BOOMPLAY WAINGIA MKATABA NA TELKOM KENYA KURAHISISHA HUDUMA ZA KUSTREAM MUZIKI

BOOMPLAY WAINGIA MKATABA NA TELKOM KENYA KURAHISISHA HUDUMA ZA KUSTREAM MUZIKI

Mtandao wa Boomplay umeingia ubia wa kufanya kazi na kampuni ya mawasiliano ya Telkom Kenya kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa huduma za kustream muziki miongoni mwa wakenya. Ushirikiano huo ambao utatoa nafasi kwa wakenya kupata huduma ya kupakua na kusikiliza muziki katika app ya Boomplay kwa urahisi, inakuja na vifurushi mbali mbali ambazo zitawezesha watumiaji wa telkom kusikiliza zaidi ya nyimbo millioni 75 za humu na kimataifa kwa shillingi 299 kwa mwezi. Vifurushi hivyo pia vitatoa fursa kwa watumiaji wa Telkom kusikiliza muziki usiokuwa na matangazo lakini pia kupakua muziki bila kikomo kutoka kwa wasanii kama Otile Brown, Khaligraph Jones, Nadia Mukami, Nikita Kering na wengine wengi. Packages zitakazozinduliwa ni pamoja na ya shilllingi 49 kwa siku, shillingi 159 kwa wiki na shilling 299 kwa mwezi, virushi ambavyo vitakuwa vinakata mjazo wa watumiaji wa Telkom.

Read More
 BAHATI APEWA TUZO BOOMPLAY

BAHATI APEWA TUZO BOOMPLAY

Nyota wa muziki nchini Bahati ametunukiwa tuzo ya silver Plaque na mtandao wa kupakua na kusikiliza muziki wa boomplay Kenya. Hii ni baada hitmaker huyo wa “Pete yangu” kufikisha zaidi ya streams millioni 8 kupitia nyimbo zake zote zilizopakiwa kwenye mtandao  huo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram bahati amewashukuru mashabiki zake kwa kuendelea kufuatilia kazi zake ambazo zinazidi kuonyesha mafanikio makubwa ndani na nje ya Kenya. Tuzo hizo maarufu kama ‘Boomplay Plaques’ hutolewa kutambua jitihada za wasanii wanaofanya vizuri kwenye App ya Boomplay.

Read More
 STREAMS ZA BOOMPLAY KUHESABIKA BILLBOARD

STREAMS ZA BOOMPLAY KUHESABIKA BILLBOARD

App namba moja ya kupakua na kusikiliza muziki Afrika,Boomplay imefanikiwa kuingiza kazi za wasanii katika chati za Billboard kama sehemu yake ya kuendelea kusaidia tasnia ya muziki wa Afrika kutanua wigo wake kamili. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa umma na Kampuni ya Transsnet Music Limited ambayo ndiyo inayomiliki Programu tumuishi (App) ya Boomplay,  itaanza kuingiza kazi za wasanii katika chati maarufu za Billboard Hot 100, Billboard 200, Artist 100 na Billboard Global 200, na pia chati zingine zote za Billboard Marekani na kimataifa ambazo zinajumuisha kazi za kupakua na kusikiliza muziki. Aidha, pamoja na mamilioni ya nyimbo za Kiafrika kusikilizwa kupitia programu hiyo duniani kote, kujumuishwa kwa taarifa za Boomplay katika chati hizo kubwa za muziki kunawapa wasanii wa Kiafrika na Kimataifa fursa ya kuonekana zaidi kwenye majukwaa makubwa duniani. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, ndani ya jukwaa la Music Connect la MRC Data, kazi za Boomplay zitajumuishwa kwenye kapu moja la takwimu linalojumuisha mahitaji ya sauti na picha ambapo picha zimeanza kuonekana kuanzia Oktoba 12, 2021 na miito Oktoba 8, 2021. Streams za Boomplay ziliizoingizwa kwenye chati za Billboard zinawakilisha streams kutoka kwa wasikilizaji waliojisaliji kawaida na wale wa kulipia huku kila stream kutoka kwa msikilizaji wa kundi husika vikipimwa kwa uzito wake.

Read More