Butita Atoa Wito wa Umoja Katika Hafla za Kitamaduni za Waluya

Butita Atoa Wito wa Umoja Katika Hafla za Kitamaduni za Waluya

Mchekeshaji, Eddie Butita, amesikitishwa na migawanyiko katika hafla za kitamaduni za jamii ya Waluya, akitoa wito kwa jamii hiyo kuungana na kuandaa tamasha moja kubwa badala ya kuwa na hafla nyingi zilizotawanyika. Akizungumza kupitia akaunti yake ya Instagram, Butita amehoji umuhimu wa kuwa na sherehe nyingi na kusema kwamba jamii hiyo haijawahi kuwa na tukio hata moja lililowahi kufanikiwa kutokana ukosefu wa umoja. Mchekeshaji huyo ambaye pia ni bosi wa SPM Buzz, amebainisha kuwa utengano wa hafla hizi unadhoofisha athari za kitamaduni za jamii, na kuwaleta watu pamoja chini ya sherehe moja kuu, kutatoa sauti yenye nguvu zaidi kwa utambulisho wa Waluya katika ngazi ya kitaifa. Aidha, Butita ametoa changamoto kwa promoters wa sherehe za kitamaduni kuchukulia jambo hilo kwa uzito na kuanza kupanga tukio moja kubwa litakalowakilisha jamii nzima. Watu wengi mitandaoni wameeleza kuwa hoja ya Butita inafungua mjadala kuhusu umuhimu wa kuunganisha tamaduni za Waluya na kuimarisha ushawishi wake katika masuala ya kitaifa.

Read More
 Butita Amkingia Kifua Flaqo Kufuatia Skit Yenye Utata

Butita Amkingia Kifua Flaqo Kufuatia Skit Yenye Utata

Mchekeshaji na mtayarishaji wa maudhui nchini Kenya, Eddie Butita, amejiunga na mjadala ulioibuka kufuatia skiti ya hivi karibuni ya Flaqo inayodaiwa kuwalenga wafanyi biashara wa forex wanaodaiwa kuwa utajiri wao unatokana na biashara ya ushoga au mahusiano ya jinsia moja. Kupitia mitandao yake ya kijamii Butita alisisitiza kuwa katika skiti hiyo, Flaqo hakumtaja mtu yeyote moja kwa moja, jambo linalomfanya ashangae ni kwa nini baadhi ya watu wanajihisi kushambuliwa ikiwa kweli hawahusiki na masuala yaliyoigizwa. Aliongeza kuwa sanaa na ucheshi huwa na jukumu la kuibua mijadala na kutoa nafasi ya jamii kujitazama kwenye kioo. Skiti hiyo ya Flaqo imezua mjadala mkali mitandaoni, ambapo baadhi ya wafuasi wake wamejitokeza kumtetea wakisema ni kazi ya kisanii inayotumia kejeli na utani kufichua uhalisia wa maisha, huku wakosoaji wakidai kuwa kugusia masuala yenye utata kama biashara ya “Sim2” au Ushoga ni kukiuka maadili na heshima, na kwamba inaweza kuathiri heshima ya sekta nyingine kama forex trading. Mjadala huu unaonekana kugawanya maoni ya umma, huku wengine wakisisitiza umuhimu wa uhuru wa ubunifu na wengine wakitaka wasanii kuwa makini wanapogusia mada nyeti zinazoweza kuibua hisia kali katika jamii.

Read More