKOSOA SERIKALI

Msanii wa Sauti Sol, Bien Aime Baraza ameonekana kuchukizwa na kitendo cha baadhi ya watu kuiombea serikali iweze kufeli kwenye utendaji kazi wake ili wapate maneno ya kuwachamba waliochagua uongozi wa sasa. Kupitia insta story yake kwenye mtandao wa Instagram hitmaker huyo wa “Inauma” amewashangaa wanaoendeleza tabia hiyo mitandaoni kwa kusema kuwa huo ni ushamba uliopitiliza ikizingatiwa kuwa msimu wa siasa ulikamilika. Bien ameenda mbali zaidi na kuwataka wanaoeneza propaganda mtandaoni kuacha kadhia hiyo na badala yake wazipambanie familia zao, kwani zama za kuwazia serikali mabaya zimepitwa na wakati. Bien amekuwa moja kati ya wasanii ambao wamekuwa mstari wa mbele kuzungumzia masuala ya siasa bila uwoga wowote, utakumbuka juzi kati alishinikiza serikali kupunguza bei ya unga wa sima kwa kuwa wakenya wengi wanapitia wakati mgumu kutokana na kupanda kwa gharama ya maisha.

Read More
 CHIKI KURUKA AMKINGIA KIFUA BIEN WA SAUTI SOL KWA MADAI YA KUPANGA UZAZI

CHIKI KURUKA AMKINGIA KIFUA BIEN WA SAUTI SOL KWA MADAI YA KUPANGA UZAZI

Mke wa msanii Bien, Chiki Kuruka amemkingia kifua msanii huyo kutokana na kauli yake ya kutaka kumsaidia kupanga uzazi kwa kukata mshipa wake wa uzazi maarufu vesectomy. Akizungumza na Mpasho mrembo huyo amesema kauli hiyo ilitafsiriwa vibaya na waandishi wa habari kwani Bien alikuwa anajaribu kuwaelimisha wanaume kuhusu umuhimu wa kuwasaidia wake zao kwenye suala la kupanga uzazi. Katika hatua nyingine amekosoa vyombo vya habari kwa kuripoti habari za uwongo dhidi ya mume wake Bien huku akisisitiza haja ya waandishi kuwa mstari wa mbele katika kuzingatia maadili ya uandishi wa habari ikiwemo kuandika habari za ukweli na uhakika kama njia ya kuepusha upotoshaji. Utakumbuka mwezi Julai mwaka huu Bein alinukuliwa akisema yupo tayari kukata mshipa wa uzazi maarufu vasectomy punde atakapo pata watoto na mke wake Chiki Kuruka. Msanii huyo wa Sauti Sol ameenda mbali Zaidi na kusema kwamba upangaji uzazi barani Afrika ni swala ambalo limeachiwa wanawake, hivyo hawezi kumwachia mke wake mzigo huo pekee licha ya wanaume wengi kuogopa kufanyiwa vasectomy.

Read More
 BIEN AFUNGUKA KUHUSU WASANII WA KIGENI KUTUMBUIZA KENYA

BIEN AFUNGUKA KUHUSU WASANII WA KIGENI KUTUMBUIZA KENYA

Msanii wa Sauti Sol Bien Aime Baraza amefunguka kuhusu suala la wasanii wa mataifa mengine kupewa kipau mbele kwenye hafla za kisiasa hapa nchini Kenya. Akipiga stori na Mpasho, Bien amesema wasanii wa kigeni wanapotumbuiza nchini ni faida kwa wasanii wa ndani kwa kuwa wasanii wa Kenya pia hupokea upendo wanaposafiri nje ya nchi. Mkali huyo wa ngoma ya “Inauma” ametaka wasanii wa kigeni kuruhusiwa kutumbuiza nchini bila kubaguliwa huku akiwataka wanaoshinikiza wasanii hao kupigwa marufuku kwenye majukwaa ya muziki nchini kuacha ubinafsi. Katika hatua nyingine amempongeza aliyekuwa msanii wa Sol Generation Crystal Asige kwa kuteuliwa kama Seneta anayewakilisha watu wanaoishi na changamoto ya ulemavu nchini. Bien amemtaja Crystal kama mwanamke mwenye akili sana huku akisema kwamba ana uhakika atawatumikia watu hao kwa uadilifu kwani ni jambo ambalo amekuwa akiliota kwa kipindi kirefu.

Read More