Bobi Wine Aonya Wasanii Kuhusu Maudhui ya Nyimbo Zao

Bobi Wine Aonya Wasanii Kuhusu Maudhui ya Nyimbo Zao

Msanii nguli wa muziki na mwanasiasa kutoka Uganda, Robert Kyagulanyi almaarufu Bobi Wine, ameonya wasanii wa kizazi kipya kwamba mashairi yasiyo na maadili na yanayokosa maudhui yenye maana huenda yakaathiri urithi wao wa muziki. Bobi Wine, ambaye ana historia ndefu kwenye tasnia ya burudani kabla ya kuingia kwenye siasa, amesema muziki una nafasi kubwa ya kubadilisha jamii na kumbaki kama urithi wa kudumu. Kwa mujibu wake, kazi za sanaa ambazo zinajikita kwenye matusi, udhalilishaji na ujumbe usio na maadili mara nyingi huishia kusahaulika, huku muziki wenye thamani ya kijamii ukibaki kwa vizazi vingi. Mwanasiasa huyo ameeleza kwamba yeye binafsi anajivunia kutumia muziki wake kama chombo cha kuhamasisha jamii na kupigania haki, jambo ambalo limemsaidia kuendelea kukumbukwa kwa miaka mingi. Alisisitiza kuwa vijana wengi wanapenda burudani, lakini ni jukumu la wasanii kuhakikisha muziki wao unachangia kuelimisha na kuboresha jamii badala ya kuathiri vibaya maadili. Bobi Wine amewataka wasanii wa Afrika Mashariki na bara kwa ujumla kuzingatia athari za muziki wao katika maisha ya watu na kufikiria ni urithi upi wanataka kuacha. Kwa sasa, licha ya changamoto za kisiasa na shinikizo analokabiliana nalo nchini Uganda, Bobi Wine anaendelea kutumia jukwaa la muziki na siasa kushinikiza mabadiliko ya kijamii na kisiasa.

Read More
 Bobi Wine Adai Serikali Inatumia Mabwenyenye Kudhibiti Muziki Uganda

Bobi Wine Adai Serikali Inatumia Mabwenyenye Kudhibiti Muziki Uganda

Msanii aliyegeukia siasa, Bobi Wine, ameendelea kutoa maoni yake kuhusu changamoto zinazokumba sekta ya muziki nchini Uganda. Wine, ambaye alijipatia umaarufu mkubwa katika muziki kwa zaidi ya miaka kumi na tano kabla ya kuingia kwenye siasa na hata kuwania urais, anasema sekta hiyo sasa inadhibitiwa na makundi yenye ushawishi makubwa yanayofanya kazi kwa niaba ya serikali. Kwa mujibu wake, serikali inalenga kuhakikisha hakuna msanii mwingine anayeweza kufikia kiwango cha ushawishi alichopata kupitia muziki wake, hivyo kuzuia sanaa kutumika kama chombo cha kuibua sauti za upinzani. Anaeleza kuwa muziki nchini humo umekuwa chombo kinachodhibitiwa kwa karibu, ambapo kila kinachozalishwa studio kinasimamiwa kwa lengo la kudhibiti ujumbe unaofika kwa wananchi. Licha ya kuingia kwenye siasa, Bobi Wine ameendelea kurekodi na kutoa nyimbo, akisisitiza kuwa wasanii wana jukumu la kueleza hali halisi ya jamii. Anawahimiza wanamuziki wenzake kutumia sanaa si tu kwa burudani, bali pia kama jukwaa la kuzungumzia changamoto za kijamii na dhuluma zinazowakumba wananchi. Kauli hizi zinajiri wakati sekta ya muziki nchini Uganda inaendelea kupanuka kibiashara, lakini changamoto za udhibiti wa kisiasa na mashindano ya kifedha kati ya wasanii na serikali zikibaki kuwa kikwazo kikubwa kwa ukuaji wake.

