Bruno K amjibu msanii Byg Ben kuhusu ukabila kwenye muziki Uganda
Msanii Bruno K ametofautiana kimawazo na msanii chipukizi Byg Ben aliyedai kuwa ni vigumu kwa wasanii wasioimba nyimbo kwa lugha ya luganda kufanikiwa kisanaa nchini Uganda kutokana na ubaguzi wa kikabila uliokithiri nchini humo. Kupitia mitandao yake ya kijamii amemtaka msanii huyo kutia bidii kwenye kazi zake badala ya kutoa malalamiko yasiokuwa na msingi kwani mashabiki watamuunga mkono akitoa muziki mzuri. “Bro acha kutoa visingizio. Watu nchini Uganda watakuunga mkono bila kujali kabila lako. Wape tu muziki mzuri,” Bruno K aliandika Twitter.
Read More