MSANII WA BONGOFLEVA HARMONIZE AKANUSHA KUWA SINGLE

MSANII WA BONGOFLEVA HARMONIZE AKANUSHA KUWA SINGLE

Baada ya kuchukua headlines siku ya jana kwa kuelezea kuwa hana mpenzi mwanamuziki wa Bongofleva Harmonize ameibuka kukanusha taarifa hizo ambazo zilienea kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii. Kupitia insta story yake kwenye mtandao wa Instagram mkali huyo wa ngoma ya Teacher’ ameandika ujumbe wa kukanusha taarifa hizo ,huku akitaka kuheshimiwa akiambatanisha na emoji za kucheka, jambo ambalo limetafsiriwa kama alikuwa anatafuta kuongelewa (kiki) Januari 22 mwaka huu  Harmonize aliibuka  kupitia mfululizo wa post zake kwenye insta story yake kusema kuwa haamini kama yupo singo tena. Haikuishia hapo alienda mbali na kuandika ujumbe ambao uliohisiwa kumlenga moja kwa moja mchumba wake Briana kwa kusema tuonane nikifikisha umri wa miaka 35 labda nina umri wa miaka. Hata hivyo Harmonize walimwengu kwenye mitandao ya kijamii walihoji kuwa huenda penzi la mwanamuziki na C.E.O.wa KondeGang Harmonize na mpenzi wake mzungu raia wa Australia Briana limevunjika. Ikumbukwe kuwa penzi la Harmonize na Briana lilianza rasmi mwishoni mwa mwaka jana miezi kadhaa baada ya kuachana na aliyekua mpenzi wake Fridah Kajala.

Read More
 PENZI LA HARMONIZE NA BRIANA LAINGIWA NA UKUNGU,HARMONIZE ATANGAZA KUWA SINGLE

PENZI LA HARMONIZE NA BRIANA LAINGIWA NA UKUNGU,HARMONIZE ATANGAZA KUWA SINGLE

Huenda penzi la mwanamuziki na C.E.O.wa KondeGang Harmonize na mpenzi wake mzungu raia wa Australia Briana limevunjika. Kulingana na mfululizo wa post zake kupitia insta story yake kwenye mtandao wa instagram harmonize amesema kuwa haamini kama yupo singo tena. Haikuishia hapo ameenda mbali na kuandika ujumbe ambao unahisiwakumlenga moja kwa moja mchumba wake Briana kwa kusema tuonane nikifikisha umri wa miaka 35 labda nina umri wa miaka. Hata hivyo Harmonize hajatoa maelezo zaidi kuhusu kiini cha uhusiano wake na Briana kuvunjika  ila walimwengu kwenye mitandao ya kijamii wamehoji kuwa huenda msanii huyo wa Bongofleva anatengeza  mazingira ya kumzungumziwa Afrika Mahariki kabla ya ujio wa ngoma yake mpya Ikumbukwe kuwa penzi la Harmonize na Briana lilianza rasmi mwishoni mwa mwaka jana miezi kadhaa baada ya kuachana na aliyekua mpenzi wake Fridah Kajala. Mbali na hayo mwanamuziki huyo ametangaza kuachia wimbo wake mpya siku ya kesho unaitwa ‘Mwaka Wangu’

Read More
 BRIANA AMTOA HARMONIZE KWENYE ULIMWENGU WA ANDROID

BRIANA AMTOA HARMONIZE KWENYE ULIMWENGU WA ANDROID

Mpenzi wa Harmonize, Briana amemzawadi bosi huyo wa lebo ya muziki ya Konde Gang Worldwide simu aina ya i-Phone 13. Harmonize amethibitisha hilo kupitia InstaStory yake kwenye mtandao wa Instagram ambapo ameonyesha kuanza kutumia simu aina iphone kwa mara ya kwanza.  Hitmaker huyo wa “Teacher” amempongeza mpenzi wake mpya Briana kwa kusema kwamba amekuwa chachu ya yeye kuanza kutumia simu hiyo aina ya iphone 13 kutoka kwenye ulimwengu wa Android ambao amekuwa akitumia siku zote. Ikumbukwe Briana kutoka Australia anakuwa mwanamke wa pili mwenye asili ya kizungu kuwa kwenye mahusiano na Harmonize, kwani awali alikuwa kwenye ndoa na Sarah Michelloti kutoka Italia kabla ya ndoa yao kuvunjika.

Read More