Read More
 “Siwezi kuacha kuvuta bangi,” akiri Irene Kayemba, dada yake Bobi Wine

“Siwezi kuacha kuvuta bangi,” akiri Irene Kayemba, dada yake Bobi Wine

Mwanamuziki na mfanyabiashara Irene Kayemba amekiri wazi kuwa hawezi kuacha kuvuta bangi, akisema ni sehemu ya maisha yake ya kila siku. Kayemba, ambaye pia ni dada wa mwanasiasa mashuhuri Bobi Wine, amesema bangi ni dawa ya asili ambayo imechangia kwa kiasi kikubwa katika afya yake na mwonekano wake. Katika mahojiano ya hivi karibuni, Kayemba anadai matumizi hayo yamezuia kuzeeka kwake mapema na kuyafanya mwili wake uendelee kung’aa. Mrembo huyo ameeleza kuwa mbali na kuitumia binafsi, pia huitumia kutibu wanyama wake wanapougua. “Siwezi kuacha bangi. Ni tiba ya mitishamba. Naweka kwenye chai, na hata naitumia kwa wanyama wangu. Inanisaidia sana, hata muonekano wangu umedumu,” alisema kwa kujiamini. Hata hivyo, aliwataka vijana kuwa waangalifu na matumizi ya kupindukia ya bangi, akieleza kuwa matumizi ya kuvuta moshi wa bangi kwa kiwango kikubwa ni hatari kwa afya, na akashauri itumike kama dawa kupitia njia mbadala kama kunywa kwenye chai. Kauli ya Kayemba imezua mjadala kwenye mitandao ya kijamii kuhusu matumizi ya bangi kama tiba ya asili, huku wengi wakisubiri majibu ya mamlaka husika kuhusu kauli hizo kutoka kwa mtu mashuhuri.

Read More
 Usiwaunge mkono Wanamuziki wanaopinga NUP – Bobi Wine awaambia mashabiki

Usiwaunge mkono Wanamuziki wanaopinga NUP – Bobi Wine awaambia mashabiki

Kinara wa chama cha NUP Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine amewataka mashabiki wake kuwakimbia wasanii wasiounga mkono chama chake cha kisiasa. Kwenye video iliyodakwa na tovuti moja ya habari nchini Uganda, Bobi Wine amesikika akiwataka wafuasi wake kutohudhuria matamasha ya watu wanaowaunga mkono mpinzani wake. “Tafadhali msijihusishe na wale wanaotupinga, msiwaunge mkono kwa namna yoyote kwa sababu ni sehemu ya wakandamizaji wetu. Hatuwezi kuwa marafiki nao wakati wanakutumia kuwakandamiza watu wangu,” alisema. Bobi Wine amehoji kuwa mashabiki kindakindaki wa chama hicho huwa wanaunga mkono shughuli za wanamuziki wanaonesha utii kwa chama cha NUP. “Lakini kwa upande mwingine unapaswa kuwasaidia wale wote wanaotumia sauti na talanta zao kupambana na dhuluma,” aliongeza.

Read More
 BOBI WINE AFUNGUKA KUHUSU UCHAGUZI WA UMA

BOBI WINE AFUNGUKA KUHUSU UCHAGUZI WA UMA

Msanii aliyegeukia siasa Bobi Wine amedai kuwa hana upendeleo kwa mgombea yeyote wa chama cha wanamuziki nchini Uganda UMA kwa kuwa wote ni marafiki zake. Katika mahojiano yake hivi karibuni Bobi Wine amesema wasanii kuwa na chama chao sio kitu kibaya ila serikali inatumia chama cha UMA kuwatengenisha wasanii kwa misingi ya kiasasa. Bobi Wine serikali haina nia ya kuboresha tasnia ya muziki, hivyo imeamua kuwahujumu wasanii ili kusiwahi tokea mtu kama yeye ambaye anatetea haki za wananchi kutoka udhalimu wa watu walio madarakani. Kauli ya Bobi Wine imekuja mara baada ya kuonekana kuegemea upande wa King Saha alipoidhinishwa kugombea urais wa chama cha wanamuziki Uganda uma kwa kutia saini fomu ya kuteuliwa kwake. Ikumbukwe inaripoti kuwa Cindy Sanyu ambaye anagombea urais wa uma ana uhusiano mzuri na serikali ya Yoweri Museveni huku King Saha akionekana kuwa upande wa upinzani unaoongozwa na Bobi Wine.

