Bruno K amjibu msanii Byg Ben kuhusu ukabila kwenye muziki Uganda

Bruno K amjibu msanii Byg Ben kuhusu ukabila kwenye muziki Uganda

Msanii Bruno K ametofautiana kimawazo na msanii chipukizi Byg Ben aliyedai kuwa ni vigumu kwa wasanii wasioimba nyimbo kwa lugha ya luganda kufanikiwa kisanaa nchini Uganda kutokana na ubaguzi wa kikabila uliokithiri nchini humo. Kupitia mitandao yake ya kijamii amemtaka msanii huyo kutia bidii kwenye kazi zake badala ya kutoa malalamiko yasiokuwa na msingi kwani mashabiki watamuunga mkono akitoa muziki mzuri. “Bro acha kutoa visingizio. Watu nchini Uganda watakuunga mkono bila kujali kabila lako. Wape tu muziki mzuri,” Bruno K aliandika Twitter.

Read More
 BRUNO K NA BINTIYE BRIELLA WALAMBA SHAVU LA UBALOZI IMPERIAL LEATHER UGANDA

BRUNO K NA BINTIYE BRIELLA WALAMBA SHAVU LA UBALOZI IMPERIAL LEATHER UGANDA

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Bruno K pamoja na binti yake Briella wamelamba dili nono la ubalozi wa kampuni ya Imperial Leather. Bruno K amethibitisha taarifa hiyo njema kwa mashabiki zake kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kushare baadhi ya picha zikiwaonyesha wakitia sahihi mkataba wa maelewano na uongozi wa kampuni ya Imperial Leather. Hata hivyo mashabiki na mastaa mbali mbali nchini Uganda wameonekana kumpongeza Bruno K pamoja na mwanae Briella kwa mafanikio hayo makubwa maishani huku baadhi wakimponda msanii huyo kwa kumtumia vibaya binti yake kujipatia pesa wakati huu angali mdogo. Ikumbukwe mwezi mmoja uliopita Bruno K alimpoteza baby mama wake Rachel Nasasira baada ya kuagua kwa muda mrefu. Baada ya kifo chake kulikuwa na ripoti kuwa msanii huyo alikatazwa kumchukua binti yake Briella kutokana na hatua ya kumtelekeza baby mama wake akiwa hai. Lakini baadae alifanikiwa kumtorosha binti yake kutoka kwa mama ya mke wake kitu ambacho kiliibua mzozo mkali kati yake na familia ya baby mama wake wa wakimtuhumu kwa hatua ya kumrubuni mtoto huyo bila ya ridhaa yao.

Read More
 OSCAR ADAI BRUNO K ALIKIMBIA NA PESA ZOTE WALIZOPOKEA KUTOKA KWA WAHISANI

OSCAR ADAI BRUNO K ALIKIMBIA NA PESA ZOTE WALIZOPOKEA KUTOKA KWA WAHISANI

Siku chache  zilizopita msanii Bruno K alimtoa mwimbaji wa zamani wa Bigtym, Oscar kutoka kwenye lindi la umaskini. Hitmaker huyo wa Omulwa alimchuka msanii huyo na akaanza kumpa support, huku akiongoza kampeni ya kufufua kipaji  chake cha muziki ambacho kilikuwa kimefifia. Sasa  baada ya Oscar kupata afueni ameibuka na kumshutumu vikali Bruno K kwa madai ya kutogawa kwa usawa pesa walizopokea kutoka kwa wasamaria wema. Msanii huyo amehoji ni kwa nini Bruno K mwanzo alikuwa anajifanya anajali sana ilhali alikuwa na ajenda zake za kujinufaisha kupitia jina lake. Hata hivyo Oscar ametoa changamoto kwa Bruno k kuonyesha namna pesa walizopokea kutoka kwa waganda na makampuni mbalimbali ilivyotumika.

Read More