Britney Spears Asema Aliwekewa Vizuwizi vya Kingono Wakati wa Uangalizi wa Kisheria

Britney Spears Asema Aliwekewa Vizuwizi vya Kingono Wakati wa Uangalizi wa Kisheria

Malkia wa muziki wa pop, Britney Spears, ameibua hali ya sintofahamu mitandaoni baada ya kufichua madai ya kushtua kuhusu kile alichopitia wakati wa kipindi cha conservatorship (uangalizi wa sheria) kilichodumu kwa zaidi ya miaka 13. Kupitia chapisho kwenye mitandao ya kijamii, Britney alidai kwamba alilazimishwa kuvaa nguo za ndani zenye tabaka tatu ili kumzuia kufanya mapenzi, jambo ambalo limezua hisia kali na uvumi kwamba huenda alinyimwa uhuru wa msingi wa kibinadamu. “Walihakikisha sifanyi chochote. Hata kuwa na faragha kama mwanamke ilikuwa ndoto. Nililazimishwa kuvaa tabaka tatu za ‘tights’ ili nisiweze kushiriki tendo la ndoa,” aliandika Britney. Madai haya yamezua maswali mengi kuhusu namna alivyokuwa akitendewa wakati wa ule uangalizi wa sheria, uliokuwa ukisimamiwa na baba yake, Jamie Spears, pamoja na timu yake ya kisheria. Mashabiki na watetezi wa haki za binadamu wamelaani vikali kile kinachotajwa kama unyanyasaji wa hali ya juu dhidi ya mwanamke mtu mzima. Wafuasi wa harakati za #FreeBritney wameeleza masikitiko yao makubwa na kushinikiza kufanyika kwa uchunguzi wa kina ili kuwawajibisha wote waliokuwa wakimnyanyasa msanii huyo. Hadi sasa, upande wa Jamie Spears haujatoa tamko rasmi kuhusu tuhuma hizi mpya. Hata hivyo, shinikizo kutoka kwa umma linaendelea kuongezeka, huku wengi wakisema ni wakati wa haki kutendeka.

Read More
 Britney Spears Afunguka Baada ya Sakata la Ndege

Britney Spears Afunguka Baada ya Sakata la Ndege

Mwanamuziki nyota wa Marekani, Britney Spears, hatimaye amezungumzia tukio lililoripotiwa kuhusu madai ya kukaidi maagizo ya kuacha kuvuta sigara akiwa ndani ya ndege. Kupitia chapisho aliloweka kwenye ukurasa wake wa Instagram, Spears ameelezea hali halisi ya kilichotokea, huku akikanusha kwa ucheshi madai ya kusababisha usumbufu, ambayo yamesambaa sana kwenye mitandao ya kijamii. Katika maelezo yake, Spears amesimulia kwa mtindo wa mzaha kuwa ilikuwa mara yake ya kwanza kunywa pombe aina ya vodka, jambo ambalo lilimfanya ahisi msisimko wa kipekee. Ameongeza kuwa alishangazwa na namna viti vya ndege hiyo vilivyokuwa na sehemu za kuweka vinywaji upande wa nje, tofauti na ilivyozoeleka. β€œMe yesterday!!! It’s actually incredibly funny!!! Some planes I’ve been on you can’t smoke mostly but this one was different because the drink holders were on outside of seat!!! Confession it was my first time drinking VODKA!!! I swear I felt so SMART.” Aliandika. Kauli hiyo imekuja baada ya vyombo vya habari kuripoti kuwa Spears alipuuza maelekezo ya wahudumu wa ndege waliomtaka azime sigara. Hata hivyo, kwa mtindo wake wa kipekee, alichagua kutoa ufafanuzi kwa njia ya ucheshi na simulizi ya kibinafsi. Chapisho hilo limezua hisia tofauti miongoni mwa mashabiki wake. Wapo waliomtetea kwa kusema kuwa kila mtu hukosea mara moja moja, huku wengine wakieleza wasiwasi wao kuhusu tabia hiyo, hasa kwa mtu mwenye ushawishi mkubwa kama yeye. Hadi sasa, haijafahamika ikiwa tukio hilo litachukuliwa kama ukiukwaji wa sheria za usalama wa anga, lakini Spears anaonekana kulichukulia kwa wepesi na bashasha kama ilivyo kawaida yake.

Read More
 MUME WA ZAMANI WA BRITNEY SPEARS ASHTAKIWA KWA KUZUA VURUGU

MUME WA ZAMANI WA BRITNEY SPEARS ASHTAKIWA KWA KUZUA VURUGU

Mume wa zamani wa mwanamuziki Britney Spears ameshtakiwa kwa kosa la kujitokeza bila taarifa wala kualikwa wakati wa harusi ya nyota huyo na Sam Asghari ambaye ni mume wake kwa sasa baada ya kufunga harusi. Jason Alexander, mwenye umri wa miaka 40, alikana shtaka hilo, pamoja na kuingia bila kibali, kutumia nguvu na kuharibu mali. Alikamatwa wiki iliyopita baada ya kudaiwa kugonga geti na kutoa video kutoka ndani ya nyumba ya Spears. Bwana Alexander alimuoa Britney Spears ambaye alikuwa rafiki wa utotoni mwaka wa 2004 lakini ndoa yao ilidumu kwa kipindi cha chini ya siku tatu.

Read More