Read More
 CHAMELEONE AFUNGUKA KUHUSU BIFU YAKE NA BOBI WINE

CHAMELEONE AFUNGUKA KUHUSU BIFU YAKE NA BOBI WINE

Msanii mkongwe nchini Uganda Jose Chameleone amefunguka uhusiano wake na Bobi Wine ambaye wamekuwa kwenye bifu kwa muda mrefu. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Chameleone amesema kwa sasa hana ugomvi wowote na msanii huyo aliyegeukia siasa kwa kuwa alishamsamehe zamani kwa hatua ya kunyima tiketi ya chama chake cha nup wakati alikuwa anawania wadhfa wa umeya wa jiji la kampala. “I have no problem with Bobi Wine and I cleansed my heart for whatever he did. I didn’t get the party ticket but I don’t mind about that anymore.” Amesema. Hitmaker huyo wa Forever ameeleza kuwa hawezi kubali  siasa iharibu uhusiano wake na Bobi Wine ambao wameujenga kwa kipindi kirefu ikizingatiwa kuwa wamekuwa kwenye tasnia ya muziki kwa zaidi ya miaka 20. “I have known Bobi Wine for twenty years and our relationship matters most,” he said in an interview with local television.” Ameongeza Utakumbuka Chameleone na Bobi Wine mara ya mwisho kukutana ilikuwa kwenye birthday party ya mwanamuziki mwenzao Eddy Yaawe ambayo ilifanyika mwezi meo mwaka huu viungani mwa jiji la Kampala.

Read More
 CHAMELEONE NA BOBI WINE WAMALIZA TOFAUTI ZAO

CHAMELEONE NA BOBI WINE WAMALIZA TOFAUTI ZAO

Mastaa wa muziki kutoka Uganda Jose Chameleone na Bobi wine hatimaye wamemaliza ugomvi wao uliodumu kwa kipindi cha miaka miwili. Hii ni baada ya wawili hao kukutana kwenye hafla ya kusherekea kumbukizi ya kuzaliwa kwa mwanamuziki eddy yawe mapema wiki ambapo walipata wasaa mzuri wakuzungumza huku wakionekana wakiwa na nyuso za tabasamu. Taarifa za Bobi wine na Chameleone kumaliza bifu yao imethibitishwa na Eddy Yawe  ambaye ni kaka wa Bob Wine kwa kusema kwamba amefurahishwa na hatua ya wawili wao kuitikia mwaliko wake huku akisisitiza waendelee kuwa marafiki licha ya utofauti wao wa kisiasa. Hata hivyo mashabiki wa muziki nchini Uganda wamewapongeza wawili hao kwa hatua ya kumaliza tofauti zao huku  wakiwataka waachie wimbo wa pamoja utakaothibitisha kuwa wamemaliza ugomvi wao. Utakumbuka  Chameleone aliingia kwenye ugomvi na Bobi Wine mwaka wa 2020 baada ya Bobi Wine kumnyima tiketi ya kuwania kiti cha umeya wa jiji la kampala  kupitia chama cha kisiasa cha NUP. Tangu wakati huo Chameleone amekuwa akimshambulia Bobi Wine pamoja na watu wake wa karibu kwa hatua ya kuwa kizingiti kwenye azma yake ya kuwa mwanasiasa.

Read More
 BOBI WINE APENDEKEZA HISTORIA YA MWANAMUZIKI MOZEY RADIO IJUMUISHWE KWENYE MTAALA WA MASOMO NCHINI UGANDA

BOBI WINE APENDEKEZA HISTORIA YA MWANAMUZIKI MOZEY RADIO IJUMUISHWE KWENYE MTAALA WA MASOMO NCHINI UGANDA

Mwanamuziki aliyegeukia siasa Bobi Wine ameibuka na kudai kuwa anatamani historia ya mwanamuziki Mozey Radio ijumuishwe kwenye mtaala wa shule za upili na msingi nchini Uganda. Kulingana na Bobi Wine, kizazi cha sasa na kijacho kitapata fursa ya kujifunza mengi kuhusu maisha ya mwendazake Radio ambaye ni mwanamuziki wa muda wote kuwahi kutokea nchini uganda kutokana na kipaji cha kipekee alichokuwa nacho kipindi cha uhai wake. Bobi Wine amesema utawala wa sasa nchini Uganda unaogopa kuwapa nafasi wanafunzi mashuleni kujifunza kuhusu maisha ya mwanamuziki Mozey Radio kwa  sababu wana hofu ya kuikuza kizazi kitakachopinga udhalimu unaoendelezwa serikali. Hata hivyo amesema akishika hatamu ya uongozini miaka zijazo atawatangaza hadharani wanamuziki Mozey Radio na Herman Basude kama mashujaa wa tasnia ya muziki nchini uganda.

Read More