LIL DUVAL APINGA BLAC CHYNA KUINGIZA KSHS. BILLIONI 2.4 KUPITIA ONLYFANS

LIL DUVAL APINGA BLAC CHYNA KUINGIZA KSHS. BILLIONI 2.4 KUPITIA ONLYFANS

Mchekeshaji na Muigizaji Lil Duval ameibuka na kuzungumzia ishu ya Blac Chyna kutengeneza zaidi ya KSh. Bilioni 2.4 kila mwezi mwaka 2021 kwenye mtandao wa OnlyFans. Kupitia mfululizo wa post zake kwenye mitandao ya kijamii, Mchekeshaji huyo amesema huu ni uzushi mtupu na hakuna ukweli wowote. “Siamini kama nyie wote mnaamini Blac Chyna alitengeneza kiasi hicho cha pesa ($20 million) kwa mwezi kupitia OnlyFans. Hapa ndio nafahamu sasa ninyi nyote hamuishi kwenye uhalisia.” aliandika Lil Duval na kucheka kisha kuongeza “Mnaamini kila mnachokiona kwenye vichwa vya habari, na hata hamuulizi. Nimeona Wanawake waki-post na kusema ‘Naweza kuamini’ hii ni ushahidi kwamba nyie wote hamjui ($20 Million) ilivyo. Mmiliki wa OnlyFans ameanika hilo ili kuwapumbaza vichwa vyenu na mfungue akaunti zenu. Namba hazidanganyi, lakini kwa hili wametupanga.” alimalizia Lil Duval.

Read More
 TYGA NA ROB KARDASHIAN WAMCHANA BLAC CHYNA BAADA YA KUSEMA HAPEWI PESA ZA MATUNZO YA WATOTO

TYGA NA ROB KARDASHIAN WAMCHANA BLAC CHYNA BAADA YA KUSEMA HAPEWI PESA ZA MATUNZO YA WATOTO

Rapa kutoka Marekani Tyga pamoja na Rob Kardashian wameamua kwa pamoja kumtolea uvivu Blac Chyna ambaye ni mama wa watoto wao baada ya kusema hadharani kwamba hapewi pesa za matunzo ya watoto na ameamua kuuza magari yake matatu kwa ajili ya kupata pesa za kujikimu. Tyga ambaye ana mtoto mmoja na Chyna (King Cairo Stevenson) alikuwa wa kwanza kuibuka kwenye comment katika post hiyo ya Blac Chyna ambayo imepostiwa kwenye ukurasa wa The Shaderoom Instagram, kwa kuandika ujumbe unaosomeka  “Nalipa ($40K) zaidi ya shilling million 4.6 kwa mwaka kwa ajili ya Ada ya mtoto wangu shule, na ninaishi naye toka Jumatatu hadi Jumamosi. Kwanini nilipe pesa za matunzo ya mtoto.” aliandika Tyga na kumalizia kwa kicheko. Rob Kardashian ambaye pia wamezaa mtoto mmoja (Dream Renèe Kardashian) alikuja na kuacha comment yake isemayo “Nalipa ($37k) zaidi ya shilling million 4.3 za Kenya kwa mwaka kama Ada ya shule ya binti yangu. Ninasimamia gharama zote za matibabu. Nalipa gharama zote za ziada kwa binti yangu. Ninakuwa naye kuanzia Jumanne hadi Jumamosi. Kwanini nilipe pesa ya matunzo ya mtoto.” aliandika Rob Kardashian.

Read More